Kuwa ugenini mateso

Hahaha kuna rafiki yangu alifikia kwa nyumban kwa rafik yake,mama wa yule rafiki yake alikuwa anawatumatuma sana kaz kuna kipindi mwanae akawa anagoma si wajua nyumban shida kwa yule mgen inabid ufanye 2 hata kama una haki ya kukataa jamaa alinyokaa.
 
Safari hii yamenikuta, inabidi nihamie kwa watu, sijui kama nitayaweza.
 
hapa ninachojifunza ni kwamba much as wengi wetu tumepitia kwa ndugu katika njia ya kuelekea hapa tulipo, ipo changamoto kwamba kwa vile 'tuliteseka' tukiwa huko (nashukuru Mungu sijawahi pitia huko), tusingependa watoto wetu wapitie maisha hayo. Wakati huo huo tunakubali kuwa changamoto hizo za kukaa kwa ndugu 'zimetupa akili' ya maisha, kujifunza kujitegemea nk. Swali ni je, inawezekana watoto wetu wakashindwa kupambana na maisha kwa kutopitia aina ya maisha tuliyopita?
 

Mh. Kaizer unachokiuliza nami nimeshajiuliza sana, mimi nimelelewa kwa mjomba baada ya Baba kutangulia kwenye HAKI.
Na kwa vile tulizaliwa 7 hivyo nduguze Mama na ndugu wa Baba (the late) wakatugawana sisi watoto kumwondolea Mama task work ya maisha, huko kwa Uncle ndipo nilipoyajua haya mnayoyasema, aidha Uncle hakua na tatizo, Mkewe ndiye alikua mwiba wa Nungunungu! Pamoja na yote maisha ya hivyo yana advantage na disadv kwani kwa upande mmoja utapata faida ya kujua Njaa inavumiliwaje utajua Branget linafuliwaje, vyombo vinaoshwaje, deki inapigwaje, utajua kupika n.k.
Watoto wanaokulia kwa wazazi wao wa kibayolojia wenye umri sawa na wanaokulia kwa ndugu walezi hawawezi kua sawa katika kumudu mazingira yanayowazunguka, wale walioko kwa walezi wanakua more active kuliko wanaokulia kwa wazazi halisi.
 

Aisee kwanza pole sana kwa ulikopitia

hapo bold ndo exactly my point, kama hiyo hypothesis ni true, then watoto wanaokuliwa kwa biological parents watakuwa disadvantaged kupambana na maisha ukilinganisha na wenzao, na hivyo kuna uwezekano in 'the strugle for existence' wakatupiliwa mbali!:shock:
 
Duh, kwa kweli kukulia kwa ndugu kama ni hivi inatisha

lakini nikisema inategemea na cultureya mhusika ntakuwa nimekosea?
Kuna sehemu zingine nimeona chakula kinapewa kipaumbele mno kiasi kwamba mtu akikupa chakula ni kama kakupa roho yake?
Na pia kuna sehemu zingine hata mpita njia kula ni lazima, usipokula unaonekana una madharau, sembuse mtu anayefugwa kwenye nyumba hiyo?
 

jibu la swali lako ni hapana. Maisha yana changamoto nyingi tena tofauti tofauti na ni kweli changamoto hizo zinatufanya tuwe imara. Changamoto unaweza kukumbana nazo hata kama unaishi na wazazi wote wawili. Haileti maana kwamba sababu wewe ulipitia kwa ndugu then na mwanao ukambwage huko ili awe imara. Malezi utakayompa hapo hapo yanaweza kumuimarisha kwa kiwango cha kutosha.
 
Inaelekea kila mtu kayapitia haya. Sasa cha kunuia hapa c kwamba mtoto wako asiende kwa mtu, bali usije mtendea hivyo mtoto wa mtu mwingine. Kwa maana hii dunia tunategemeana, ina wezekana ukawa umejidhatiti vya kujitosheleza, lakini kunamatukio yanatokea mtoto anajikuta yupo kwa watu bila kupenda. kila mtu akimjali mtoto wa Mwingine kama wakwake, hakuna mtoto atakaye nyanyasika.
 
hah hah haha...............we mchokozi?
wajukuu zako kiunoni wanakusalimia!!!!!
kumbuka idadi ya hao wajukuu ulopewa haizidi 450. Kumbuka ulianza lini kupoteza mmoja mmoja kwa mwezi ukizidisha kwa idadi ya miezi lapsed tangu uvunje ungo hadi sasa, alafu toa kwa 450 baki itakuwa ndo idadi ya watoto ulobaki nao!
 

kwa sababu wanawake ndio msingi wa nyumba mambo yote ya jikoni na mengineyo ni wao na si kinababa so ni vigumu sana kukuta baba ananyima mtu chakula na ndio maana sio rahisi kuona akina baba wana roho mbaya but kwa experience yangu mimi wakina baba wanaweza wakawa wabbaya zaidi hasa inapokuja kama wewe ni mwanamke. so wote ni sawa tu!!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…