Mr mutuu
JF-Expert Member
- Jan 27, 2023
- 2,027
- 10,040
Jana nipo mtaani jioni wakapita madogo wawili wanasajili line, hawa sio wageni sana machoni huwa nawaona mara moja moja, basi nikawaita nikawa nasajili namba ya halotel. Sijawahi kuwa na line ya halotel hapo kabla.
Katika kusajili sarakasi zikawa nyingi mara mtandao unasumbua, mara ngoja nijaribu kutumia mashine ya mwenzangu, ikachukua muda kidogo. Kwasababu nilikua nimekaa mahali napata kinywaji nikawunulia soda pale wakiwa wanasubiri mtandao ukae sawa ikachukua let's say dakika 40 zoezi kukamilika wakinipa line yangu ya halotel.
Sasa leo nimeamka sijui nikachezwa na machale gani, nikawa naona kama hawa madogo kuna ujanja wamenifanyia, nikaingia menu ya *106# nicheki usajili namba za halotel zilizosajiliwa na nida yangu, aisee, nakuta nina namba za halotel 4!
Nikawa kama siamini, kumbuka jana ndio mara ya kwanza nasajili line ya halotel maishani mwangu! Nikaziandika hizi namba tatu ambazo sipo nazo pembeni nikazipiga zote hazipatikani.
Nikashikwa na hasira kweli, nikawa najiuliza hivi mtu akifanya uhalifu mkubwa kwa kutumia identity yangu si naweza kwenda jela bure au waanze ujinga wa ile hela tuma kwenye namba hii si ntaonekana nimeanza utapeli mjini.
Basi leo mchana kuna shughuli namalizia nimeamua kula sahani moja na huyu dogo, kwanza naanzia polisi naenda kuchukua rb, naenda halotel lazima watakuwa wanamjua aliyenisajilia hizi line naamsha noma huko mpaka kieleweke. Nataka niende makao makuu kabisa na waniambie ni hatua gani wanamchukulia huyu tapeli+ nizifutie usajili hizi line.
Nimeshafanya upelelezi wa mtaa nimeambiwa sehemu wanapokutana asubuhi kufanya morning briefing kabla hawajaanza kazi, kesho naenda kumwinda hapo ikiwezekana nimalizane nae 'kimtaa mtaa'.
Rai yangu, kuweni makini na hawa wasajili line ikiwezekana tuwe tunahakiki usajili wetu mara kwa mara, usajili wa line unabeba identity yetu ipo siku mtu anatumia identity yako akafanya tukio kubwa ukaja kuozea jela bure.
Katika kusajili sarakasi zikawa nyingi mara mtandao unasumbua, mara ngoja nijaribu kutumia mashine ya mwenzangu, ikachukua muda kidogo. Kwasababu nilikua nimekaa mahali napata kinywaji nikawunulia soda pale wakiwa wanasubiri mtandao ukae sawa ikachukua let's say dakika 40 zoezi kukamilika wakinipa line yangu ya halotel.
Sasa leo nimeamka sijui nikachezwa na machale gani, nikawa naona kama hawa madogo kuna ujanja wamenifanyia, nikaingia menu ya *106# nicheki usajili namba za halotel zilizosajiliwa na nida yangu, aisee, nakuta nina namba za halotel 4!
Nikawa kama siamini, kumbuka jana ndio mara ya kwanza nasajili line ya halotel maishani mwangu! Nikaziandika hizi namba tatu ambazo sipo nazo pembeni nikazipiga zote hazipatikani.
Nikashikwa na hasira kweli, nikawa najiuliza hivi mtu akifanya uhalifu mkubwa kwa kutumia identity yangu si naweza kwenda jela bure au waanze ujinga wa ile hela tuma kwenye namba hii si ntaonekana nimeanza utapeli mjini.
Basi leo mchana kuna shughuli namalizia nimeamua kula sahani moja na huyu dogo, kwanza naanzia polisi naenda kuchukua rb, naenda halotel lazima watakuwa wanamjua aliyenisajilia hizi line naamsha noma huko mpaka kieleweke. Nataka niende makao makuu kabisa na waniambie ni hatua gani wanamchukulia huyu tapeli+ nizifutie usajili hizi line.
Nimeshafanya upelelezi wa mtaa nimeambiwa sehemu wanapokutana asubuhi kufanya morning briefing kabla hawajaanza kazi, kesho naenda kumwinda hapo ikiwezekana nimalizane nae 'kimtaa mtaa'.
Rai yangu, kuweni makini na hawa wasajili line ikiwezekana tuwe tunahakiki usajili wetu mara kwa mara, usajili wa line unabeba identity yetu ipo siku mtu anatumia identity yako akafanya tukio kubwa ukaja kuozea jela bure.