Mbunge wa viti maalum Susan Kiwanga wa Kilombero kama sijakosea jina, amekesha stand ya Moro baada ya basi alimokuwemo kuzuiwa kuendelea na safari ya kuelekea Dar kutokana kufika Moro saa 5:00 usiku. Japokuwa mbunge angeweza kuchukua chumba cha kulala katika nyumba za wageni zilizopo karibu na stand lakini hakufanya hivyo na badala yake usiku huo aliutumia kutoa elimu kwa baadhi ya wasafiri walioonekana kuguswa na kitendo chake hicho cha kujichanganya na watu wa tabaka la chini la watanzania mpaka saa 12: 00 asubuhi muda ulioruhusu basi kuendelea na safari ya Dar, kitendo ambacho ni nadra sana kufanywa na wabunge wa CCM. Peoples...........