test man
JF-Expert Member
- Aug 13, 2016
- 1,014
- 970
Jamani kuweni makini na matapeli leo wamenipiga sh 10,000 nimetuma mwenyewe ishu iko hivi, nilipigiwa simu namb ngeni ya vod mida saa nne asbh akajitambulisha kuwa customers care vodacom, kuwa Kuna mteja hapa anaitwa wilfrida Nelson ametuma hela kwa makosa kwako sh 17,000 kama umepata huo muamala tuambie mm nikamwambia kama upo vodacom customers care kwann usirudishe huo muamala kwa mwenyewe akasema hata ww unaweza kutusaidia samahani lkn, kidgo meseji ikaingia kutoka Voda M-Pesa kuwa nimepokea sh 17,000 kutoka kwa huyo wilfrida, Muda huo bado naongea na huyu customers care fake, nikamwambia nimeiona hiyo meseji akasema ahsante tunaomb imurudishie hela yake tuma hata sh 10,000 nyingn iwe makato nikamwambia pw na Muda huo ni kweli meseji ya M-Pesa, anakata tu huyu wilfrida kanipigia anataka hadi kulia samahani nimekosea kutuma hela imekuja kwako nikamwambia pole ngoja nikutumie nimeambiwa, sasa kumbe Muda huo naongea na wilfrida huyu jamaa karudisha huo muamala kwao mm haraka haraka nikamtumie huyu dada sh 10,000 salio kurudi nimebakia na sh 350 daaah kuwapigia simu haipatikani nikatuma meseji inapokelewa lkn wahajibu nami nikakimbilia karudisha muamala kuingiza hizo namb naambiwa huyu mtu tayar ameshaitumia hela nimekasirika kweli hapo nikakubali nimepigwa nikafuta hadi namb zao sikutaka hata kuziona nikaakimya nikaona niwape taadhari wadau huo ndo wizi mpya wa matapeli mtandaoni chonde chonde usikubali kurudisha muamala wa hela ambayo mtu amekosea.


