agwedegwede
Member
- Jan 12, 2011
- 42
- 24
Ndugu wana jamii wenzangu, jana wakati Chadema wanatoka Bungeni kupinga mabadiliko ya kanuni kuhusu tafsiri ya neno KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI wabunge wengine waliwazomea, kwa mimi nilisikia mwishoni wakati wabunge wanatoka Sauti ya Spika wa Bunge nae alizomea au kutoa neno la kejeli kwa Chadema, sikumbuki vizuri hapo, ila ilinishtua kusikia sauti ya Spika nae kwenye mkumbo wa kuzomea.
Mnalionaje hili wana Jamii wenzangu, naomba tulijadili na kama kuna mmoja wetu ana hiyo Clip naomba aiweke ili tuisikilize kwa makini, ila mimi nilisikia kuna sauti ya Spika pia akitoa kejeli kwa wabunge wa CHADEMA.
Naomba kutoa Hoja.
Mnalionaje hili wana Jamii wenzangu, naomba tulijadili na kama kuna mmoja wetu ana hiyo Clip naomba aiweke ili tuisikilize kwa makini, ila mimi nilisikia kuna sauti ya Spika pia akitoa kejeli kwa wabunge wa CHADEMA.
Naomba kutoa Hoja.