Kwa ajili yako Maimuna

Kwa ajili yako Maimuna

Sasa hivi unatupia mwendelezo within few hours, uzi ukipata viewers wengi unaanza nyodo na kuturusha ooh, mara kazi Ni nyingi, mara hamnilipi, mara hamna shukrani, mara njooni WhatsApp kupata mwendelezo n.k.
Kwahiyo mi sitasoma Ila nitaendelea kufatilia hadi pale nitakapoona umefika episode ya mwisho ndo naanza kusoma.
Kwamba unataka kusoma bure mwanzo mwisho ??? Ila binadamu bhana
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 08

MAWASILIANO: 9783642467

SONGA NAYO.......

Rajabu akainuka alipokuwa amekaa na kumfata maimuna na wakati huo alikuwa amechukia mno yaani hasira alizokuwa nazo zilikuwa azipimiki, shyna aliigopa sana na anajua hasira za kaka yake, haraka akamdaka kwa kumvuta mkono

"Kaka...."

Aliita shyna akistua akili ya rajabu yaani ni kama alishaama kwenye eneo lile lakini rajabu akuelewa alizmsogelea zaidia maimuna ambaye wasiwasi ulimtawala maana anaijua vizuri akili ta tajabu...

"Mnaona anataka kunipiga anataka kuniumiza, hakuwa kumpokea huyu mtoto katika maisha yake lakini ndo hivyo ndio maana jana alinipiga na kutaka kumuangamiza huyu mtoto lakini kwa uwezo wa Mungu mtoto wangu anaishi 🥹"

Aliongea maimuna na majilani wengi walimuamini na kuamini kuwa maimuna anazungumza ukweli na anapitia wakati mgumu, rajabu alinyanyua mkono wake kutaka kumpiga maimuna lakini mama rukia aliwai na kudaka mkono

"Hii nyumba yenu ishakuwa ya maonyesho sasa si ndio ??"

Alifoka mama rukia

"Mai rajabu amekubaka lini ??"

"Juzi....."

"Na mimba yako ina miezi mingapi ??"

"Mitatu "

Ila nyie njia ya muongo ni fupi sana akikuta kwa muda mmoja akijibu maswali mawili yenye ukweli halisi kila mtu alicheka yaani

"Umeamua kunichanganya kwa maswali ili kuficha ukweli sio, mama mtu mzima hovyo kwani sijui kama unatoka na rajabu
....."

Uwiiiiiiih🥹 maimuna si ndo akavuka mipaka na kuongea maneno ya hovyo kwa mama rukia ambaye alikuwa ni mtu mzima anayejiheshimu sana, yaani daaah huyu binti sijui anashida gani hapo hasira ya rajabu ilivuka kiwango ingawa alikuwa ameshikwa na watu lakini alirusha take moja ambalo moja kwa moja lilifika kwa maimuna na kumpeleka maimuna chini, na kwakuwa maimuna alikuwa amezoea drama na siku hiyo alifanya alijipanga kufanya drama zake, alianza kugalagala na kulia sana kuwa anamaumivu ya tumbo lakini kwa muda huo hakuna ata mmoja alikuwa akijali yeye kila mtu alikuwa bize na kumtuliza rajabu

"Maimuna nitakuua we binti sawa ?? Usije ukacheza karibu na hasira yangu najua kila kitu, najua kila uchafu wako naaangaika natafuta hela uku na uku silali mimi nachukua mpaka Dabo kazini kazi yenyewe ya kuzunguka uku na uku pasi na kupumzika kwaajili ya mama halafu ninapoondoka unamshindisha njaa, ukumbuki kumpa ata dawaz unafikili sijui, niliamua tu kukaa kimya kwasababu mama apikupenda na kutuambia kukufanya wewe ni mdugu yetu na utakuja kubadilika lakini sio kwa sasa nitakuua mai usicheze na mimi...."

Weeeh nyiee motrooh aliouwasha maimuna kwa rajabu auziki ata kwa maji bahari nzima kaka anajua kuwaka huyu hatari,

"Basi rajabu basi....."

Watu waliendelea kumtuliza rajabu mwaya maana alikuwa akiongea uku analia ni wazi alikuwa na mengi juu ya mai na siku hiyo aliamua kuyatema

"Rajabu......"

Sauti nzuri na nyororo na utulivu ilisikika ikiita jina la rajabu, ila nyie nagma chombo watu wote waliganda kwanza wakimshangaa maana daaah mtoto kaumbika huyu

"Tuliza jazba rafiki yangu...."

Eeeh maimuna jamani akomiz akainuka Chap na kumvamia Nagma wa watu

"Wewe ndio Chanzo cha rajabu kunikataa rajabu ni wangu....."

Alifoka maimuna muda huo alikuwa amemng'ang'ania nagma ambaye hata kupigana alionekana kuwa hajui alikuwa akiangaika tu kujitoa mikononi mwa maimuna, hata sijui shyna alitoka na wapi akiwa na Nuala alimtandika maimuna mgongoni mfululizo yaani mpaka kanikumbusha mbali enzi hizo ndala ndio ilikuwa siraha kuu kwa mama yangu akitaka kuninyoosha .

Kwa Nuala zile ambazo alichapwa maimuna mwenyewe alimuachia nagma wa watu, nyie rajabu anajua kujali akamshika mshika nagma vizuri kabisa

"Niangalie nagma...."

Aliongea rajabu kwa wasi wasi sana akionesha kujali

"Niangalie nagma usilie hivyo sasa niangalie mama...."

Nyie me nataka mchumba kama rajabu the way alivyokua anamuuliza Nagma mpaka nilitamani kaka anajua huyu, Rajabu aliweza kugundua kuwa nagma anawasiwasi sana akamshika mkono na kumuingiza ndani, mama rukia ingawaje alikuwa amechafuliwa na maimuna lakini haikuwa sababu ya yeye kumuacha alimchukua na kumuingiza ndani kwake...

"Na nyie ondokeni uko umbea tu...
"

Kuchanganyikiwa kubaya yaani shyna akaamishia hasira zake kwa majilani ambao baada ya kusema hivyo walimchek

"Umbea tu imewajaa msiende kulisha familia zetu uko, cheki watoto wadogo umbea si mwende shule "

Aliendelea kulalamika shyna

"Hii nyumba tangu amefariki bi rehema amani hakuna sipati picha hii nyumba ingekuwa ya kwao...."

Upande wa mama rukia aliingia ndani na maimuna na kumuweka atulie

"We unashida gani kwani ?? Eeeh ?? Halafu kwanini unaongea uongo ?? Me najua kila kitu sawa ilikua ni umbea lakini nilishuhudia kila kitu nilikuwa nimetoka kwenda chooni nilikukuta ukiongea na kijana fulani kwamba ulale na rajabu umsingizie mimba au sio wewe ?? Haya dokta wa watu mwaya najua umemdanganya huyo sio mtoto wake sio ?? Mtoto hasidi wewe..."

"We nawe mtu mzima kileja niache "

"Ukweli unauma eeeh ?? Na unabahati sijamwaga mchele mbele ya watu najua kila kitu, we mtoto wa aina gani usikii kwanza wewe usingezaliwa mapema ungemuua mama yako "

Siku hiyo mama rukia aliamua kutoa ya kohoni maana alishachoshwa na mambo ya maimuna....

Kwa upande wa pili wa rajabu alitumia muda wakw vizuri kabisa kumtuliza Nagma.

"Rajabu huyu msichana ni nani yenu ??"

"Kama ambavyo ulimsikia mama alimuokota miaka kadhaa nyuma na kumlea "

"Leo ndio nimemjua vizuri nishawai kumfumania huyu huyu maimuna na mume wangu....."

"Unasemaje ??"

Alistuka rajabu na kuuliza

"Nakuja...."

Nagma aliinuka na kuondoka kwa kasi ya ajabu sana aiseeeh yaani aliondoka kwa mwendo wa haraka, akapanda kwenye gari yake na kuondoa Chap uku akiacha vumbi....


ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 09

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO..........

Yaani siku hiyo, nyumba ya kina rajabu ilikuwa ni sehemu ya madrama na maigizo ya kutosha yaani ile anaondoka tu Nagma baba mwenye nyumba akaingia akiwa ameongozana na gari ile ya bomoa bomoa, Rajabu alishtuka sana kuwaona maana anajua kabisa kuwa anadaiwa kodi ya takribani miezi 8 hivi.....

"Baba......"

Rajabu alimuwai baba mwenye nyumba lengo likiwa ni kuzungumza nae....

"Kijana me sio baba yako na tulishazungumza ili suala, nilikuambia kuwa nimeuza hii nyumba nimekuja tu kukusaidia utoa bitu vyako, mwenyewe anabadilisha kila kitu.....

"Daaah mzee wangu unatutoa gafla sanaz naomba tupatie ata siku tatu zinatosha sana....."

"Vunja........"

Mzee yule hakutaka kumsikiliza tena rajabu na malalamiko yake

"Subili tunatoa vitu....."

Ila nyie shyna ni mwanamke nusu alijikaza na kusimama imara akachukua kanga yake na kujikaza tumboni kisha akaanza kutoa vitu, rajabu pi hakukaa kizembe akaanza kumsaidia kaka yake bila kumsahau mama rukia muda huo maimuna alikuwa amekaa pembeni akiwacheka

"Mmelinga wenyewe mmeninyanyasa kumbe nyumba ya kupanga eeeeh maimuna mie kijukuu cha mtume "

Alizungumza maimuna lakini kwa wakati huo kila mtu alikuwa bize akiangaika kutoa vitu ingawaje walimsikia waliamua kumpotezea

"Kwanza nashukuru sijabeba mimba yaki walahi ningeteseka mimi, kwahiyo hapo mmnaenda mtaani au ?? Aaah nilisahau kumbe mna mama mwingine eti mama rukia si utachukua vifaranga vyako ?? Na kuvilea ??"

Maimuna aliongea maneno ya ovyo mno lakini hakuna ata mmoja ambaye aliweza kumjibu

"Makubwa kumbe wote mmekuwa mabubu"

Alizungumza maimuna kisha akainuka na kufata begi lake la nguo

"Kwaherini naenda zangu kwa bwana angu Tajiri dokta wangu, uzuri ni kwamba ameamini kuwa huyu mtoto ni wake....."

Maimuna akaita bajaji na kuondoka, Rajabu na dada yake walimaliza kutoa vitu na bila kupoteza muda gari ya bomoa ilianza kazi yake rajabu alilia kama mtoto wa kike vile akikumbuka kuwa nyumba hiyo ilikuwa na kumbukumbu nyingi sana za maisha yao yaani walianza kuishi tangu wakiwa watoto, wameishi hapo tangu enzi za uhai wa baba yao, leo hii wanatoka tena kwa kufukuzwa....

"Kaka usilie sasa....."

Shyna pekee ndio aliweza kujikaza na alikuwa akimbembeleza kaka yake ingawaje ilikuaa kazi nzito sana kwani rajabu alikuwa analia sana aliwaza anampeleka wapi dada yake kwa siku hiyo kwenda kulala akifikilia muda wa kazini umefika lakini pia hawezi kwenda na kumuacha dada rajabu alilia sana alikosa cha kufanya, mwisho alichoka zaidi na kupitiwa na usingizi muda huo alikuwa amelala chini ya mti....

Baada ya masaa kama matatu alikuja Nagma akiwa na katoto kadogo sana yaani kwa kukadilia ni miaka miwili au mitatu kalikiwa katoto karembo Sana yaani, nagma alishangaa sana kukuta hali ile yaani daaah 🥹 ameondoka na kuacha nyumba ikiwa imesimama lakini anarudi na kukuta nyumba imeshavunjwa na majilani wengine walikuwa wakijitaidi kujizolea matofali ambayo yalikuwa hayajavunjia....

Shyna alimkimbilia Nagma na kumkumbatia hapo kidogo alipata ata muda wa kupunguza maumivu ya moyo wake ambayo aliyaficha kwa muda maumivu ambayo aliyaweka kando ili kaka yake asiumie zaidia

"Nini kinaendelea....??"

"Tumekwisha tumekwisha sisi......"

Kilio cha shyna kilimtoa rajabu kwenye njozi nzito na nzuri aliyokuwa akiiota, alistuka na kupiga kelele

"Lilian......"

Cha ajabu yule binti mdogo aliyekuja akiwa na Nagma aliitika ikimaanisha kuwa Lilian ni jina lake nyieeeeh hapa sijui nini kinaendelea walahi.....

"Ooooh nagma....."

Alizungumza rajabu muda huo akijaribu kuweka Macho yake sawa kwani ndio kwanza alikuwa ametoka kwenye usingizi

"Mbona ukunipigia simu ?? Ili tukio limefanyika saa ngap ??"

Nyie Nagma mbona anajali sana kuhusu rajabu maana muda huo alimuachia shyna na kumshika rajabu....

Nagma tena mama mifedha, alimfata mama rukia na kuzungumza nae kisha akatoka nje

"Tuondokeni....."

"Eeeeh....."

Yaani shyna ndio alikuwa wakwanza kuitika ni kama alikuwa aamini hivi kuwa wanaambiwa waondoke ingawaje alikuwa ajui wanapelekwa wapi alifurahi tu.....

"Dereva atakuja kubeba hii mizigo nimeshamtumia location "

Alizungumza Nagma na muda huo tayali walikuwa ndani ya gari na safari ilikuwa ikiyoyoma, muda wote huo Rajabu alikuwa akimya sana hakuongea wala kuweka neno ila sasa shyna anajua kula na kipofu bhana muda wote alikuwa akimchekesha yule mtoto maana anajua mama yake anatusaidia wacha na mimi nifanye jukumu la kuchekesha mtoto.......

Safari iliishia getini kwenye nyumba ya Nagma....

"Nyumbani kwako ??"

Aliuliza rajabu

"Ndio, najua unamuandafia mume wangu nikutoe wasiwasi kabisa hayupo huyo mbwa nimemtimua kitambo....."

"Mmmmh kumtimua ??"

Hapo rajabu kidogo akataka kujua mambo akakaa mkao wa kula umbea .

"Wacha tuingie ndani tutaongea...."

Waliingia mpaka ndani kasheshe shyna alikuwa anacheka kama chizi kaona jalala jipya

"Karibuni sana...."

Aliwakaribisha kisha akaingia chumbani kwake na kuwaacha sebuleni.....

ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 10

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO.......

"Kaka hii nyumba yake ??"

"Shyna kimya kwanza kaa kimya ujui tu kichwa changu kina mambo mengi mpaka sijielewi nahisi kitapasuka....."

Alizungumza rajabu ambaye muda wote huo kichwa chake kilikuwa kinaangalia juu tu kwa mawazo

"Basi kaka....'

Muda huo huo, akashuka nagma akiwa ameshabadili nguo amevalia tu Dela....

"Lily mpeleke antie chumbani kwako ndio rafiki yako huyo....."

"Sawa mama...."

"Rajabu naomba nifate"

Liliane na shyna alielekea chumbani kisha nagma na Rajabu wakaingia jikoni
..

"Pole sana rajabu pole najua kwa sasa hivi unapitia mambo makubwa sana nikuulize kitu unanikumbuka ??"

Aliuliza nagma swali ambalo lilimchanganya sana Rajabu ambaye alikaa akiwaza na kujiuliza kimoyomoyo mwisho akajibu

"Hapana kwakweli sikukumbuki ata kidogo kwani we unanijua kabla....??"

"Sana tena zaidi ya sana, tuachane na hayo najua unajua mambo ya mapishi sana wacha tupike kwa pamoja"

"Wait Nagma nambie wewe ni nani ?? Nachanganyikiwa kabisa nachanganyikiwa "

"Raj tulia basi kwani shida yako nini ?? Utanijua kwanza kabisa nataka kukufanya uwe mwenye furaha siku zote, nataka kukufanya uwe mwenye tabasamu kama mwanzo "

Rajabu alishusha pumzi nzito sana kisha hakufanya ajizi ukizingatia anapenda sana mambo ya mapishi akaanza kichangamka na kifanya mambo mazuri pale jikoni

"Rajabu yule yule ninayemjua jamani......"

Alizungumza nagma kimoyomoyo kisha akawa anamtazama rajabu na kutabasamu...

Walipika walipomaliza wakatenga mezani kama familia wakakaa na kuanza kula....

"Mmmh da nagma unapika vizuri kama kaka rajabu
...."

Alizungumza shyna ikionesha wazi kuwa mapishi ya rajabu anayafahamu vilivyo

"Mmmh sijapika mimi ni rajabu...."

Alidakia nagma na muda huo huo rajabu akajibu..

"Tumepika wote "

Wakiwa wanaendelea kula muda huo huo aliingia mume wa Nagma akiwa na hasira sana nyuma akifatiwa na mlinzi wa getini kwa nagma

"Boss nimemwambia uruhusiwi kuingia ameingia kwa kutumia mabavu nimeogopa kutumia mabavu yangu jingemuua..."

"Eeeh we nawe maneno mengi si ungemuua au ebu nitokee "

Alifoka nagma akainuka kwenye Meza ya chakula na kusimama mbele ya mume wake huyo...

"Kilichokuleta ??"

"Huyu ndo Rajabu sio ?? Yaani huyu ndio anakufanya wewe unidharau mimi si ndio ?? Huyu anakufanya wewe unaniona mimi kama kichaa eti ?? Kumbuka nagma mimi na wewe tumetoka wapi kumbuka, me kuteleza kidogo tu unanijukumu kiasi hiki ??"

Alilalamika mume wa Nagma muda huo hali ya hewa ilichafuka hakuna ata mtu ambaye aliendelea na kula na jinsi ambavyo mwanaume huyo alikuwa akifoka alimpa wasiwasi sana lily ambaye aliangua kilio ukizingatia bi binti mdogo......

"Shyna naomba beba chakula mkale na lily chumbani kwenu, halafu wewe kiazi nataka unisikilize kwa makini sana...."

"Unafikia hatua ya kuniita mimi kiazi kisa huyu muhuni ??"

Alifoka mume wa nagma na kumrukia rajabu ambaye naye hakukaa kizembe alimdaka vizuri hakutaka tu kupigana nae akamsukumizia pembeni

"Mwanaume mzima uoni haya kukaa kwenye nyumba ya mwanamke yaani umejitanu mwenyewe kwa mke wangu "

Aliendelea kufoka mwanaume huyo akitoa maneno machafu sana juu rajabu ambaye kwa wakati huo aliamua kukaa kimya kwakuwa ulikuwa ni ugomvi wa mume hakuona kama kuna haja ya kuingilia....

"Nagma mke wangu me ndio nakupenda kwa dhati hawa wengine wote wanataka mali zako tu...."

"Unakichaa wewe me mkeo ?? Ebu nioneshe cheti cha ndoa ?? Kwani wewe ulikuwa utumii mali zangu ?? Nimekutafutia kazi ngapi ? Umeacha ukiwa unaamini kabisa utatumia pesa zangu bado ndani kwangu unaleta wanawake kila siku rangi Mpya, sikia nisije nikaongea maneno machafu zaidi ukahaibika naba toka umu ndani na uone kama kituo cha police "

"Lakini nagma nilikuambia nitakuoa ??"

"Kwa kutumia pesa zangu sio ?? Sio wewe uliyeniambia (kabla hajamaliza kuongea nagma akamgeuki rajabu na kusema ) tajabu unaweza kuamini huyu mwanaume nimemlisha nimemvisha Nampa hela ya kwenda kuinjoy na marafiki, kitu alichoanza kunikwaza ni pale aliponiambia nimkopeshe pesa afanye mahali yaani ajatoe kwetu ?? kiasi gani hana aibu "

"Nagma nagma nagma nakuita mara tatu hakuna mwanaume anakupenda kama mimi huyu anakuchezea kwajili ya pesa zako "

"Haya toka nje mbona king'ang'anizi sikutaki....."

Muda huo huo waliingia police watatu

"Afande mtu wenu ndo huyo chukueni atoke hapa sitaki ata kumuona "

"Hii ni bifu umeanzisha nagma nitakukomesha nagma wewe wa kuita police kwaajili yangu najua utanitafuta hakuna mwanaume kama mimi kwako subili uone utakuja ukiwa unapiga magoti "

Alilalamika mwanaume huyo pasi na aibu na police walikuwa wakifanya kazi ya kumvuta uku na uku....

Walimchukua na kuondoka nae hapo nagma alilia sana

"Nilikurupuka mimi 🥹 haraka haraka zangu za kujiona mpweke muda wote nikangukia kwenye mikono ya mtu ambaye si sahihi nilichoka kila kitu...."

Alilalamika Nagma akiwa analia sana rajabu hakuwa mbali alitumia muda huo kumbembeleza, alimuweka kwenye kifua chake akimtuliza taratibu kabisa yaani anamembeleza kwa vitendo hakuongea kitu chochote mwisho Nagma alipitiwa na usingizi na rajabu pia alipitiwa na usingizi kwa pamoja wakalala kwenye kochi moja.....

Kwa upande wa Maimuna alikuwa amelala nje ya geti la mtu ikiwa ni majila ya saa 4 usiku, na muda huo huo ilikuja gari nzuri ya kifahari na kusimama getini

"Msichana......."

Aliita mwanamama mtu mzima kabisa na ndio alikuwa mmiliki halali wa nyumba hiyo, maimuna alishtuka sana na kuangalia

"Shikamoo mama...."

"Marahaba mbona na mabegi ?? Na ni usiku we ni nani ??"

"Mama naitwa maimuna 🥹 naomba nipokee nimekaa hapa siku nzima dokta Matias ndio mwenyeji wangu "

"Inuka kwanza twende ndani "

Mama huyo akaingiza gari ndani kisha yeye na maimuna wakaongozana na kuingia ndani

"Karibu...."

Alikaribisha mama huyo kisha akaanza kuita

"Matias ? Matias......"

"Oooh mama kumbe umerudi "

Alizungumza dokta Matias baada ya kufika sebuleni alikuwa amevalia nguo za kulalia na alikuwa ametoka usingizini alistuka baada ya kumuona maimuna

"Wewe ? Nje....."

Alifoka kwa kutaka kumfukuza maimuna lakini mama yake akamzuia.....

Upande wa rajabu na Nagma ambao walikuwa wamelala sebuleni nagma alionekana kuota ndoto mbaya sana akapiga kelele na kuangua kilioz kelele zake zilimshtua kila mtu mpaka mlinziabaye alikuja mbio.

"Kabosi kangu kuna nini tena....??"

"Mama...."

Lilia aliita na kumkumbatia mama yake

"Nyamaza mwanangu nyamaza 🥹"

"Nagma una nini jamani umenishtua mno "

Aliuliza rajabu

"Rajabu naomba nikuambie kitu nachanganyikiwa kabla chochote hakijanifika naomba ujue kua......"

Alishindwa kumalizia maana alianza kukohoa mfululizo shyna akawai jikoni na kurudi na kikombe cha maji alipotulia tu akampatia

"Rajabu hakuna Muda wa kupoteza naomba ujue kua lily ni binti yako....."

Kila mtu ak.......

ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 11

MAWASILIANO: 0783642467

JINA PATRICIA DAMAS.......

SONGA NAYO..........

Kila mtu alishangaa na kumuangalia nagma kwa macho ya kiulizo ni kama alikuwa anawachanganya tu kwanza shyna aliangua kicheko alicheka mno yaani alimuona Nagma kama punguani amechanganyikiwa mno ata tajabu alicheka

"Nagma tulia hapa Sawa njoo "

Rajabu alizungumza na kumshika nagma vizuri na kumlaza kifuani kwake

"Rajabu Lily ni mtoto wako mtunze mtunze sana nahisi Maisha yake yako hatarini"

Alizungumza tena nagma lakini hakuna mtu aliweza kuchukulia hayo maneno kuwa ni serious kila mtu aliwaza kuwa nagma amechanganyikiwa tu...

Rajabu alimtuliza nagma mwisho akalala hapo akapata na nafasi ya kumpeleka chumbani kwake na kumlaza kisha rajabu akarudi kulala sebuleni maana hakuwa amekabiziwa chumba alichoshukuru ni kwamba alipata sehemu ya kupumzika yeye nadogo wake, usiku wa rajabu ulikuwa mzito sana aliwaza na kuwazua pasi nakupata majibu sahihi mawazo yake yalikuwa ya hali ya juu

Asubuhi na mapema upande wa maimuna nyumbani kwa dokta Matias, maimuna aliamka na kuanza kufanya usafi na kujishughulisha kama mke bora hivi

"Shikamoo mama "

"Marahaba mwanangu jamani mbona unajisumbuq usafi uwa kuna mtu anakuja kutufanyia ungeacha "

"Amna mama ni wajibu wangu "

"Haya na huyu mwenzio yuko wapi ??"

"Yuko ndani, mama Matias bado ana hasira na mimi, naomba ongea nae, Mimi ninachotaka ni ifadhi tu 🥹 mpaka pale nitakapojifungua au naendelea kutafuta ndugu zangu nikiwapata tu naondoka "

"Uondoke uendee wapi na mjukuu wangu huyo Matias asikutishe....."

"Mama mjukuu gani unaongelea ? Nasemaje natoka naenda kazini nikirudi nisikukute, mama huyu anaigiza anajiliza hakuna kitu cha kweli kwake, hakuna kitu sijamfanyia mai nilimpenda sana lakini nilikuja kumchukia baada ya kujua kuwa mimba sio yangu yaani uwezi amini hospital nzima wanajua kuwa nampenda mai nilimtambulisha kwa kila mai nasema uongo au ?? Lakini bado akanicheat yaani mimba ni ya mpiga debe ambaye kaadhilika na madawa uko lakini bado alikuwa akimtaka kaka yake kimapenzi au sio wewe ??"

Dokta Matias alionekana kujua mengi sana juu ya maimuna, kwanza mama mkwe akachoka na kukaa chini maana daaah, maimuna akapiga goti akiwa analia sana

"Nisamehe Matias kwa kila kitu ni shetani alinipitia lakini kuhusu ujauzito ni wako "

"Sitaki kuonekana nakuonea ebu mama sikiliza hii "

Matias alitoa simu yake na kuweka audio

"Usijali me nakupenda mno lakini hakikisha kuwa una achana na madawa, na hii kazi ukatafute kazi ya kueleweka sawa kipenzi tuje kumlea mtoto wetu kwa pamoja kilichobaki kwa dokta Matias nitamuacha Alee ujauzito nikijifungua namlia pesa za mwanzo na kumfilisi kabisa nije kuinjoy na wewe kipenzi "

Matias aliamua kustopisha sauti ile maana aliona kuwa ni mambo ya aibu sana

"Nafikili siitaji kuongea tena mama nachelewa kazini we kunguni nisikukute hapa "

Matias aliondoka na kumuacha mama yake akiwa na maimuna mama yule alimuangalia sana maimuna mwisho akazungumza

"Binti chukua begi yako tutoke nje nataka kufunga nyumba yangu "

"Kwanini ufunge mama ? Mimi nipo hapa nitakuwa naangalia kila kitu na nitawaandalia chakula "

"Weeeh cheza na mjinga wako Matias sio mimi ebu changanya miguu yaki nje "

Nyie mama mkwe pambe hatari kwanza hana maneno mengi ni hatua moja mbele

"Fanya haraka bhana kwanza umekuja na kunguni wako kwenye nyumba yangu mai kama usichana wako unashindwa kuutumia vizuri utazeka ukiwa unaangaika tu "

"Mama.......🥹"

Alilia maimuna kwa kuita mama

"Nani mama yako ?? Me naweza nikazaa kahaba kama wewe ?? Toka nje nimesema "

Mama yule alimuita mlinzi ambaye alimvuta maimuna mpaka nje na kumtupia begi lake kisha mama yule akapanda kwenye gari yake

"Maghati huyu asiingie ndani na wala hapa nje nisimkute "

Alitoa amri kwa mlinzi wake kisha akawasha gari na kuondoka....

Upande Rajabu alijiandaa na kwenda kazini alipofika akaitwa na meneja

"Naona sasa hivi umekuwa boss sio ?? Unakuja unavyotaka leo ukiamua unakuja kazini ukiamua hauji sio ?? Haua boss watu wanataka mishahara yao "

"Amna meneja ni mambo magumu tu ambayo napitia kwa sasa lakini kila kitu kitakaa sawa "

"Kuna elfu 50 yako hapa ya mshahara pesa nyingine tumekata kwenye hasara ulizoingiza kwenye bar yetu kuvunja glass na vitu vingine na mwanzo mwisho leo kukuona kwenye hii bar nikija kukuona hapa labda uje kama muhudumu "

Alifokewa sana siku hiyo rajabu wa watu, alichukua pesa yake aliyoambiwa kisha akaanza kuondoka

"Kabla ujaondoka kwa siku ambazo haukuja pesa yako tumejumlisha umo hivyo basi utafidia kwa kitudekia ukumbi wa chini "

"Unakichaa wewe nyo nyo nyo nyo nyooooo kumbavu nisije nikakuchota mtama mie na huo ufupi wako toka nipite "

Alifoka rajabu weeh meneja mwenyewe alisogea kwa heshima zote maana anamjua rajabu vizuri kwani yeye ndiye uwa anatulizaga vulugu zote zinazotokeaga na hakuna mtu anaweza kumgusa....

"Halafu sikia mwambie boss wako na wewe mwenyewe msinizoee "

Rajabu alirudi nyumbani akiwa na mawazo sana alikuta shyna akiwa anacheza na lily na nagma alikuwa akiangalia TV

"Eeeh mbona mapema mwenzetu ??"

Aliuliza nagma baada ya kumuona rajabu, hapo shyna na Lily wakageuka kumuangalia rajabu ambaye alifika na kukaa chini katibu na nagma......

"Nagma nakuomba tuongee nje mara moja "

Nagma hakujibu kitu zaidia alimshika mkono Rajabu na moja kwa moja wakaelekea chumbani kwa nagma

"Haya zungumza najua ukutaka kuzungumza mbele ya mdogo wako wala mwanao "

"Nagma please hapa nilipo nimechanganyikiwa vya kutosha na wewe unaniletea drama zingine kwanini unakazana kusema kuwa lily ni mwanangu naomba acha hizo sawa uko na shida na mume wako lakini hiyo sio sa babu ya kumbadilishia mtoto baba "

Alilalamika rajabu

"Rajabu najua najua kama umefukuzwa kazi nimepat ujumbe kutoka kwa mtu wa reception ni rafiki yangu lakini pia naomba ujue kuwa sikuwai kufunga ndoa na yeyote yule lakini nafikili muda sahihi umefika wa lily kuwa karibu na baba yake "

"Unanichanganya nagma kaa kimya kimya kimyaa kuchwa changu kinawaka moto "

"Rajabu me sio nagma, me ni shenaya wako.....🥹 "

Hawa nao wanatuchanganya sasa ata me sielewi au wasomaji mnaelewa ??

ITAENDELEA....
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 12

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO.......

Rajabu aliposikia jina la shenaya alishtuka sana haraka akamuachia Nagma maana alikuwa amemshika akasogea pembeni kabisa rajabu alianza kutetemeka uku machozi yakimtoka alikosa nguvu na kukaa chini, nagma aliinuka pale kitandani na kutaka kumfata lakini Rajabu alimzuia kwa kumnyooshea mkono

"Rajabu....."

"Nagma sawa nakaa kwako lakini usinifanyie haya mambo please, unajua jini kuhusu shenaya ?? Unajua nini kuhusu yeye, sasa nagundua kitu nagma unanijua na kuna kitu unanichunguza si ndio ??

"Unaongea kuhusu nini Rajabu nakujua nakujua mpaka nakujua tena na hakuna mtu wananijua mimi kama ambavyo unanijua wewe "

"Nagma kimya me sikujui "

Rajabu alionesha kuchanganyikiwa sana alitoka nje alilalamika kwa sauti ya juu sana mpaka mlinzi akawa anamshangaa

"Aaah madamu boss huyu rafiki yako ni mwezi mchanga si ndio ??"

Aliuliza mlinzi swali ambalo lilimchukiza Nagma, rajabu alimuamsha mdogo wake yaani shyna

"Naomba paki mizigo yako tu naondoka hapa "

"Kaka tunaenda wapi jamani tuanze kuzurula mtaani au ??"

"Nimesema chukua mizigo yako tuondoke "

Mwaya shyna wa watu maisha yalishamnogea hakukuwa na kuuza mboga tena mtaani msosi mzuri maisha safi muda wote full kiyoyozi halafu kaka analeta mambo meusi

"Rajabu please please nisikilize basi nisikilize Kosa langu nini kukuambia ukweli au ?? 🥹 ulitaka nikae na iki kitu moyoni kininyonge ?? Ujui tu nimeangaika kukutafuta sana mpaka siku nimekupata nilifurahi sana, siku ambayo nimejua wewe ndio rajabu wangu nilihisi kuchanganyikiwa nilitamani kukumbatiw lakini najua ningeonekana kichaa kama ambavyo unaniona sasa hivi 🥹 najua unajua kuwa shenaya amefariki lakini hapana Rajabu wangu me naishi....."

Aliongea nagma kwa masikitiko na sauti ya maumivu ndani yake kiukweli mpaka muda huo rajabu hakujua nini afanye halafu mwenzangu na mimi yaani shyna ndio aelewi ata watu hao wanaongea kuhusu nini....
Rajabu alimsogelea nagma kwa hasira sana akamshika mkono na kumvuta mpaka chumbani alipofika hakuangaika sana alichofanya ni kitumia nguvu na kuchana mavazi aliyokuwa amevaa Nagma hapo rajabu aliishiwa nguvu kabisa alirudi nyuma kwa nguvu na kujigonga ukutani muda wote huo nagma alikuwa amefumba macho machozi yakimtililika

"Inawezekanaje ?? Yaani hii sio sawa no no no wewe sio shenaya "

"Lakini hiyo tattoo ulinichora kwa mikono yako, rajabu wewe ndio uliniambia kuwa mimi na wewe tukiunganisha majina yetu tutapata mtoto wetu mzuri sana wewe ndio ulisema kuwa mtoto wetu akizaliwa tutamuita Raya au sio wewe ?? Ukimaanisha kuwa ulinichora tattoo ya mtoto kabla hata ajazaliwa rajabu sikuwa najua kuchora lakini ukaniambia nikuchore jina la mwanao 🥹 nilikuchora vibaya ingawaje ulikuwa umepitia maumivu unajua uliniambia nini ?? Jina la mwanao ndio kila kitu kwako nakumbuka siku ya mwisho uliniambia kuwa katika wanawake Mungu amewaumba kwaajili yako basi ni mimi, shyana mama yako na Raya, ulikuwa ukimtaja sana Raya ingawa kipindi iko alikuwa akicheza ndani ya tumbo langu najua unajiuliza imekuwaje mtoto nimempa jina la lily mama yangu alimrithisha jina lake kipindi iko nilikuwa hospital kwaajili ya surgery, mtoto wangu mwenyewe nimeanza kumshika akiwa na mwaka 🥹 nilipoamka kwenye usingizi mzito basi akili yangu ilikuwa juu yako na binti yetu tu "

Aliongea sana nagma wa watu uku akilia sana Rajabu alimsogelea na kumkumbatia kwa nyuma alimkumbatia kwa muda mrefu sana

"Leo najihisi na mimi ni binadamu ujui tu rajabu hii siku nimeisubili kwa muda gani "

"Usizungumze Nagma "

"Kwanini unaniita nagma ?? Niite jina lako pendwa shenaya lakini pia ukitaka kumbabadilisha jina lily wako mbadilishe mfanye kuwa Raya wa ndoto zako "

Nyie hawa mbona kama wananichanganya ila mahaba yao sasa yananifanya nijione yatima wa mapenzi Rajabu mwingine aje tupendane.


NARUDI....
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 13

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO.......

Rajabu alitumia muda mrefu sana kumtuliza Nagma na kweli akatulia

Upande wa pili shoga yetu maimuna kazurula mitaa yote kila mwanaume wake aliyeenda alimkata akiwa ameshachoka na kukata tamaa alikumbuka na kuamua kurudi kwa mama rukia

"Makubwa......"

Alizungumza mama rukia baada ya kumuona maimuna

"Shikamoo mama....."

"Eeeh wacha weeeh na cheo nimepewa, nambie maimuna "

" nimekukumbuka sana, nikakumbuka na ndugu zangu nimekuja kuwaona "

"We umenikumbuka mimi au ? Ebu subili kwanza umenikumbuka na hayo mabegi yako au ??"

" mama rukia bhana "

Alijichekesha maimuna uku akiangalia uku na uku alitumia muda mwingi kuangalia nyumba yao iliyobomolewa ambayo kwa muda huo mafundi walikuwa bize na kichimba msingi wa Ramani mpya

"Kaka rajabu na shyna wako wapi au wametoka ??"

"We wale ndugu zako ??"

Yaani ma rukia alikuwa na majibu ya hapo kwa hapo

"Acha hizo mama rukia nimechoka ujue, nikaribishe basi, niweze kuzungumza na ndugu zangu "

"Mtoto huna haya wewe wala hujui vibaya, yaani kwa yule ambaye umemsema na kumtukana ukampa matusi yote, nikuambie kitu maimuna kati matusi yote tusi ambalo silisahau ni wewe kuniambia kuwa Nina mahusiano na Rajabu sikutaka kusema yote haya lakini pia niseme tu kuwa wewe kuwa yatima yaani kuwa mtu ambaye haujui ndugu zako upo upo tu unastahili kabisa na kama ndugu wapo bora wasijitokeze "

"Mama rukia mbona unaniambia maneno mazito sana ?? ata mimi ni binti sijapishana sana na mabinti zako sikupenda kuwa hivi mimi napenda sana kuwa na ndugu zangu, napenda sana kujua mama yangu,.kwanza kabisa naomba niambie ndugu zangu wako wapi ??"

"Ata me sijui wako wapi na wanaishi wapi wnaafanya nini sijui kwakweli "

"Unamaanisha hapa hawapo ??"

"Me mwenyeewe nina chumba na sebule ulitaka niwaweke wapi ? Kwanza unanipotezea muda ondoka "

Maimuna akapiga magoti akilia sana akiitaji msamaha na msaada kutoka kwa Mama rukia maana mpaka alipofikia hakuwa na msaada wa watu wengine....

Kelele za maimuna ziliwashtua majilani, walimzunguka maimuna ambaye aliendelea kulia na kuomba huruma ya mama rukia lakini mama rukia alikataa kabisa mpaka pale mwenyekiti alipomuomba mama rukia kumpokea tena maimuna.

Siku mbili zilipita ikiwa ni majila ya saa 1 usiku Nagma akiwa amekaa na familia yake mpya muda huo walishapata chakula cha usiku hivyo walikaa kuangalia TV wakipoteza poteza muda lily muda wote alikuwa kwenye mikono ya shyna yaani hakutaka kumuacha ata dakika....

"Weeh lily ebu muache antie sasa kaaaah muda wote uko mikononi "

"Muache bhana da nagma....."

"Nimekumbuka "

Alizungumza rajabu na kila mtu alimgeukia akisubili asungumze

"Shyna....."

"Abeeh kaka "

"Ata sijui naanzia wapi lakini naomba niende moja kwa moja, lily ni antie yako "

"Si ndio mbona ananiita antie tangu siku ya kwanza "

"Sijamaanisha hivyo namaanisha kuwa lily ni mtoto wangu mimi na wewe ni shangazi wa ukweli kabisa "

"Ahahahaha thubutu "

Shyna ni mimi kabisa aligoma kukubali

"Kwa ubishi sikushangai kwakuwa umezaliwa nao, najua unajiuliza kama lily ni mtoto wangu kwanini sikumleta kwa mama enzi za uhai wake, kiukweli nimejua juzi tu kuwa lily ni mtoto wangu, unajua nini siku ya kwanza nilihisi kuwa Nagma amechanganyikiwa lakini alikuwa na akili timamu huyu sio Nagma kaka unavyojua huyu anaitwa shenaya....."

"Subili kwanza, kaka naogopa natetemeka shenaya ni mwanamke wako ambaye aliwai kufariki ? Nakumbuka uli......"

"Najua unachanganyikiwa lakini nimeshajua ukweli nakuambia kila kitu mdogo wangu "

"Rajabu acha nitamwambia kila kitu....."

Alijibu Nagma kisha akakaa vizuri na kuanza kutoa hostoria ya nini kilitokea uko nyuma....

"Mimi ndo shenaya kama mnavyojua since familia yangu imekuwa ni yenye pesa mingi na mambo mengine tumekuwa tukikumbwa na na matatizo mengi sana aswaah ya chuki tulichukiwa mno, na adui zetu ni wale wafanybiashara wakubwa ambao walikuwa wakijumuika na baba katika plan zao za kuchukua kila kitu chetu kwanza kabisa walipanga kunimaliza mimi kwakuwa ndiye mrithi pekee wa mali za familia 🥹 nakumbuka nilishawai kunusulika kunywa sumu kwenye juice akiniwekea kwenye juice kwa kulipwa na watu hao lakini Mungu mkubwa sikunywa nilijua hayo nikiwa marekani, mara ya pili ilikuaa ni kipindi kile ambacho rajabu ulipambana na wale waliotaka kuniteka ndio maana nashindwa kukusahau mara ya tatu ndio ile tindikali ambayo iliharibu uso wangu na sehemu kubwa ya shingo yangu, niliwaishwa hospital na kwakuwa pesa zipo baba yangu akafanya utaratibu nikaamishwa nchi kimya kimya na taarifa za kifo changu kuzagaa, najua Rajabu uliumia sana, nilifanyiwa surgery na ilienda powa nikapatiwa sura mpya ambayo mnaiona sasa, imechukua muda sana kuwa hivi kipindi kile ambacho nilikuwa nimemwagia tindikali ndio kipindi ambacho nilikuwa na ujauzito rajabu alishatoa jina kwa binti yake, tulipanga mengi sana na rajabu "

Nagma akaanza kulia kwa sauti

"Kinachoniuma ata mama mkwe hakuwai kunijua hakuwai kumuona mjukuu wake shyna wifi yangu uwezi amini mtoto wangu nimekuja kumuona akiwa na mwaka mmoja na miezi 8 yaani nilijifungua kwa upasuaji tena kabla ya muda 🥹 hii yote kwaajili ya matibabu makubwa niliyokuwa nikiendelea nayo, nilipokuwa sawa nilibadilishwa Uraia na ata jina uwezi amini wazazi wangu wanaiogopa nchi yao kwa sasa ata mimi naogopa lakini hakuna mtu wa kunijua nashukuru ilo na nilirudi kwaajili ya kumkutanisha lily na baba yake lakini pia kumtafuta mtu nimpendaye, najua unawaza kwanini nilikuaa nikiishi na mtu mwingine, nimeishi nae tu lakini bado nilikuwa nikikutafuta tangu nimeishi na huyu mwanaume ni mateso tu.....

Basi shyna alimsogelea na kuanza kumbembeleza wifi yake

"Hujui tu natamani kulipiza kisasi kwani nawakumbuka waliofanya hivi, nakumbuka sura ya mtu ambaye alinimwagia tindikali 🥹 na namuona kila kona, lakini nani atanielewa nani atajua kuwa mimi ni shenaya familia yangu kila siku inaniambia niondoke lakini naondokaje nishapata familia yangu sidanganyi moyo wangu una kidonda kikubwa "

Lily alikua akilia tu baada ya kumuona mama yake analia

"Njoo mwanangu "

Rajabu alitaka kumbeba lily lakini lily alikataa rajabu aliumia mno lakini alielewa ilo...

"Nimekumbuka "

"Nini tena ??"

Alizungumza nagma na rajabu akauliza

"Kwakuaa familia yangu imekamilika sina budi kumchkua Raya aje kuishi na sisi hapa nyumbani "

"Raya ??

Rajabu alishtuka sana maana jina ilo alipaswa kupatiwa lily lakini leo anatajwa mtu mwingine ambaye hakuwa akimjua

"Ndio Raya ni mtoto wa maimuna namaanisha mtoto binti aliyeokotwa na mama yako 🥹 sijui kama mtanielewa nachanganyikiwa kabisa....."

Ata me mwandishi nachanganyikiwa bhana .

ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 14

WHATSAPP: 0676604830

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO......

"Nagma acha kulia kwanza halafu tuelewane unaongea kuhusu nini ?? Yaani mtoto wa maimuna sijui anaitwa Raya sijui maimuna ndugu yenu me sikuelewi unaongea kuhusu nini ??"

Muda huo rajabu uvumilivu ulishamshinda maana nagma analia sana halafu anavyoongea avieleweki

"Kaka, kaka polepole basi mbona unamfokea sana "

"Ananikera, ukweli nagma unanikera uongei mambo yakaeleweka "

"Sio rahisi kunielewa lakini ndo hivyo maimuna ana mtoto ambaye ana miaka miwili 🥹 maimuna amezaa na mwanaume ambaye nilikuwa naishi nae hapa "

"Eeeeh nakuwa chizi sasa hivi shyna sikia mpeleke huyu ndani nitampiga mbao hapa bure "

"Jamani kaka kwani si polepole msikilize kwa makini utamuelewa"

Shyna alimsogelea Nagma na kumshika mabega

"WiFi yangu tulia nyamaza basi nyamaza "

"Usijali shyna niko sawa, rajabu anashindwa kunielewa subili niwaulize kwani nyie hamjui kua maimuna aliwai kuwa na mtoto si mmekuwa mkishi nae kwa miaka ??"

"Unanivuluga bhana walahi Nagma unaweza kuniona me nina hasira au sina akili lakini nikuambie maimuna hakuwai kuwa mjamzito ata mara moja mimba ya sasa hivi ndio ya kwanza

"Subili maimuna hakuwai kutoka nyumbani ata mara moja ??"

Aliuliza nagma akadakia shyna

"Nakumbuka aliwai kutoka mwaka juzi alisema amepata kazi arusha lakini alirudi baada ya miezi kaka 11 hivi akidai kuwa boss wake anamtesa "

"Ndio na mimi ndio nilimtumia nauli ya kurudia baada ya kunipigia akiwa analia sana kuwa anataka kurudi "

"Walahi maimuna ni jambazi tena professional, kitu ambacho hamkijui kipindi iko maimuna alikuwa naishi na mwanaume wangu huyu uko masaki tena mimi ndo nilikuwa nikitoa pesa nakumbuka huyu mwanaume aliniomba pesa ya biashara na alisema kuwa kuna mzigo anaufata nje nilimpa pesa nyingi sana akaondoka kuna siku katika tembea tembea zangu nilikutana nao wakiwa wanaingia super market sikuamini nikawafatilia na kujua kuwa wanaishi pamoja niliumia mno kwakuwa account niliyomuwekea pesa nilimfungulia mimi niliifunga na hapo hakuweza kupata pesa nilimblock whatsapp nikamblock kila kona hakuweza kupata mawasiliano na mimi hawakuwa na pesa ya matumizi wala ya kufanya chochote kile, maisha yalizisi kuwa magumu Sana, mai akajifungua mtoto lakini alikuwa na shida na ingewaghalimu pesa kubwa sana baada ya mwezi mai alichofanya ni kumtoloka mwanaume na mtoto nahisi hapo ndo akarudi nyumbani kwa stahili ya kusema kuwa anateswa na boss wake mwanaume wangu namjua nilikuwa namfatilia sana alichokifanya ni kutaka kumuua mtoto 🥹 mimi jamani uwiii naogopa na umri wangu huu nimeona mengi mno msione nimekaa hivi namtafutia kitu huyu mwanaume namfunga, nashukuru Mungu niliweza kumuokoa yule mtoto yupo anaishai 🥹 na kwakua familia yangu imekamilika nitamtoa aliko na kumrudisha nyumbani mai anajua mtoto alifariki kutokana na maelezo ya mume wangu, lakini mume wangu pia anajua kuwa mtoto alifariki baada ya yeye kuwasha moto chumbani na kumuacha mtoto ndani niliwai sikuogopa moto "

Daaah Rajabu alihisi kuchoka zaidi akamsogelea Nagma wake na kumkumbatia

"Najivunia wewe, najivunia wewe mwanamke wangu shenaya we ni zaidi ya mwanamke "

Nyie we ushawai kuambiwa kuwa we ni zaidi ya mwanamke au ?? au basi nisiwakele....

"Shyna, naomba kaa na kila mtu hakikisha hawatoki nje kuna sehemu naenda "

"Unaenda wapi ??"

"Kwani mpaka ujue we tulia hapo nimesema waangalie maswali mengi ya nini ??"

"Hakuna kwenda mahali nakujua hapo uko na hasira ya kwenda..."

"Shyna nitakuwasha mabao "

Lakini shyna hakumuelewa kaka yake zaidi alienda kufunga mlango na kuchukua funguo, rajabu alichukia na kutaka kumpiga shyna

"Wifiiiiii....."

Alipiga kelele shyna na Nagma akatoka chumbani mbio

"Nini jamani ??"

Shyna alimuwai wifi yake na kukaa nyuma yake

"Mwanaume wako anataka kunipiga unajua anataka kutoka kwenda kumtafuta maimuna "

"Rajabu jamani mbona unadiliki wewe ??

"Niweje rangi nyeupe au blue, nipe funguo hizo "

"Shyna nenda ndani wifi yangu huyu niachie mimi"

Basi shyna akafata maelezo ya wifi kama wifi, Nagma akamsogelea baby wake

"Ni kweli una hasira kiasi hiko ?? Na haunimisi ata kidogo "

"Unaongea kuhusu nini nawe ebu niache usiniguse nagma nitakupiga "

"Haya baba niko hapa nipige "

Nagma alimvimbishia kifua Rajabu na hakuacha kumchokoza mwisho rajabu akacheka na kumnyanyua baby wake moja kwa moja chumbani, hakuna mkate mgumu mbele ya chai....

Siku iliyofuta maimuna na rajabu walifunga safari mpaka kwenye kituo cha watoto yatima.

"Eeeh jamani tutammisi sana Raya wetu uwe una mleta acheze na wenzie "

"Usijali madamu"

"Pole baba "

"Aaah Asante mama "

"Pole sana mwaya umeumwa mda mrefu mpaka mtoto amekuwa mkubwa miaka miwili sio mchezo "

Alizungumza muhusika mkuu wa kituo iko rajabu aliitika tu ata hakuwa akijua wanaongea kuhusu nini akiitika kwakuwa Nagma alikuwa akimpa ushara kwa kumkanyaga miguuni

"Mama......."

Alikuja binti mdogo ambaye hakuwa na tofauti na maimuna jamani walifanana sana hadi rangi rajabu akubaki akiwa ametoa macho, muda wa Raya kuondoka ulifika na rajabu ndio alimbeba kwani alitambulika kama baba Raya alifurahi sana akiamini kuwa Rajabu ndio Baba yake ambaye alikuwa akimsubilia kwa muda

"Mama lily mbona hajaja ??"

Aliuliza Raya ambaye alionekana anaongea sana

"Eeeeh maimuna kajizaa walahi lakini asiwe Amejizaa na tabia "

Alizungumza rajabu muda huo walikuwa kwenye gari

"Rajabu maneno gani jamani kaaaah "

"Haya basi ma mchungaji nisamehe kwanza subili yule mama alikuwa anaongea nini na ulikuwa unanifinya na kunikanyaga tu "

"Ahaha sema mshikaji wangu umecheza kama Pele, unajua kituo cha watoto uwa hawapokei watoto kijolela nilivyomleta kwakua alikuaa mdogo nilitoa sababu kuaa familia yangu iko nje na wewe mume wangu uko Hoi mahututi na hauna mtu wa kukuangalia zaidi yangu nilidanganya hivyo ili aweze kulelewa pale na kumuweka mbali na kila mtu "

"Sizani kama umeweza kumuweka mbali na kila kitu yaani huyu mtoto amefanana kila kitu na maimuna "

"Unataka nifanye nini Rajabu ?? Nachoka mimi ujue nachoka naishiwa nguvu lakini lazima niishi na huyu mtoto Raya ananipenda mno "

Ukimya ukatawala na safari ilikuwa ni kurudi nyumbani....

ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 15

MAWASILIANO: 0783642467

SONGA NAYO...........

Rajabu na familia yake walifika nyumbani wakiwa na binti yao Mpya ambaye ni mtoto wa maimuna aliyekuwa akiitwa Raya

"Oooh my God lily uwiiiih nilikukumbuka sana "

Alipiga kelele za furaha Raya, shyna alibaki akimshangaa mtoto yule akamshika mkono kaka yake na kusogea nae pembeni

"We kaka mbona maimuna kajizaa ??"

Alivyouliza hivyo rajabu akaangua kicheko uku machozi yanamtoka

"Sikuelewi unalia unacheka "

"Ilo swali na mimi nilimuuliza Nagma tukiwa njiani uwezi amini wamefanana hadi sauti na anaongea mama chiriku yaani hapo ni kasheshe....."

"Mmmmh eti nimeambiwa huyu wa nje ndio baba yangu ndo alikuwa ana umwa lakini mbona ye mweusi sana "

Alisikika mtoto wa maimuna vya kurithi vinazidi

"Ata mimi mama kaniambia huyu ndo baba angu ila analia Lia huyo muda mwingine anafoka "

"Eeeh achana na kufoka analia kama wale watoto wa kituoni kwetu au ??"

"Aaah sio hivyo yeye analia na sauti yakw kubwa halafu inakwangua kama hivi aaaaaaaaaaah "

Nyie hawa watoto wamenishinda tabia yaani walikuwa wanapiga story utazani ni watu wazima kabisa muda huo Nagma, rajabu na shyna walisimama tu wakiwasikiliza wenyewe walikuwa bize hawana ata habari kuwa kuna watu wanawaangalia na kuwasikiliza

"Yaani umu ndani kunabowa mdada mzuri ambaye Alii hovyo ni antie shyna kwanza mpole halafu anaupendo mama, anaupendo lakini muda wote analia Lia kama mtoto halafu baba anamwambiaga mama kachanganyikiwa "

"Umeona sasa nagma ulikua unanivuluga mno leo hii tumekuwa kivutio cha stori kwa hawa watoto "

"Kwahiyo me ndo chanzo sio ??"

"Ndio kwani ujioni ?? ila watu wafupi mnashida sana "

Alitania rajabu na Nagma akaanza kumkimbiza wakakimbilia chumbani kwao

"Haya Waone kama watoto wadogo waje kuanguka "

Alizungumza Raya na wote wakacheka

"Mtoto mzuri mambo ??"

"Naitwa Raya sio mtoto mzuri "

"We Raya huyu ndo antie shyna usimjibu hivyo ni antie yangu mzuri "

" ni antie yako me anihusu chumbani kwako wapi nikapaone maana tangu nimefika sijui natakiwa kwenda wapi "

"Usijali Raya nitakupeleka antie yako niko hapa haya twende watoto wazuri "

"Huyu shangazi yako ata sijampenda "

"Ni antie sio shangazi We mbona hivyo ?? Halafu umeanza kuwa na bad manners kwa wakubwa si ndio ??"

"Niache bhana "

Kivumbi iki walahi yaani ni kama maimuna karudi upga kwa kasi ya 4g kulaleki mtoto anaongea kama kalishwa usembe...

Asubuhi na mapema kama kawaida Rajabu alikua wa kwanza kuamka maana usingizi wake ni wa kuotea otea tu kutokana na kua na mawazo mengi sana yasiyoelezeka hivyo uwa anawai kuamka na kufanya shughuli zote za nyumbani na kuandaa kifungua kinywa....

"Kaboss bhana ila madamu wangu anajua kuwalea bhana kasoro weee kidogo nakuona unajituma ata kukata maua "

Walahi muacheni Rajabu awe na stress tu anadharauliwa hadi na mlinzi wa getini

"Masai hizi kazi nafanya ili kukupunguzia wewe upate muda wa kupumzika lakini pia kama una muda wa kukaa na kufatilia maisha yangu nafikili hii kazi ungeendelea nayo mwenyewe "

Alichukia rajabu akaweka vifaa chini na kuanza kuondoka

"Aka nako kangekuwa kabosi ningekoma mimi kautani kadogo tu kachukia kama sio mwanaume "

Rajabu aliingia chumbani akavaa na kuondoka alizunguka uku na uku kutafuta ajila lakini ilikuwa shida sana kupata akapakumbuka nyumbani kwao akaona sio mbaya kama ataenda kumuona mama rukia

"Eeeh jamani Rajabu mwanangu eeeh nilikukumbuka sana sema tu ndo hivyo simu yangu imeingia kwenye maji "

"Ata mimi nilikukumbuka ndio maana nimekuja shyna pia anakusalimia sana "

Wakiwa bize na story za hapa na hala rajabu alishtuka kusikia sauti ya maimuna kutokea upande wa pili ambao ni upande wa jiko

"Mama umesema hawa danga nichanganye na tembele au ?? "

"Ndio pika haraka mgeni ale "

Subili hiyo ni sauti ya maimuna au ni mimi nachanganyikiwa ??

"Ni yeye mwanangu ndo nilikuwa nataka kukupa taarifa sema sasa hivi anebadilika na anajitambua sana sana, kila siku anawakumbuka kama juzi jana asubuhi ameenda makaburini kwa mama yako kusafisha "

" nacheka kama mazuri mama rukia umempokea huyu mtu ?? nikupe hongera yako na pole maana hapo anavuta sumu yake ikijaa shingoni lazima akutemee kweheri mama nashukuru kuwa nimekukuta uko salama "

"Jamani rajabu ndo unaondoka "

"Huyu mtoto wako Mpya namuogopa kama ukoma apa tupu kuna kopi yake kule inanienyesha nikikutana na yeye rajabu mimi nakuwa kuchaa "

Alizungumza rajabu na kuondoka kwa mwendo wa haraka mama rukia alibaki akishangaa tu pasi na kuelewa ata neno moja kutoka kwa rajabu....

"Nimesikia unaitilia jina la rajabu "

Aliuliza maimuna baada ya kutoa jikoni mbio mbio

"Umbea tu kapike uko "

"Jamani mama "

Rajabu alirudi nyumbani akiwa kama kachanganyikiwa vile.....

ItanipitaKWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 16

Mawasiliano: 0783642467

Songa nayo.......

Rajabu alirudi nyumbani moja kwa moja akaenda chumbani na kumuita Nagma

"Kuna nini jamani me naandaa chakula kule ? Kwanza umeondoka asubuhi bila kuaga umenikera ujui tu "

"Naangalia vibarua uko siwezi kukaa tu nyumbani "

"Si nilishakuambia kuwa kazi nitakutafutia tena sio kukutafutia nakuunganishia moja kwa moja, Rajabu najua iki kipindi kichwa chako kijo less sana ndio maana nataka upumzike utulie na kuwa sawa "

"Niko sawa nilichokutana nacho Leo ni mawazo matupu "

"Unaona sasa ata taarifa zako sio nzuri ni stress muda wote, Rajabu subili nikuambie mimi ningekuwa mtu wa kupaniki kama wewe nakuambia sasa hivi ningekuwa chini tena wa jalalani, nina mengi sana kichwani mwangu najua adui zangu wote na wamenizunguka na naishi nao pasi na wao kujua kuwa mimi ndo yule ambaye walinikosea na bado nakosewa kila siku lakini sijaruhusu mambo yao yanipe presha na namna hiyo "

"Unaongea tu nimekutana a na maimuna anaishi kule kwa mama rukia "

"Kwahiyo kama anaishi kule ??"

"Kwanza ilikuwaje umefika kule ? Rajabu mume wangu we ni mbishi toleo oa mwisho kabisa kaah "

"Eeeh basi nawe mke wangu "

"Ebu niache mtu sina amani na mwanaume wangu kila tukikaa ni habari za mawazo "

Alizungumza nagma na kutoka nje

"Ila ni kweli namkosesha amani Nagma wangu lazima nimfanye mwenye furaha na amani....."

Kwakuwa rajabu alichoka sana alijilaza kwenye kochi lililopo pembeni ya kitanda chao na kulala

"Eeeh huyu jamani "

Alizungumza Nagma baada ya kumkuta rajabu akiwa amelala akamshtua kwa kumtikisa

"Amka amka amka we baba wewe ata kuoga kweli "

"Aaah me nilijua unaniamshia mambo ya maana labda chakula kimeiva unaanza kuniambia mambo ya kuoga mwili wenyewe wa udongo nikimomonyoka ??"

"Una wazimu kweli kaoge uko "

"Halafu we mbona kama "

"Kama nini malizia unataka kusema kuwa nakufanya kama mtoto sio ?? "

Rajabu hakujibu zaidia alimnyanyua Nagma ambaye na yeye alikubali kubebeka

"Kwani saaa hivi una kilo ngapi ?? maana nahisi uzito unanizidia "

"Tabia mbaya hiyo nibebe vizuri "

"We unataka kunivunja nini kwenye mwili wangu yaani hapa najikaza ili nikuangalie mke wangu kwa juu ulivyokuwa mzuri walahi uliumbwa mwezi wa 12 "

"Unaupenda sana msemo wako huo "

"Ni kwaajili yako tu "

Rajabu akiwa amembeba nagma aamkaingia nae bafuni wakaoga kwa pamoja na kutoka....

Majila ya usiku wakiwa chumbani walishangaa sana kusikia mlango wao ukigongwa mfululizo walishtuka na kuwai kwenda kuangalia kuna nini

"Nyie tena ??"

Alichoka Nagma baada ya kuwaona lily na Raya ndio walikuwa wakigonga

"Tunataka kulala na ninyi "

Nagma na Rajabu waliishia kuangaliana tu na hawakuwa na budi zaidi ya kuingia nao chumbani kwa usiku huo waliweza kutumia muda mwingi na mzuri na watoto wao

"Natamani mama ungekuwa hapa uone furaha za wajukuu zako, najua ungempenda Raya kama ambavyo ulimpenda maimuna"

Alizungumza rajabu kimoyomoyo mwisho watoto walipitiwa na usingizi na wakalala nao....

Asubuhi na mapema kama kawaida rajabu aliamka akaandaa kifungua kinywa na kufanya usafi wa nyumba

"Shikamoo kaka"

Alisalimia shyna baada ya kukutana na kaka yake sebuleni

"Marahaba hali yako ??"

"Salama naona leo umechangamka sana"

"Sana, kwanza nikuulize ilikuwaje ukawaacha watoto usiku wakaja chumbani kwetu "

"Sasa si walitaka wazazi wao me nifanye nini "

"Sa........"

Kabla rajabu hajamaliza maneno yake alikuja Raya

"Kulala na baba raha sana leo nitalala nae tena "

Rajabu alibaki akimuangalia shyna tu maana hakuwa na jibu zuri la kumpa Raya

"Baba kati ya mwanao mimi na Raya unampenda nani ??"

Muda huo huo Lili alifika na kuuliza swali, rajabu akachuchumaa na kuwanyanyua watoto wote

"Eeeeh Baba baunsa "

Alipiga kelele Raya

"Umeuliza kati ya huyu na huyu nampenda nani sio ??"

"Ndio baba "

"Sasa atakayekuwa wa kwanza kunikisi ndo huyo nampenda sana "

Kwa pamoja wale watoto walimkisi rajabu kila mtu alimkisi upande wake

"Mmeona sasa hii inamaanisha kuwa wote mmnampenda baba na baba anawapenda sana si ndio ??"

"Yeeeeeeh "

Wenyeee walifurahi pale na shyna akaaachukua kwaajili ya kwenda kuwaogesha

"Lily ila baba yetu ni mtu mwema sana"

"Nilikuambia tu kuwa rangi sio roho "

hawa watoto au watu wazima maana maneno yao eti rangi sio roho .

"Lily unamaanisha nini kusema hivyo ??"

Aliuliza shyna maana aliona wanamchanganya tu

"Baba yetuweusi lakini moyo wake mweupe anatupenda sana "

Hapo ata shyna aliangua kicheko cha hali ya juu....

Siku ziliendelea kwenda rajabu aliweza kuwateka watoto walitokea kumpenda sana, baada ya mambo ya familia kukaa vizuri na kila kitu watoto walipelekwa Shule ambapo walikua wakiingia asubuhi na kutoka saa 12 jioni, Nagma aliendelea na kazi zake uku Rajabu na shyna wakiwa bize na restaurant yao ambayo walifunguliwa na Nagma, restaurant ilianza kupata umaarufu wadada walikuwa hawakauki kwaajili ya rajabu nyie rajabu anavutia sana kumuangalia......

Siku hiyo wakiwa bize na kuwahudumia wateje shyna aliweza kumuona maimuna ambaye kwa wakati huo tumbo lake lilikuwa mbele kabisa kwamba ni kubwa, maimuna alikuwa amebeba kimfuki ikionesha wazi kuwa alikuwa ametoka matembezimi akiwa na dera lake lililochakaa kwa kupauka sana alikuwa akitembea kwa mwendo wa polepole kwaajili ya uchovu na jua kali....

Shyna baada ya kumuona maimuna kwajili ya mshangao alijikuta akiita

"Maimuna...."

Mai aligeuka alifurahi kumuona shyna kwa furaha na shauku akavuka barabara pasi na kuangalia uku na uku akajikuta akisukumwa na pikipiki ambayo ilikuwa kasi sana......🥹.

ITAENDELEA
 
KWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹

MTUNZI: PATRICIA ANTONY

SEHEMU YA: 16

Mawasiliano: 0783642467

Songa nayo.......

Rajabu alirudi nyumbani moja kwa moja akaenda chumbani na kumuita Nagma

"Kuna nini jamani me naandaa chakula kule ? Kwanza umeondoka asubuhi bila kuaga umenikera ujui tu "

"Naangalia vibarua uko siwezi kukaa tu nyumbani "

"Si nilishakuambia kuwa kazi nitakutafutia tena sio kukutafutia nakuunganishia moja kwa moja, Rajabu najua iki kipindi kichwa chako kijo less sana ndio maana nataka upumzike utulie na kuwa sawa "

"Niko sawa nilichokutana nacho Leo ni mawazo matupu "

"Unaona sasa ata taarifa zako sio nzuri ni stress muda wote, Rajabu subili nikuambie mimi ningekuwa mtu wa kupaniki kama wewe nakuambia sasa hivi ningekuwa chini tena wa jalalani, nina mengi sana kichwani mwangu najua adui zangu wote na wamenizunguka na naishi nao pasi na wao kujua kuwa mimi ndo yule ambaye walinikosea na bado nakosewa kila siku lakini sijaruhusu mambo yao yanipe presha na namna hiyo "

"Unaongea tu nimekutana a na maimuna anaishi kule kwa mama rukia "

"Kwahiyo kama anaishi kule ??"

"Kwanza ilikuwaje umefika kule ? Rajabu mume wangu we ni mbishi toleo oa mwisho kabisa kaah "

"Eeeh basi nawe mke wangu "

"Ebu niache mtu sina amani na mwanaume wangu kila tukikaa ni habari za mawazo "

Alizungumza nagma na kutoka nje

"Ila ni kweli namkosesha amani Nagma wangu lazima nimfanye mwenye furaha na amani....."

Kwakuwa rajabu alichoka sana alijilaza kwenye kochi lililopo pembeni ya kitanda chao na kulala

"Eeeh huyu jamani "

Alizungumza Nagma baada ya kumkuta rajabu akiwa amelala akamshtua kwa kumtikisa

"Amka amka amka we baba wewe ata kuoga kweli "

"Aaah me nilijua unaniamshia mambo ya maana labda chakula kimeiva unaanza kuniambia mambo ya kuoga mwili wenyewe wa udongo nikimomonyoka ??"

"Una wazimu kweli kaoge uko "

"Halafu we mbona kama "

"Kama nini malizia unataka kusema kuwa nakufanya kama mtoto sio ?? "

Rajabu hakujibu zaidia alimnyanyua Nagma ambaye na yeye alikubali kubebeka

"Kwani saaa hivi una kilo ngapi ?? maana nahisi uzito unanizidia "

"Tabia mbaya hiyo nibebe vizuri "

"We unataka kunivunja nini kwenye mwili wangu yaani hapa najikaza ili nikuangalie mke wangu kwa juu ulivyokuwa mzuri walahi uliumbwa mwezi wa 12 "

"Unaupenda sana msemo wako huo "

"Ni kwaajili yako tu "

Rajabu akiwa amembeba nagma aamkaingia nae bafuni wakaoga kwa pamoja na kutoka....

Majila ya usiku wakiwa chumbani walishangaa sana kusikia mlango wao ukigongwa mfululizo walishtuka na kuwai kwenda kuangalia kuna nini

"Nyie tena ??"

Alichoka Nagma baada ya kuwaona lily na Raya ndio walikuwa wakigonga

"Tunataka kulala na ninyi "

Nagma na Rajabu waliishia kuangaliana tu na hawakuwa na budi zaidi ya kuingia nao chumbani kwa usiku huo waliweza kutumia muda mwingi na mzuri na watoto wao

"Natamani mama ungekuwa hapa uone furaha za wajukuu zako, najua ungempenda Raya kama ambavyo ulimpenda maimuna"

Alizungumza rajabu kimoyomoyo mwisho watoto walipitiwa na usingizi na wakalala nao....

Asubuhi na mapema kama kawaida rajabu aliamka akaandaa kifungua kinywa na kufanya usafi wa nyumba

"Shikamoo kaka"

Alisalimia shyna baada ya kukutana na kaka yake sebuleni

"Marahaba hali yako ??"

"Salama naona leo umechangamka sana"

"Sana, kwanza nikuulize ilikuwaje ukawaacha watoto usiku wakaja chumbani kwetu "

"Sasa si walitaka wazazi wao me nifanye nini "

"Sa........"

Kabla rajabu hajamaliza maneno yake alikuja Raya

"Kulala na baba raha sana leo nitalala nae tena "

Rajabu alibaki akimuangalia shyna tu maana hakuwa na jibu zuri la kumpa Raya

"Baba kati ya mwanao mimi na Raya unampenda nani ??"

Muda huo huo Lili alifika na kuuliza swali, rajabu akachuchumaa na kuwanyanyua watoto wote

"Eeeeh Baba baunsa "

Alipiga kelele Raya

"Umeuliza kati ya huyu na huyu nampenda nani sio ??"

"Ndio baba "

"Sasa atakayekuwa wa kwanza kunikisi ndo huyo nampenda sana "

Kwa pamoja wale watoto walimkisi rajabu kila mtu alimkisi upande wake

"Mmeona sasa hii inamaanisha kuwa wote mmnampenda baba na baba anawapenda sana si ndio ??"

"Yeeeeeeh "

Wenyeee walifurahi pale na shyna akaaachukua kwaajili ya kwenda kuwaogesha

"Lily ila baba yetu ni mtu mwema sana"

"Nilikuambia tu kuwa rangi sio roho "

hawa watoto au watu wazima maana maneno yao eti rangi sio roho .

"Lily unamaanisha nini kusema hivyo ??"

Aliuliza shyna maana aliona wanamchanganya tu

"Baba yetuweusi lakini moyo wake mweupe anatupenda sana "

Hapo ata shyna aliangua kicheko cha hali ya juu....

Siku ziliendelea kwenda rajabu aliweza kuwateka watoto walitokea kumpenda sana, baada ya mambo ya familia kukaa vizuri na kila kitu watoto walipelekwa Shule ambapo walikua wakiingia asubuhi na kutoka saa 12 jioni, Nagma aliendelea na kazi zake uku Rajabu na shyna wakiwa bize na restaurant yao ambayo walifunguliwa na Nagma, restaurant ilianza kupata umaarufu wadada walikuwa hawakauki kwaajili ya rajabu nyie rajabu anavutia sana kumuangalia......

Siku hiyo wakiwa bize na kuwahudumia wateje shyna aliweza kumuona maimuna ambaye kwa wakati huo tumbo lake lilikuwa mbele kabisa kwamba ni kubwa, maimuna alikuwa amebeba kimfuki ikionesha wazi kuwa alikuwa ametoka matembezimi akiwa na dera lake lililochakaa kwa kupauka sana alikuwa akitembea kwa mwendo wa polepole kwaajili ya uchovu na jua kali....

Shyna baada ya kumuona maimuna kwajili ya mshangao alijikuta akiita

"Maimuna...."

Mai aligeuka alifurahi kumuona shyna kwa furaha na shauku akavuka barabara pasi na kuangalia uku na uku akajikuta akisukumwa na pikipiki ambayo ilikuwa kasi sana......🥹.

ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom