Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,860
- 12,291
Ndugu zangu imezoeleka katika dunia ya leo kila mtu kutumia uongo na unafiki kufanya siasa nchini kwake. Njia hii ya uongo na unafiki imekuwa njia nzuri na yenye mafanikio ya haraka kwa wanasiasa hao.
Mfano tumeona wanasiasa mbali mbali duniani wakitumia uongo na unafiki kuvuna wanachama wengi mbumbumbu wasiojielewa na hata wachache wanaojielewa, tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki kurubuni wapiga kura na hatimae kupigiwa kura
Tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki kutafuna mamilioni ya ruzuku za vyama vyao ambazo zinatokana na kodi za wananchi tajiri na masikini
Tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki katika mikutano mbali mbali ya chama, iwe ya ndani au nje kukusanya michango kutoka kwa wananchi masikini na kugawanwa na wajanja wachache ndani ya chama husika.
Wakati hayo yakifanyika, wale wanaodanganywa ambao ni wananchi wa kawaida huishia kuumia rohoni kwa kupewa ahadi zisizotekelezwa. Katika style hii ya uongo na unafiki, wanasiasa wengi hutumia njia mbali mbali kuficha uongo na unafiki wao ili kuendelea kuwarubuni wadanganywa.
Lakini kwa viongozi wa Chadema kwao ni tofauti. Kila uongo na unafiki wao waliuweka hadharani ili wale wanaowaunga mkono waamue wenyewe, aidha waendelee kuwaunga mkono ili wawadanganye zaidi au waachane nao na kuendelea na mishe zingine za kujitafutia riziki kupitia akili zao, nguvu zao, mikono yao na maarifa yao.
Dunia hii mtu kuwa muongo na mnafiki halafu kuuweka hadharani uongo na unafiki wako sio jambo la mchezo. Pongeza kubwa kwa Chadema na wanachadema kwa kuupokea na kuukubali uongo na unafiki wote unaoletwa na viongozi wao wa juu bila kuhoji wala kuuliza chochote.
Mfano tumeona wanasiasa mbali mbali duniani wakitumia uongo na unafiki kuvuna wanachama wengi mbumbumbu wasiojielewa na hata wachache wanaojielewa, tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki kurubuni wapiga kura na hatimae kupigiwa kura
Tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki kutafuna mamilioni ya ruzuku za vyama vyao ambazo zinatokana na kodi za wananchi tajiri na masikini
Tumeona wanasiasa hao wakitumia uongo na unafiki katika mikutano mbali mbali ya chama, iwe ya ndani au nje kukusanya michango kutoka kwa wananchi masikini na kugawanwa na wajanja wachache ndani ya chama husika.
Wakati hayo yakifanyika, wale wanaodanganywa ambao ni wananchi wa kawaida huishia kuumia rohoni kwa kupewa ahadi zisizotekelezwa. Katika style hii ya uongo na unafiki, wanasiasa wengi hutumia njia mbali mbali kuficha uongo na unafiki wao ili kuendelea kuwarubuni wadanganywa.
Lakini kwa viongozi wa Chadema kwao ni tofauti. Kila uongo na unafiki wao waliuweka hadharani ili wale wanaowaunga mkono waamue wenyewe, aidha waendelee kuwaunga mkono ili wawadanganye zaidi au waachane nao na kuendelea na mishe zingine za kujitafutia riziki kupitia akili zao, nguvu zao, mikono yao na maarifa yao.
Dunia hii mtu kuwa muongo na mnafiki halafu kuuweka hadharani uongo na unafiki wako sio jambo la mchezo. Pongeza kubwa kwa Chadema na wanachadema kwa kuupokea na kuukubali uongo na unafiki wote unaoletwa na viongozi wao wa juu bila kuhoji wala kuuliza chochote.