Kuweni makini, utapeli mpya umeibuka Dar

Hamuyu

Senior Member
Joined
Mar 29, 2010
Posts
118
Reaction score
21
Nilikua njiani naelekea ofisini kwangu, nikiwa mitaa ya Darajani Zanzibar simu yangu iliita aliyenipigia alijitambulisha na nilikua simjui, alisema yupo Mkoani Kigoma anafanya kazi shirika moja la kimataifa, alinieleza anahitaji mtu wa kushirikiana naye katika mambo ya kibiashara anayetoka Zanzibar, alidai alipatiwa namba yangu na moja kati ya rafiki zangu wanao ishi Uk, na hakutaka nimuulize niliendelea kumsikiliza.

Akaanza kunielekeza anafanya Biashara ya kununua Product ambayo inahifadhi vyakula visiharibike na akanipatia namba ya mtu anayehusika katika utengenezaji wa production na jina lake akadai anaitwa Ibrahim na anapatikana Mahonda Zanzibar, akaniambianimpigie Ibra kumuuliza kama hiyo Production ipo na inapatikana kwa bei gani, nilimpata Ibrahim na akanieleza wanazo bidhaa kutoka ncho tofauti lakini best zinatoka Sweeden na bei yake kwa chupa 2 ni T shs 1,200,000/= nikamjibu yule jamaa aliyenitambulisha kwa Ibra kwamba bei yake ndio hiyo, baada ya hapo akaniambia kwamba pia wapo mabosi wake wa kizungu wamefikia Zamani Kenpisky Hotel Pwani Mchangani wananunua hiyo bidhaa kwa bei ya juu sana mara 2 ya bei ya kununulia, wakati nawasiliana na hawa jamaa tokea dakika ya kwanza niligundua kwamba hawa ni matapeli na nilichukua hatua za kuripoti tukio hili kituo cha Polisi na walifika kwa wakati nikawa nawashirikisha katika mawasiliano na hawa matapeli.

Polisi niliwapatia namba za simu za hawa jamaa wakaweza kuzifanyia utafiti na wakagungua wenye kuzimiliki, na sasa baada ya muda mfupi nilipokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwamba anaitwa Fred yupo Kenpsky na ameelekezwa kwangu kuja kununua Product mimi sikujivunga nikamwambia zitapatikana ndio hapo akaniambia kabla sijapeleka mzigo nimpelekee sample 1 pair ili akiridhika nao ndio tunaondoka pamoja na kwenda kuchukua mzigo wote.

Nikamweleza yule jamaa aliyenipigia simu mwanzoni kwamba wanunuzi wanahitaji sample wakiridhika ndio wanunue mzigo wote, hivyo akaniambia niwasiliane na Ibra kuhusu sample nikampigia akaniambia beio yake ndio hiyo aliyoniambia hapo juu Milioni moja na laki mbili, nikamjulisha jamaa akaniambia nifanye maarifa nipeleke hizo pesa.

Nikawaeleza Polisi tukaweka mtego baada ya muda kidogo nikawaambia kwamba fedha tayari waniletee mzigo, wakanielekeza walipo wakaniambia wapo Kibweni tukaenda mimi nilitangulia na polisi wakiwa nyumba yangu kwa umbali kidogo, nikapiga simu akaja kijana mmoja akaniuliza ni wewe niliyeagizwa kuhusu mzigo nikamwambia ni mimi na mzigo uko wapi nikupatioe hizo fedha? akaniambia nimsubiri kidogo akaufuate niliendelea kusubiri pale na kupiga simu hakutokea baadae alizima simu kabisa.

Nikawaarifu polisi kwamba jamaa wameshtuka nikarudi ofisini kwangu. nilichoamua kufanya baada ya hapo niliwapigia simu wale jamaa wote tuliokuwa tunawasiliana kwamba nawashukuru sana mzigo nimeupata na tumeshafanya biashara nimemkabidhi jamaa Milioni moja na Laki mbili ispokuwa jamaa aliyepokea pesa alitaka wale jamaa wote wasijue kama tayari ameshapokea fedha.

na nikawashukuru sana sikujua kilichoendelea baada ya hapo, hii ni tahadhari natoa kwa wenzangu wa JF na watanzania tuwe makini na tujiepushe na tamaa za kijinga tutaingizwa mjini.

nawasilisha.
 
Mjini shule ami, pole sana. Namshukuru Mungu hukuingia kwenye mtego wao....
 
Mjini shule ami, pole sana. Namshukuru Mungu hukuingia kwenye mtego wao....

Mkuu nilipofika ofisini niliwashirikisha wenzangu tukawa tunashauriana cha kufanya, haya mambo nikuepuka tamaa zisizo na msingi hakuna short cut ya kihivyo kwenye maisha tunahitaji kupambana Ahsante
 
ami pole sana hizo dili wameandika wengi kweli humu zingine wameumizwa ndio wakaja wengine ka wewew wamewah..pole ami
 
ami pole sana hizo dili wameandika wengi kweli humu zingine wameumizwa ndio wakaja wengine ka wewew wamewah..pole ami

Ok, niliona kwenye moja ya magazeti ya udaku kuna Miss Tz mmoja na yeye yalimkuta tena niliposona walitumia nyia za mana hii hii, Ahsante tuwe makini kwa pamoja
 
Wengi wamelizwa na huuutapeli, lakini mimi nadhani ni wajinga kwa sababu mtiririko wooote wa hao matapeli unaacha maswali mengi kwa mtu anayejiuliza mara mbili mbili.

Kuna jamaa mmoja walimwingiza mjini kikwelikweli.... Unajua walifanyaje?

Walipoleta ile sampo akaichukua kwa shilingi milioni moja.... halafu kule alokoagiziwa apeleke akakuta ni 'wateja wa ukweli'.... na wakamlipa fedha nzuri tu..... mara mbili ya ile aliyotoa, na wakamwambia wanataka mzigo zaidi. Si jamaa alikimbia mbio mbio dukani kwake akamwambia kijana wake kusanya mauzo yooote unipe kwani nimepata dili la nguvu...
akapitia benki akakomba ka-akiba alikokuwa nako kooote, akaona haitoshi akaenda kwenye duka la rafiki yake akakopa fedha... akaenda kuchukua 'mzigo' wake. Sasa kazi ilikuwa 'kuuza' kwani jamaa wale wanunuzi waliyeyuka wooote.

Sisi tukamwambia yale 'madawa' si madawa kweli, lakini hakuamini alikaa na yale mafurushi kwa mda mrefu .... sijajua kama aliyatupa lini, ila jamaa alikonda sana, japo sasa amejitahidi hali yake kifedha imeanza kuwa nzuri....
 
Tuache tamaa ya kutaka utajiri wa haraka haraka ndipo tutapona kwenye utapeli huu. Kwenye mazingira ya kawaida mtu usiyemfahamu hawezi akakuunganisha na dili zenye faida kwani yeye hana ndugu zake! Hongera sana umepona kuibiwa.
 
Haya yote yanatokana na kuwa na tamaa ya utajiri wa haraka!
 
Hii taadhari ilitolewa humu mara nyiiiiiiiiiingi mpaka! Wewe hukuwepo naona pole sana
 
Pole sana hata mimi last year ili nitokea, lakini nilikua nimeshasoma malalamiko kama haya humuhumu nadhani so walivonieleza baada ya hapo sikupokea cm ya huyo mtu. Pole sana.
 
Wadau kuna utapeli mpya ambao unafanana na blackmailing kwa wafanyakazi wa Serikali, wafanyabiashara na watu wengine.

Matapeli wanawapigia simu za kuwatisha wafanyakazi wa Serikali kwamba wao ni maofisa usalama wa taifa na wameona mafaili yao ni machafu hivyo wanashawishi wawasaidie ili wayasafishe kwa kuwahonga.

Wafanyabiashara wanatishwa kwamba wanakwepa kulipa kodi na wakigundua una fedha wanaweza kukuteka.
 
Utapeli huu umeshika kasi sana siku hizi.
Ugumu wa maisha unapoongezea huenda sambamba na kuongezeka kwa uhalifu
 
Hii nzuri sana.
Sasa kama wewe ni mfanyakazi wa serikali mtu akakupigia simu akakwambia ana faili lako chafu na wewe ni msafi unaogopa nini?

kama wewe ni mfanyabiashara mtu anakupigia simu anakwambia unakwepa kodi wakati wewe ni msafi unaogopa nini?

Mimi naona hao matapeli waaendelee kuwepo tu.
 
kama we ni msafi sioni watakutapeli vip... uwe mfanyakazi au mfanyabiashara kama ni muadilifu huna haja ya kuwaogopa hao watu
 
mbona wakizamani ivyo auna update kdogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…