Kwa hali hii ni uoga na kutokujiamini

Kwa hali hii ni uoga na kutokujiamini

Shida na raha

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
3,773
Reaction score
3,474
Habari zenu wana MMU,

Nimekutana na suala hili hii ni mara ya pili, utakuta mtu anaenda hospitali akiwa na makonfidensi kibao, mwisho wa yote huishia ukingoni.

Nikiwa na maana mtu umeenda kupima VVU, ikifika muda wa kupata majibu unakuta mtu yule ameshakimbia, kulikoni? Hii husababishwa na nini, uoga au kutokujiamini na anachokifanya?

Leo nilikua hospitali ya Mnazi Mmoja, jamaa kaja kuchek afya wakati wa kutakiwa apokee majibu hayupo. Inakuaje?
 
Mi akisha pima wife inatosha.

Teh teh teh hiyo siku nilikuwa na wife mbona nilijuta kwenda,Dr anawauliza haya majibu niwape wote kwa pamoja au kila mtu peke yake mara wife akadakia tupe wote kwa pamoja,Dr akawa anaongea kiupole sasa nikiwapa haya majibu ukiwa umeathirika utafanya nini?dah hapo nilitaka nitoke nje kabisa,wife akajibu ataishi kwa matumaini na kuanza tiba. Mara Dr kavuta file majibu ndio haya Bwana Mgodo inaonyesha kuwa Afya yako ipo poa,duh nilishusha pumzi mpaka Dr akashangaa.
 
Mkuu mbona unauliza maswal yenye majibu hapo hapo labda nirudie majibu.

Uoga
Kutokujiamini
Hofu


Hayo ndio yanasababisha kukimbia


Kutokujiamini kunatokana na kuwa kama ulicheza gem bila ndomu na timu chafuchafu
 
Sasa kama dawa hakuna nipime ili iweje ??
 
Kupima kwawafaa wanawake,Mwanaume mzima unaenda kupima HIV? mambo ya kike hayo.
 
kwangu ni kawaida sijui kwa vile nimeacha kupenda na kufanya ngono?
 
Asikuambie mtu kupokea majibu siku hyo mpaka kijasho kilinitoka mpaka nurse akawa anaogopa hata kunipa majibu kiti hakikaliki mapigo ya moyo spidi 140 niliyapokea kwa mbinde nashukuru mungu nikakutwa mzima
 
Nenda hospitali wodi ya waathirika wa HIV utapata jibu la swali lako
 
Majibu sio mchezo,mimi nilipima chuoni nikakutwa nao basi pale nilijikaza nikatoka kwenye kibanda chao na tabasamu nikatafuta chakula na maji nikaingia rum,nikala alafu nikaanza kulia mpaka nikaishiwa nguvu..dah
 
Majibu sio mchezo,mimi nilipima chuoni nikakutwa nao basi pale nilijikaza nikatoka kwenye kibanda chao na tabasamu nikatafuta chakula na maji nikaingia rum,nikala alafu nikaanza kulia mpaka nikaishiwa nguvu..dah
Pole sana Mkuu ni hali ya kawaida, wengine woga undo unatufanya tusipime
 
Majibu sio mchezo,mimi nilipima chuoni nikakutwa nao basi pale nilijikaza nikatoka kwenye kibanda chao na tabasamu nikatafuta chakula na maji nikaingia rum,nikala alafu nikaanza kulia mpaka nikaishiwa nguvu..dah

Aiseee ulikutwa nao?? Yaan ukapata na hamu ya kula kabisaaaa.. aisee au ulikua unajijua kabisa eeeeh
 
Back
Top Bottom