Hacheni ubaguzi, janja yenu inajulikana mnamchoka MOD ili haifute hii hoja.
Sasa 4 ya 29 hadi 33 unaweza kufanyia nini? Unajua pass rates kwa level ya div one had div three ni kiasi gani? Na unajua kwamba hizo shule za mavuvuzela alizojenga Kikwete kwa kutumia mipango na mikakati ya Mkapa ya kupunguza umaskini by 2025, wanasoma watoto wa masikini tu?
Natamani Mkapa angeongezewa muda wa kuongoza nchi kwa kuwa alikuwa ana vision ya wapi nchi inakwenda. Naamini angekuwepo yeye hali ya shule isingekuwa hovyo kiasi hiki. Mwenzenu Mkapa aliendesha MMEM kwa mafanikio ya ajabu bila kuathiri ubora wa elimu. Nyie mmeshindwa hata kujenga darasa, mkaachia wananchi wachangie kila kitu, halafu mnakaa mbele za watu kujigamba. Hamjui tu huwa mnanikera kiasi gani. Nashukuru kwamba tunafanya mijadala hii kwenye mtandao naamini tungekuwa tunakutana ana kwa ana lazima zingerushwa ngumi. Nakasirika sana kuona watu ambao kwa maslahi yao binafsi wanajifanya hawaoni hali ya nchi ilivyo.
Bwana Dubo kazana sana kula hiyo rushwa na kuwakandamiza masikini kama unavyofanya. Mwisho wa yote ni kaburi. Hakuna atakayeishi juu ya nchi milele. Kwa hiyo haisaidii kujilimbikizia mali na kuwaumiza wengine kwa maslahi yako binafsi. Ni bora zaidi kusimamia haki ya kila mmoja huku ukitambua kwamba kuwepo kwetu duniani ni kwa neema tu.
Sasa 4 ya 29 hadi 33 unaweza kufanyia nini? Unajua pass rates kwa level ya div one had div three ni kiasi gani? Na unajua kwamba hizo shule za mavuvuzela alizojenga Kikwete kwa kutumia mipango na mikakati ya Mkapa ya kupunguza umaskini by 2025, wanasoma watoto wa masikini tu?
Natamani Mkapa angeongezewa muda wa kuongoza nchi kwa kuwa alikuwa ana vision ya wapi nchi inakwenda. Naamini angekuwepo yeye hali ya shule isingekuwa hovyo kiasi hiki. Mwenzenu Mkapa aliendesha MMEM kwa mafanikio ya ajabu bila kuathiri ubora wa elimu. Nyie mmeshindwa hata kujenga darasa, mkaachia wananchi wachangie kila kitu, halafu mnakaa mbele za watu kujigamba. Hamjui tu huwa mnanikera kiasi gani. Nashukuru kwamba tunafanya mijadala hii kwenye mtandao naamini tungekuwa tunakutana ana kwa ana lazima zingerushwa ngumi. Nakasirika sana kuona watu ambao kwa maslahi yao binafsi wanajifanya hawaoni hali ya nchi ilivyo.
Bwana Dubo kazana sana kula hiyo rushwa na kuwakandamiza masikini kama unavyofanya. Mwisho wa yote ni kaburi. Hakuna atakayeishi juu ya nchi milele. Kwa hiyo haisaidii kujilimbikizia mali na kuwaumiza wengine kwa maslahi yako binafsi. Ni bora zaidi kusimamia haki ya kila mmoja huku ukitambua kwamba kuwepo kwetu duniani ni kwa neema tu.
Mleta thread amesema annur na si alhudda. Yaelekea wewe haupo Tanzania ndo maana huoni hata shule moja katika kata yako. Bila shaka hakuna hata mwana JF yeyote atakaekubaliana nawe kwa hilo.Al Hudda kuja na twakimu za maeneo ya DSM na kusema JK kafanya kazi kubwa katika nyanja ya Elimu ni kutumia takwimu vibaya sana. DSM ni sehemu ndogo ya nchi mzima kwa hiyo haiwezi ikawa kigezo cha mafanikio katika Tanzania nzima. Mimi ninakotoka katika Jimbo la langu la uchaguzi la Nkenge sijaona shule hata moja iliyojengwa tangu 2005 hadi leo. Hata moja. Juzi juzi tumeambiwa kwamba hata foleni DSM ni dalili ya maendeleo. Ni matusi!!