Kuweni Makini na SD Card Fake

Kuweni Makini na SD Card Fake

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,179
Kuna wimbi kubwa la bidhaa fake hasa vifaa vya simu.

Unaweza kununua simu yako nzuri tena kwa gharama kubwa lakini ukaishia kupata kero katika matumizi sababu tu ya SD card fake.

SD card fake husababisha simu kuwa slow, kustuck marakwamara, kufuta apps na data, kuharibu system apps, na mara nyingine utaona ujumbe 'sd card removed unexpectedly'

Suala hili limeshagharimu na kusumbua watu wengi. Nami ni mmojawapo.

Tuwe makini katika kununua sd card. Na namna bora ya kupata original SDs ni kununua kwa mawakala waliothibitishwa.

Lets share this alerting msg..
 
Kuna wimbi la bidhaa fake hasa vifaa vya simu. Unaweza kununua simu yk nzuri tena kwa gharama kubwa lakini ukaishia kuidispose simply because of these fake SD Card. Mara nyingi wauzaji wa simu hutoa SD original na kuweka fake.

Na mara nyingi wauzaji wa SD card huuza fake. Unaponunua simu kama ni Samsung basi SD card lazima iwe na maandishi Samsung.
SD card fake husababisha simu kuwa slow, ku stuck, apps kurestart mara kwa mara, na msg za 'sd card removed unexpectedly'.

Suala hili limeshagharimu na kusumbua watu wengi. Mimi mmojawapo.

Lets share this alerting msg
Asante sana kwa kutupa hii elimu,mimi nimewahi kununua simu kwa bei mbaya,lakini nilishangaa kuwa na matatizo kama hayo.Kila mara huwa naenda kwa fundi,huwa akinambia toa memory card,bila kunifahamisha kama tatizo ni hilo la memory card fake.Ukitoa memory card,simu inafanyakazi kama kawaida,hata kama ilikuwa yakataa kuwaka.
 
Watu wengi wanahangaika kwa mafundi bila kujua tatizo
 
mkuu ahsante kwa kutuelimisha sasa tutakuwa makini
 
Kuuuumbee...., nishapata maana! ahsante sana mkuu.
 
Do not accept the box if broken. .... HUJAWAHI KUSOMA HAYO MAANDISHI??? Pale pa kufungulia box la simu

Mi nijuavyo ukienda kununua simu kwenye maduka yenye simu orginal nyingi KULIKO michina fake hawawezi kukufanyia uhuni huu..

WARNING: BEFORE HUJANUNUA BIDHAA ZA ELECTRONIC INGIA INTERNET ULIZIA WHAT'S IN THE BOX... Mfano mzuri ingia YouTube

Eg... what's in the box for Samsung galaxy s3??

Itakupa kila kitu. Ukienda dukani huibiwi..
 
daaaaah kweli mi huwa inaniambia "SD card damaged, you are required to format it"
 
Ndio hivyo.
...Itakusumbua mpaka ubadilishe hy memory card
 
dah nasikitika sana kwa hilo lakin mm pia ni mfanyabiashara wa hizo bidhaa lakin naomba niongee ukweli ninazo orginal na guarantee natoa na bei zangu nafuu sanaa km 2gb 6000/: 4GB TSHS 8000/: 8GB 10000/: kwa mawasiliano 0712552294
 
Huwezi kusibitisha kuwa wauzaji wanatoa memory na kuweka feki ilihali kama wewe si muuzaji, suala la vitu vingi hapa Tz kuwa feki ni la wateja wenyewe ambao wanapenda vitu vya rahisi au ikiwezekana kiwe cha wizi yeye ndo kinamfaa zaidi. Wakianza wateja wenyewe kubadilika kila kitu kitabadilika sasa hivi ni nadra sana kukuta memory org hapa Tz, pengine niseme zile zinazokuja na simu za Tecno zina viwango.
 
Huwezi kusibitisha kuwa wauzaji wanatoa memory na kuweka feki ilihali kama wewe si muuzaji, suala la vitu vingi hapa Tz kuwa feki ni la wateja wenyewe ambao wanapenda vitu vya rahisi au ikiwezekana kiwe cha wizi yeye ndo kinamfaa zaidi. Wakianza wateja wenyewe kubadilika kila kitu kitabadilika sasa hivi ni nadra sana kukuta memory org hapa Tz, pengine niseme zile zinazokuja na simu za Tecno zina viwango.

Sure, ila mimi yangu niliwekewa fake na muuzaji mkubwa tu wa simu.

Wale wafanyakazi wao huwa wanabadilisha bila matajiri kujua
 
Back
Top Bottom