Kwa hali hii, Je mimi ni Genius??

Kwa hali hii, Je mimi ni Genius??

Hi members, nitaanza kwa kujitambulisha hapa chini kabla ya kwenda kwenye mada kamili.

Jina: Free ideas(Not official)
Umri:29yrs
Elimu:Shahada
Kabila:Kanda ya ziwa
Familia: Married with 2 kids


Kiufupi nimesoma 0-A level hapa Tanzania kisha nikaenda nje ya nchi(Europe) kuchukua Bachala.

Binafsi kuna hali inanitokea hua mpaka mwenyewe nashindwa kujielewa kama ni kwangu tu ama hata kwa watu wengine, lakini kila nikijaribu kumsimulia mtu kuhusu yanayonitokea hua ananishangaa na kuona kwamba mimi sio mtu wa kawaida.

Nitaeleza japo kwa ufupi hapa chini kuhusu hali hiyo.


.
.
2. Napenda sana kukaa mwenyewe na hua nikiwa mwenyewe najikuta naongeaongea na wakati mwingine kucheka mwenyewe.Pia mama yangu aliponizaa anasema kwanza hakusikia uchungu wa uzazi kabisa.Pia nilipozaliwa tu nilicheka badala ya kulia kama watoto wengine.Nikiwa na miaka 3 nikikua na uwezo wa kusoma bila kukosea.
.
.

.
.

.
.
.
.
.
6. Mwaka mmoja kabla ya babu wa Loliondo nikiwa nje ya nchi nilimwambia jamaa yangu kwamba mwakani kuna mtu ataibuka maarufu kwa kusema anatibu ukimwi tanzania na atapata watu wengi.Kweli ikawa jamaa yangu mpaka leo anaamini mimi ni ndugu yake huyo babu na kwamba nilijua paln zake.
.
.

.
.

.
.

.

.
.

.
.
13. Sipendi kabisa habari za Dini na maswala yamuhusuyo mungu(mimi ni Atheist) na hua najickia vibaya sana kujadili maswala hayo.Ninaamini hakuna mungu.Pia sina ushabiki wa vitu vinavyopendwa na watu wengi mfano mpira ama siasa.
.
.
14. Napenda kukaa sana vijijini (japo kwa sasa niko mjini sababu ya kazi)na kufanya kazi huko, sipendi kuajiliwa na wala sifurahii kabisa kulipwa mshahara na mtu mwingine.Napenda pia kuzunguka zunguka sehemu zenye mito ama maji yanayotiririka na kuyaangalia huku nikijiongelea mwenyewe.
.
.
15. Kuna mwaka flani nilikua kijijini eneo la mto akili ikanituma niangalie juu ghafla kikashuka kitu kizito sana kutoka angani kama jiwe kubwa, baada ya kutua chini ghafla kitu kile kikageuka ndege mzuri na sijawahi kuona ndege wa aina kama ile tena mpaka leo.Ndege yule aliruka ruka kunizunguka kisha akapaa kurrudi angani vertically. Cha ajabu sikuogopa kabisa hali ile.
.
.
.
17. Tangu niwe na akili timamu sijawahi kutoa chozi kwa maana ya kulia.Hata misibani nikienda hua naona ni hali ya kawaida na napenda sana kuishika maiti hasa kichwani.Wakati mwingine hua naomba nioshe maiti iliradi niishike kichwa tu kisha nami najishika kichwa halafu naondoka msibani.
.
.
18. Napenda harufu mbaya sana.Nikipita mahali kuna mzoga naweza kumaliza nusu saa hapo navuta harufu mpaka tumbo hua linajaa.Nikimuona mtu analia ama yuko kwenye huzuni mimi hua nafsi inafarijika na napenda kumwangalia huku natabasamu.
.

.
.






.....Free ideas.......

Hili ni Tatizo kubwa Sana unalo mkuu.
Namba 2,13, 15, 17, na 18,

Zinaweza kukufikirisha. Kwakua sio hali ya kawaida.

Naweza kusema hauishi maisha yako halisi. Uko possessed under spirit.

Ushauri.

Jaribu kufuatilia dini hasa unazozichukia kisha uone zinaleta effect gani katika maisha yako.

Nina uhakika utafungua Pandora box kuhusu wewe ni nani hasa...?
 
TIKITI.jpg
 
kama mama yako alichelewa kupata mtoto,labda kukupata alienda kwa waganga
 
Hili ni Tatizo kubwa Sana unalo mkuu.
Namba 2,13, 15, 17, na 18,

Zinaweza kukufikirisha. Kwakua sio hali ya kawaida.

Naweza kusema hauishi maisha yako halisi. Uko possessed under spirit.

Ushauri.

Jaribu kufuatilia dini hasa unazozichukia kisha uone zinaleta effect gani katika maisha yako.

Nina uhakika utafungua Pandora box kuhusu wewe ni nani hasa...?
Nashukuru kwa ushauri mkuu
 
kama mama yako alichelewa kupata mtoto,labda kukupata alienda kwa waganga
Hapana ndugu mimi ni mtoto sahihi sa tatu kati ya watoto 6, ila nimepishana na kaka yangu miezi 8 kwa maana hiyo mama alinibeba mimba kaka akiwa hajaachishwa
 
Maelezo yake yanautata ndani yake mengine yanaeleweka ingawa anajichanganya pale anaposema hapendi mshahara wala kuajiriwa but anamaliza kazi yake ndani ya dk3 na anawasaidia wafanyakazi wenzake kama una akiri nyingi kiasi hicho ungekuwa tayari unafanya mambo makubwa zaidi ya kusaidia kazi za wafanya kazi wenzako
So chukua hatua tumia hiyo akiri yako kujenga uchumi wako na jamii yako kwa ujumla.
 
Binadamu anashangaza sana, pengine kuliko viumbe vingine vilivyoumbwa na Mwenyezi Mungu.

Binadamu akiwa na UHAI na UZIMA anakuwa na KUFURU sana kwa Muumba wake

Mtoa mada wewe si Genius, ila kama kweli unayo hata tabia robo ya hizo ulizotaja maana yake ni una MAONO au UCHAWI. Kuwa na maono ni zawadi tu kutoka kwa Mwenyezi Mungu wapewayo watu wachache...mfano kuweza kuona yajayo mbeleni kabla ya watu wengine kuona.

PIA, Ungejua idadi ilivyo kubwa ya Atheists wanaorudi kwa Mwenyezi Mungu na kuamini uwepo wake ungeshangaa.

Halafu usifikiri kila Atheist ni Genius.

Kuna uwezekano umesoma tu habari za Geniuses wengi ukagundua hizo tabia zao sasa unataka nasisi tukutazame kwa perception hiyo.
 
Mkuu namba 9 mbona kama inakataa hivi.. Sababu huu uzi tuu umechapia herufi kibao.
 
Una uwezo Wa kuandika haraka bila kukosea ilhali hili andiko tu lenyewe umekoseakosea sehemu nyingi tu. Nadhani uongeze paragraph nyingine kuwa...


"Nina uwezo Wa kuandika kwa kukoseakosea bila kujua kama nimekosea"

[emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom