Mangisandy
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 2,652
- 2,272
Chonde chonde kamati kuu ya CHADEMA, huu mtego utegueni kwa hekima.
Kuwafukuza wanawake 19, au 20, ambao Ndio Wanawake imara na wenye nguvu zaidi nchini kwa sasa, siyo tu kujipiga risasi mguuni, ni kumpa adui nafasi ya kujilinda na kukushambulia.
Sisiemu wana pandikiza mapandikizi kila leo, wale kina ‘Mamvi’, mzee ‘gusa unuke’, nk! Kwanini tusiwachezee mchezo wao huo huo? Unapata wapi fursa nyingine kama hii? Naomba suala la wamama tulimalize, alafu watu kadhaa vichwa kama Mnyika, na Catherine Ruge waunge juhudi mkono, waende jikoni mle, wakatulee mbinu. Kwa nini tutegemee njia moja tu? Huyu adui tunatumia njia hiyo tangu 1995, na tunapigwa? Ok, Lisu na Lema wamekimbilia uhamishoni, ni mbinu lakini isiwe ya mwisho.
Wacha watutukane, watubeze na kutudharau, lakini mwishoni tuwatoe madarakani! Lengo lao chama kisambaratike na kufa, lakini sisi tuamue kusambaratika na kuishi!
Kesho tokeni na agenda ya kukivunja vunja chama, Kama kawaida Mwamba Mbowe abebeshwe lawama ya kawaida ya kupenda ruzuku, kuwa ameteua 19 peke yake, alafu wajumbe wengine wakuu wajivue uanachama, waunge juhudi waingie Serikalini, ‘kimafia’ tufe ili kuishi, sambaratisha chama kiingie kila uwanja wa vita.
Kila tutakapo ingia tueneze u-CHADEMA wetu, kama Wakristo wanavyoeneza Ukristo wao China, chini kwa chini, tusitake mafanikio ya mda mfupi tu, tujipangeni ‘kimafia’ kwa ajili ya mafanikio ya muda mrefu.
Ni maoni yangu lakini nitaendelea kuunga mkono upinzani kwa hali na mali, hata kama ushauri wangu hautafuatwa.
Kuwafukuza wanawake 19, au 20, ambao Ndio Wanawake imara na wenye nguvu zaidi nchini kwa sasa, siyo tu kujipiga risasi mguuni, ni kumpa adui nafasi ya kujilinda na kukushambulia.
Sisiemu wana pandikiza mapandikizi kila leo, wale kina ‘Mamvi’, mzee ‘gusa unuke’, nk! Kwanini tusiwachezee mchezo wao huo huo? Unapata wapi fursa nyingine kama hii? Naomba suala la wamama tulimalize, alafu watu kadhaa vichwa kama Mnyika, na Catherine Ruge waunge juhudi mkono, waende jikoni mle, wakatulee mbinu. Kwa nini tutegemee njia moja tu? Huyu adui tunatumia njia hiyo tangu 1995, na tunapigwa? Ok, Lisu na Lema wamekimbilia uhamishoni, ni mbinu lakini isiwe ya mwisho.
Wacha watutukane, watubeze na kutudharau, lakini mwishoni tuwatoe madarakani! Lengo lao chama kisambaratike na kufa, lakini sisi tuamue kusambaratika na kuishi!
Kesho tokeni na agenda ya kukivunja vunja chama, Kama kawaida Mwamba Mbowe abebeshwe lawama ya kawaida ya kupenda ruzuku, kuwa ameteua 19 peke yake, alafu wajumbe wengine wakuu wajivue uanachama, waunge juhudi waingie Serikalini, ‘kimafia’ tufe ili kuishi, sambaratisha chama kiingie kila uwanja wa vita.
Kila tutakapo ingia tueneze u-CHADEMA wetu, kama Wakristo wanavyoeneza Ukristo wao China, chini kwa chini, tusitake mafanikio ya mda mfupi tu, tujipangeni ‘kimafia’ kwa ajili ya mafanikio ya muda mrefu.
Ni maoni yangu lakini nitaendelea kuunga mkono upinzani kwa hali na mali, hata kama ushauri wangu hautafuatwa.