Kwa hili la Ben, CCM wasikose utu

Kwa hili la Ben, CCM wasikose utu

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,357
Reaction score
100,372
Nawapongeza baadhi ya Wana CCM walioguswa na kutoweka kwa Ndugu Saanane, naamini sio kwamba ni kwa sababu wanamfahamu pengine lah ila kwasababu Ben ni binadamu kama Wewe na Mimi.

Hata hivyo nimeshangazwa na kuumizwa na asilimia kubwa sana ya baadhi ya Wafuasi, Makada na Wapenzi wa CCM wakifurahia au kuonyesha kufurahia kutoweka kwa Binadamu mwenzao. Nichukue fursa hii kwamba hakuna MTU mwenye damu ya chama, dini ya chama wala uhai wa chama. Sisi wote tunabaki kuwa ndugu, Leo hii tukifurahia baya la Ben kisa tu sio "mwenzetu" kesho tutafutwa machozi na nani??? Ben ni mdhambi kiasi gani cha kustahili dhihaka hizi za Wafuasi hawa???

Yamemkuta Ben Leo, hatujui yuko hai ama lah! Vyovyote vile lazima tusikubali au kuruhusu itikadi na mapenzi yetu ya vyama yatufikishe hapa. Wanetu watarithi nini? Chuki? Ubaguzi? Kamwe hatutabaki Salama, siasa zitapita Bali maisha yetu na undugu wetu utabaki hata baada ya vizazi na vizazi.

Naomba labda kwa namna ile ile ambayo tulilaani wale walioshangilia mauaji ya Polisi wetu kipindi kile hivyo hivyo tulaani na wana CCM hawa wachache wa mitandaonj Wanaona ni sawa kwa Ben kutoweashwa.

Kama yametokea kwa Ben na tukachekelea usisahau kuwa yanaweza kutokea kwako au kwangu pia. Ben ana ndugu, ana Marafiki, ana majirani ana damu na mwili kama wako na wangu. Ya Mungu mengi, nani anaifahamu kesho yake??

Kama Wewe unafanya hayo kwakua Uko chini ya mwamvuli wa chama Fulani basi jua wazi kuwa hayo hayo yatakuja kukupata au kuwapata ndugu zako hata baada ya Wewe kuondoka. Maumivu na vidonda hivi tunavyowasababishia wengine basi Mungu ni mwaminifu sana na hajawahi kushindwa, atalipa muda ukifika.

Tunakuombea Ben huko uliko!¡
 
Kuna watu wanashangilia utadhani wao wana mkataba wa kuto kufa. Hivi ndivyo tunavyoishi. Kwamba msiba ukitokea huko wa huku wanashangilia.
Kuna mahali watu waneacha kuzikana. Wala kununua bidhaa kwenye maduka ya mahasimu wao. Ndiko tunapokwenda.
Maana dhihaka hizi zinaacha vidonda kwa waliobaki ambao wanatekeleza kwa kulipa kisasi vile wanaweza. Jee ndiyo utanzania huo???????
 
Kuna watu wanashangilia utadhani wao wana mkataba wa kuto kufa. Hivi ndivyo tunavyoishi. Kwamba msiba ukitokea huko wa huku wanashangilia.
Kuna mahali watu waneacha kuzikana. Wala kununua bidhaa kwenye maduka ya mahasimu wao. Ndiko tunapokwenda.
Maana dhihaka hizi zinaacha vidonda kwa waliobaki ambao wanatekeleza kwa kulipa kisasi vile wanaweza. Jee ndiyo utanzania huo???????


Mkuu, kwani amekufa? Imekua confirmed.
 
Wameji milikisha nchi na kujiona ni viongozi
wenye nguvu na uwezo kuliko MUNGU. Ila kila jambo lina mwisho wake. Ipo siku
 
Ok
Haijawa confirmed Lakini ukifatilia yanayozungumzwa na watu humu yanakera sana. Baadhi
Ok, ni kweli inatia mashaka. Ila kwa lolote linalo endelea juu yake lazima kuna mkono wa dola.
 
Ben si ndie huyu alieitisha serikali isipomtoa CDF ndani ya siku saba ataifanyia kitu mbaya
 
mm wananishughulisha zaidi wale maiti saba,walikufaje wote kwa pamoja na kufungwa mawe.
Kuna kitu nataka niseme lakini roho yangu inasita saaaana, ila naamini hicho ninachokiamini huenda kikawa na ukweli flani.
 
Amejijibu mwenyewe kwa kujiteka. Jeuri yote ile ya kumkebehi Rais, leo anatafutwa na wazazi wake? Yaani kama watoto wakienda kucheza, jioni wazazi wao wanawatafuta waende kuoga, kula na kulala. Tough online, childish at home[emoji23][emoji23]
Ndio Watanzania hawa
 
Acheni upumbavu wenu kama Taifa tuna mambo mengi sana yakufikiria sio kuwaza siasa zenu za majitaka zakujiteka ili mpate kiki Nyumbu mnasumbua sana
 
Kama polisi hawajui, na tiss hawanar, basi ccm wanajua
 
Back
Top Bottom