KWAAJILI YAKO MAIMUNA

MTUNZI: PATRICIA ANTONY
SEHEMU YA: 15
MAWASILIANO: 0783642467
SONGA NAYO...........
Rajabu na familia yake walifika nyumbani wakiwa na binti yao Mpya ambaye ni mtoto wa maimuna aliyekuwa akiitwa Raya
"Oooh my God lily uwiiiih nilikukumbuka sana "
Alipiga kelele za furaha Raya, shyna alibaki akimshangaa mtoto yule akamshika mkono kaka yake na kusogea nae pembeni
"We kaka mbona maimuna kajizaa ??"
Alivyouliza hivyo rajabu akaangua kicheko uku machozi yanamtoka
"Sikuelewi unalia unacheka "
"Ilo swali na mimi nilimuuliza Nagma tukiwa njiani uwezi amini wamefanana hadi sauti na anaongea mama chiriku

yaani hapo ni kasheshe....."
"Mmmmh eti nimeambiwa huyu wa nje ndio baba yangu ndo alikuwa ana umwa lakini mbona ye mweusi sana "
Alisikika mtoto wa maimuna


vya kurithi vinazidi
"Ata mimi mama kaniambia huyu ndo baba angu

ila analia Lia huyo muda mwingine anafoka "
"Eeeh achana na kufoka analia kama wale watoto wa kituoni kwetu au ??"
"Aaah sio hivyo yeye analia na sauti yakw kubwa halafu inakwangua kama hivi aaaaaaaaaaah

"
Nyie hawa watoto wamenishinda tabia yaani walikuwa wanapiga story utazani ni watu wazima kabisa muda huo Nagma, rajabu na shyna walisimama tu wakiwasikiliza wenyewe walikuwa bize hawana ata habari kuwa kuna watu wanawaangalia na kuwasikiliza
"Yaani umu ndani kunabowa mdada mzuri ambaye Alii hovyo ni antie shyna kwanza mpole halafu anaupendo mama, anaupendo lakini muda wote analia Lia kama mtoto halafu baba anamwambiaga mama kachanganyikiwa "
"Umeona sasa nagma ulikua unanivuluga mno leo hii tumekuwa kivutio cha stori kwa hawa watoto "
"Kwahiyo me ndo chanzo sio ??"
"Ndio kwani ujioni ??

ila watu wafupi mnashida sana "
Alitania rajabu na Nagma akaanza kumkimbiza wakakimbilia chumbani kwao
"Haya Waone kama watoto wadogo waje kuanguka "
Alizungumza Raya na wote wakacheka
"Mtoto mzuri mambo ??"
"Naitwa Raya sio mtoto mzuri "
"We Raya huyu ndo antie shyna usimjibu hivyo ni antie yangu mzuri "
" ni antie yako me anihusu chumbani kwako wapi nikapaone maana tangu nimefika sijui natakiwa kwenda wapi "
"Usijali Raya nitakupeleka antie yako niko hapa haya twende watoto wazuri "
"Huyu shangazi yako ata sijampenda "
"Ni antie sio shangazi We mbona hivyo ?? Halafu umeanza kuwa na bad manners kwa wakubwa si ndio ??"
"Niache bhana "
Kivumbi iki walahi yaani ni kama maimuna karudi upga kwa kasi ya 4g kulaleki mtoto anaongea kama kalishwa usembe...
Asubuhi na mapema kama kawaida Rajabu alikua wa kwanza kuamka maana usingizi wake ni wa kuotea otea tu kutokana na kua na mawazo mengi sana yasiyoelezeka hivyo uwa anawai kuamka na kufanya shughuli zote za nyumbani na kuandaa kifungua kinywa....
"Kaboss bhana

ila madamu wangu anajua kuwalea bhana kasoro weee kidogo nakuona unajituma ata kukata maua "
Walahi muacheni Rajabu awe na stress

tu anadharauliwa hadi na mlinzi wa getini
"Masai hizi kazi nafanya ili kukupunguzia wewe upate muda wa kupumzika lakini pia kama una muda wa kukaa na kufatilia maisha yangu nafikili hii kazi ungeendelea nayo mwenyewe "
Alichukia rajabu akaweka vifaa chini na kuanza kuondoka
"Aka nako kangekuwa kabosi ningekoma mimi kautani kadogo tu kachukia kama sio mwanaume "
Rajabu aliingia chumbani akavaa na kuondoka alizunguka uku na uku kutafuta ajila lakini ilikuwa shida sana kupata akapakumbuka nyumbani kwao akaona sio mbaya kama ataenda kumuona mama rukia
"Eeeh jamani Rajabu mwanangu eeeh nilikukumbuka sana sema tu ndo hivyo simu yangu imeingia kwenye maji "
"Ata mimi nilikukumbuka ndio maana nimekuja shyna pia anakusalimia sana "
Wakiwa bize na story za hapa na hala rajabu alishtuka kusikia sauti ya maimuna kutokea upande wa pili ambao ni upande wa jiko
"Mama umesema hawa danga nichanganye na tembele au ?? "
"Ndio pika haraka mgeni ale "
Subili hiyo ni sauti ya maimuna au ni mimi nachanganyikiwa ??
"Ni yeye mwanangu ndo nilikuwa nataka kukupa taarifa sema sasa hivi anebadilika na anajitambua sana sana, kila siku anawakumbuka kama juzi jana asubuhi ameenda makaburini kwa mama yako kusafisha "
"

nacheka kama mazuri mama rukia umempokea huyu mtu ??


nikupe hongera yako na pole maana hapo anavuta sumu yake ikijaa shingoni lazima akutemee kweheri mama nashukuru kuwa nimekukuta uko salama "
"Jamani rajabu ndo unaondoka "
"Huyu mtoto wako Mpya namuogopa kama ukoma apa tupu kuna kopi yake kule inanienyesha nikikutana na yeye rajabu mimi nakuwa kuchaa "
Alizungumza rajabu na kuondoka kwa mwendo wa haraka mama rukia alibaki akishangaa tu pasi na kuelewa ata neno moja kutoka kwa rajabu....
"Nimesikia unaitilia jina la rajabu "
Aliuliza maimuna baada ya kutoa jikoni mbio mbio
"Umbea tu kapike uko "
"Jamani mama "
Rajabu alirudi nyumbani akiwa kama kachanganyikiwa vile.....
ItanipitaKWAAJILI YAKO MAIMUNA 🥹
MTUNZI: PATRICIA ANTONY
SEHEMU YA: 16
Mawasiliano: 0783642467
Songa nayo.......
Rajabu alirudi nyumbani moja kwa moja akaenda chumbani na kumuita Nagma
"Kuna nini jamani me naandaa chakula kule ? Kwanza umeondoka asubuhi bila kuaga umenikera ujui tu "
"Naangalia vibarua uko siwezi kukaa tu nyumbani "
"Si nilishakuambia kuwa kazi nitakutafutia tena sio kukutafutia nakuunganishia moja kwa moja, Rajabu najua iki kipindi kichwa chako kijo less sana ndio maana nataka upumzike utulie na kuwa sawa "
"Niko sawa nilichokutana nacho Leo ni mawazo matupu "
"Unaona sasa ata taarifa zako sio nzuri ni stress muda wote, Rajabu subili nikuambie mimi ningekuwa mtu wa kupaniki kama wewe nakuambia sasa hivi ningekuwa chini tena wa jalalani, nina mengi sana kichwani mwangu najua adui zangu wote na wamenizunguka na naishi nao pasi na wao kujua kuwa mimi ndo yule ambaye walinikosea na bado nakosewa kila siku lakini sijaruhusu mambo yao yanipe presha na namna hiyo "
"Unaongea tu nimekutana a na maimuna anaishi kule kwa mama rukia "
"Kwahiyo kama anaishi kule ??"
"Kwanza ilikuwaje umefika kule ? Rajabu mume wangu we ni mbishi toleo oa mwisho kabisa kaah "
"Eeeh basi nawe mke wangu "
"Ebu niache mtu sina amani na mwanaume wangu kila tukikaa ni habari za mawazo "
Alizungumza nagma na kutoka nje
"Ila ni kweli namkosesha amani Nagma wangu lazima nimfanye mwenye furaha na amani....."
Kwakuwa rajabu alichoka sana alijilaza kwenye kochi lililopo pembeni ya kitanda chao na kulala
"Eeeh huyu jamani "
Alizungumza Nagma baada ya kumkuta rajabu akiwa amelala akamshtua kwa kumtikisa
"Amka amka amka we baba wewe ata kuoga kweli "
"Aaah me nilijua unaniamshia mambo ya maana labda chakula kimeiva unaanza kuniambia mambo ya kuoga mwili wenyewe wa udongo nikimomonyoka ??"
"Una wazimu kweli kaoge uko "
"Halafu we mbona kama "
"Kama nini malizia unataka kusema kuwa nakufanya kama mtoto sio ?? "
Rajabu hakujibu zaidia alimnyanyua Nagma ambaye na yeye alikubali kubebeka
"Kwani saaa hivi una kilo ngapi ??

maana nahisi uzito unanizidia "
"Tabia mbaya hiyo nibebe vizuri "
"We unataka kunivunja nini kwenye mwili wangu yaani hapa najikaza ili nikuangalie mke wangu kwa juu ulivyokuwa mzuri

walahi uliumbwa mwezi wa 12 "
"Unaupenda sana msemo wako huo "
"Ni kwaajili yako tu "
Rajabu akiwa amembeba nagma aamkaingia nae bafuni wakaoga kwa pamoja na kutoka....
Majila ya usiku wakiwa chumbani walishangaa sana kusikia mlango wao ukigongwa mfululizo walishtuka na kuwai kwenda kuangalia kuna nini
"Nyie tena ??"
Alichoka Nagma baada ya kuwaona lily na Raya ndio walikuwa wakigonga
"Tunataka kulala na ninyi "
Nagma na Rajabu waliishia kuangaliana tu na hawakuwa na budi zaidi ya kuingia nao chumbani kwa usiku huo waliweza kutumia muda mwingi na mzuri na watoto wao
"Natamani mama ungekuwa hapa uone furaha za wajukuu zako, najua ungempenda Raya kama ambavyo ulimpenda maimuna"
Alizungumza rajabu kimoyomoyo mwisho watoto walipitiwa na usingizi na wakalala nao....
Asubuhi na mapema kama kawaida rajabu aliamka akaandaa kifungua kinywa na kufanya usafi wa nyumba
"Shikamoo kaka"
Alisalimia shyna baada ya kukutana na kaka yake sebuleni
"Marahaba hali yako ??"
"Salama naona leo umechangamka sana"
"Sana, kwanza nikuulize ilikuwaje ukawaacha watoto usiku wakaja chumbani kwetu "
"Sasa si walitaka wazazi wao me nifanye nini "
"Sa........"
Kabla rajabu hajamaliza maneno yake alikuja Raya
"Kulala na baba raha sana leo nitalala nae tena "
Rajabu alibaki akimuangalia shyna tu

maana hakuwa na jibu zuri la kumpa Raya
"Baba kati ya mwanao mimi na Raya unampenda nani ??"
Muda huo huo Lili alifika na kuuliza swali, rajabu akachuchumaa na kuwanyanyua watoto wote
"Eeeeh Baba baunsa "
Alipiga kelele Raya
"Umeuliza kati ya huyu na huyu nampenda nani sio ??"
"Ndio baba "
"Sasa atakayekuwa wa kwanza kunikisi ndo huyo nampenda sana "
Kwa pamoja wale watoto walimkisi rajabu kila mtu alimkisi upande wake
"Mmeona sasa hii inamaanisha kuwa wote mmnampenda baba na baba anawapenda sana si ndio ??"
"Yeeeeeeh "
Wenyeee walifurahi pale na shyna akaaachukua kwaajili ya kwenda kuwaogesha
"Lily ila baba yetu ni mtu mwema sana"
"Nilikuambia tu kuwa rangi sio roho "



hawa watoto au watu wazima maana maneno yao eti rangi sio roho .
"Lily unamaanisha nini kusema hivyo ??"
Aliuliza shyna maana aliona wanamchanganya tu
"Baba yetuweusi lakini moyo wake mweupe anatupenda sana "
Hapo ata shyna aliangua kicheko cha hali ya juu....
Siku ziliendelea kwenda rajabu aliweza kuwateka watoto walitokea kumpenda sana, baada ya mambo ya familia kukaa vizuri na kila kitu watoto walipelekwa Shule ambapo walikua wakiingia asubuhi na kutoka saa 12 jioni, Nagma aliendelea na kazi zake uku Rajabu na shyna wakiwa bize na restaurant yao ambayo walifunguliwa na Nagma, restaurant ilianza kupata umaarufu wadada walikuwa hawakauki kwaajili ya rajabu nyie rajabu anavutia sana kumuangalia......
Siku hiyo wakiwa bize na kuwahudumia wateje shyna aliweza kumuona maimuna ambaye kwa wakati huo tumbo lake lilikuwa mbele kabisa kwamba ni kubwa, maimuna alikuwa amebeba kimfuki ikionesha wazi kuwa alikuwa ametoka matembezimi akiwa na dera lake lililochakaa kwa kupauka sana alikuwa akitembea kwa mwendo wa polepole kwaajili ya uchovu na jua kali....
Shyna baada ya kumuona maimuna kwajili ya mshangao alijikuta akiita
"Maimuna...."
Mai aligeuka alifurahi kumuona shyna kwa furaha na shauku akavuka barabara pasi na kuangalia uku na uku akajikuta akisukumwa na pikipiki ambayo ilikuwa kasi sana......

🥹.
ITAENDELEA