Shinto
JF-Expert Member
- Dec 6, 2010
- 1,781
- 96
Wakati hakuna anayeelewa kwa undani maana halisi ya " kujivua magamba" labda wana CCM wenyewe waliokaribu na CC, kilichowazi ni kuwa CCM imekubali kuwa chama chao kiligubikwa na tuhuma za ufisadi au kulikuwa na ufisadi wa kupanga kweli ndani ya chama.
Hii ni hatua nzuri na ni ukomavu wa kisiasa. Si wengi miongoni mwetu wana ujasiri wa kukiri hadharani mapungufu yao! Ukiondoa wanafiki!
Nadhani hii iwe changamoto kwa vyama na taasisi nyingine kujipima na kukiri makosa yao au mapungufu yao! Huku ni kujiimarisha si kujidhoofisha kama wengi humu wanvyodhani.
Ni wakati sasa Chadema nayo iangalie kwa kina shutuma zinazoelekezwa dhidi yake, hususani Udini, Ukabila,Ukanda na Umangimeza kwenye uongozi wa kitaifa wa chama hicho!
Kufumbia macho hayo ni kukidhoofisha chama chenu, acheni kujidanganya!
Hii ni hatua nzuri na ni ukomavu wa kisiasa. Si wengi miongoni mwetu wana ujasiri wa kukiri hadharani mapungufu yao! Ukiondoa wanafiki!
Nadhani hii iwe changamoto kwa vyama na taasisi nyingine kujipima na kukiri makosa yao au mapungufu yao! Huku ni kujiimarisha si kujidhoofisha kama wengi humu wanvyodhani.
Ni wakati sasa Chadema nayo iangalie kwa kina shutuma zinazoelekezwa dhidi yake, hususani Udini, Ukabila,Ukanda na Umangimeza kwenye uongozi wa kitaifa wa chama hicho!
Kufumbia macho hayo ni kukidhoofisha chama chenu, acheni kujidanganya!