Katika hatua za awali za mchakato wa katiba mpya sisi wengine tuliamini kuwa ifikapo mwaka 2015 itapatikana katiba mpya hasa baada ya ule mswaada wa awali kurejeshwa bungeni baada ya kelele za wadau kuwa nyingi. Niliamini hatua ile ingekuwa ndio mwisho wa kufanywa hadaa katika jambo hili nyeti kwa taifa na mustkbali wa vizazi vijavyo. Lakini yaliyotokea hivi karibuni kule Bungeni ni ishara tosha KUWA UPATIKANAJI WA KATIBA MPYA UKO SHAKANI SASA.
TUJIKUMBUSHE HAYA.
1.Katika mswaada wa awali kabisa ulipata upinzani hasa kwa upande wa Zanzibar kutokana na kutokuwa na usawa katika baadhi ya vipengele hasa vilivyohusu wajumbe na uwakilishi katika ngazi za maamuzi( wajumbe wa tume na muundo wa bunge la katiba) na baadhi ya Term of reference- kumbukeni suala la kujadili kuwepo au kutokuwepo muungano lilipigwa marufuku.
2. Tokea awali suala la katiba mpya lilitekwa na wanasiasa na kusahau uwakilishi mpana wa wananchi kwa nini muundo wa bunge la katiba liliwataja wabunge wanaotokana na vyama na wawakilishi kuwa wajumbe wa moja kwa moja na ikasahau kuwa kuna watanzania wengi zaidi ambao hawana vyama na hili suala lilinyamaziwa?
Maelezo hayo yanaaminisha jambo moja tu. HAKUKUWA NA NIA HASA YA KUTENGENEZA KATIBA YA WANANCHI ila ni kujaribu kufanywa hilba kwa kisingizio cha wakati na ukweli ni kwamba huo wakati wenyewe hauheshimiwi.Kwa nini katiba ya wakati iwatenge baadhi ya watu wa wakati wa leo( wananchi wengi wasio na vyama) ?
MWENDELEZO WA HILBA NA KILICHOJIRI
Mara baada ya kutoka rasimu ya awali na kuonekana wazi kuwa inatishia maslahi ya baadhi ya wanasiasa (CCM) chama ambacho ndicho kinaisimamia serikali inayoandaa katiba mpya walianza kucharuka na kuzidi kuuteka mchakato.
Taarifa za wazi za kupinga zilisikika kutoka kila kona mpaka kwa wale ambao walikuwa wamesahaulika waliibuka na sasa ikawa ni kujihami kwa kila hali. Zilivuja taarifa kutoka katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa ilifika mahali wajumbe wa NEC ya CCM walidiriki kuhoji ilikotoka sera ya katiba mpya wakati ile ya CCM 2010-2015 haimo. kuanzia hapo imekuwa ni kuandamwa kwa mwenyekiti wa chama mpaka leo.
Kilichojiri ni kwa makusudi kuharibu hatua muhimu ambayo kwa mwendelezo wa mchakato wa katiba ambapo kwenye nia njema hatukutarajia kutokea- hii ni dalili nyengine kuwa HAKUNA NIA NJEMA YA KUPATIKANA KATIBA. waliofanya hivi ni watu wale wale waliojazana katika hilo bunge tajwa la katiba linalokuja mbeleni, ni wale wale wanaoongoza nchi ni wale wale ambao serikali inayoongozwa na chama chao walileta hoja na mswaadawa katiba mpya.na ndio hawa hawa wanaopinga mapendekezo ya tume.( naona kisutu na mwenye kisutu simwoni) ndivyo ninavyoweza kusema.
Kinachoendelea kwa sasa baada ya bunge kupitisha mswaada wa upande wa chama kimoja kilichoteka bunge, licha ya wapinzani kuchachamaa jamaa hawa wamefanikiwa suala moja kubwa na muhimu la KUPOTEZA MUDA ili kwa maslahi yao uchaguzi ujao ufanyike katika katiba ya sasa maana wanajuwa hata rais akatae kutia saini kwa mfano muda utakuwa umekwenda sana na na kwa hili la katiba kwa sasa ni sawa na kuwa limesimamama. Katika hali hii tayari washenga wa CCM na wanaopinga rasimu ya katiba wanatumia mwanya huo kuonesha kasoro lukuki na hapa kwa mtazamo wangu wanataka kuhalalisha mchakato usiendelee mbele. wametumia wingi wao bungeni kusitisha mchakato usiendelee na hii ndio jeuri ya CCM ikiwa jambo hawalitaki. Wao ni daima tu.
MAWAZO YANGU.
Ikiwa suala la katiba limetokana na utashi wa kweli kwa ajili ya wananchi na tanzania mpya kutoka kwa raisi mwenyewe na timu yake yaserikali basi hili suala litapita vizuri na hayo mengine vijana wa leo wanaliita shengesha tu na ikiwa Mh mwenyewe yumo anacheza na wakati , basi hili limefika mwisho ingawa kuna dalili za kuharimu kila kitu,mali, wakati na hata nafsi za watu ziko hatarini kupotea
SASA tunasubiri Rais wetu akiondoka madarakani kwa aibu mbaya au kwa kuandika HISTORIA YA UKWELI
Uamuzi anao yeye mwenyewe.
Nawasilisha
TUJIKUMBUSHE HAYA.
1.Katika mswaada wa awali kabisa ulipata upinzani hasa kwa upande wa Zanzibar kutokana na kutokuwa na usawa katika baadhi ya vipengele hasa vilivyohusu wajumbe na uwakilishi katika ngazi za maamuzi( wajumbe wa tume na muundo wa bunge la katiba) na baadhi ya Term of reference- kumbukeni suala la kujadili kuwepo au kutokuwepo muungano lilipigwa marufuku.
2. Tokea awali suala la katiba mpya lilitekwa na wanasiasa na kusahau uwakilishi mpana wa wananchi kwa nini muundo wa bunge la katiba liliwataja wabunge wanaotokana na vyama na wawakilishi kuwa wajumbe wa moja kwa moja na ikasahau kuwa kuna watanzania wengi zaidi ambao hawana vyama na hili suala lilinyamaziwa?
Maelezo hayo yanaaminisha jambo moja tu. HAKUKUWA NA NIA HASA YA KUTENGENEZA KATIBA YA WANANCHI ila ni kujaribu kufanywa hilba kwa kisingizio cha wakati na ukweli ni kwamba huo wakati wenyewe hauheshimiwi.Kwa nini katiba ya wakati iwatenge baadhi ya watu wa wakati wa leo( wananchi wengi wasio na vyama) ?
MWENDELEZO WA HILBA NA KILICHOJIRI
Mara baada ya kutoka rasimu ya awali na kuonekana wazi kuwa inatishia maslahi ya baadhi ya wanasiasa (CCM) chama ambacho ndicho kinaisimamia serikali inayoandaa katiba mpya walianza kucharuka na kuzidi kuuteka mchakato.
Taarifa za wazi za kupinga zilisikika kutoka kila kona mpaka kwa wale ambao walikuwa wamesahaulika waliibuka na sasa ikawa ni kujihami kwa kila hali. Zilivuja taarifa kutoka katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa ilifika mahali wajumbe wa NEC ya CCM walidiriki kuhoji ilikotoka sera ya katiba mpya wakati ile ya CCM 2010-2015 haimo. kuanzia hapo imekuwa ni kuandamwa kwa mwenyekiti wa chama mpaka leo.
Kilichojiri ni kwa makusudi kuharibu hatua muhimu ambayo kwa mwendelezo wa mchakato wa katiba ambapo kwenye nia njema hatukutarajia kutokea- hii ni dalili nyengine kuwa HAKUNA NIA NJEMA YA KUPATIKANA KATIBA. waliofanya hivi ni watu wale wale waliojazana katika hilo bunge tajwa la katiba linalokuja mbeleni, ni wale wale wanaoongoza nchi ni wale wale ambao serikali inayoongozwa na chama chao walileta hoja na mswaadawa katiba mpya.na ndio hawa hawa wanaopinga mapendekezo ya tume.( naona kisutu na mwenye kisutu simwoni) ndivyo ninavyoweza kusema.
Kinachoendelea kwa sasa baada ya bunge kupitisha mswaada wa upande wa chama kimoja kilichoteka bunge, licha ya wapinzani kuchachamaa jamaa hawa wamefanikiwa suala moja kubwa na muhimu la KUPOTEZA MUDA ili kwa maslahi yao uchaguzi ujao ufanyike katika katiba ya sasa maana wanajuwa hata rais akatae kutia saini kwa mfano muda utakuwa umekwenda sana na na kwa hili la katiba kwa sasa ni sawa na kuwa limesimamama. Katika hali hii tayari washenga wa CCM na wanaopinga rasimu ya katiba wanatumia mwanya huo kuonesha kasoro lukuki na hapa kwa mtazamo wangu wanataka kuhalalisha mchakato usiendelee mbele. wametumia wingi wao bungeni kusitisha mchakato usiendelee na hii ndio jeuri ya CCM ikiwa jambo hawalitaki. Wao ni daima tu.
MAWAZO YANGU.
Ikiwa suala la katiba limetokana na utashi wa kweli kwa ajili ya wananchi na tanzania mpya kutoka kwa raisi mwenyewe na timu yake yaserikali basi hili suala litapita vizuri na hayo mengine vijana wa leo wanaliita shengesha tu na ikiwa Mh mwenyewe yumo anacheza na wakati , basi hili limefika mwisho ingawa kuna dalili za kuharimu kila kitu,mali, wakati na hata nafsi za watu ziko hatarini kupotea
SASA tunasubiri Rais wetu akiondoka madarakani kwa aibu mbaya au kwa kuandika HISTORIA YA UKWELI
Uamuzi anao yeye mwenyewe.
Nawasilisha