Kutumia jina la Mwenyezi Mungu kisiasa ni kujitafutia balaa

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,505
51,107
Imekuwepo tabia katika nchi hii hivi karibuni, serikali au viongozi wakitaka kuungwa mkono na umma katika mambo kadha wa kadha wanakimbilia kwenye dini.

Tabia hii ya ajabu kwa kiasi kikubwa ilianzishwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda smbaye kila alipokuwa akipata msukosuko wa kisiasa, akitakiwa atoe majibu ya tuhuma zinazomkabili kama vile Vyeti feki, au kuvamia Studio za redio alikuwa immediately anakimbilia makanisani, kanisa moja baada ya jingine, amewahi kwenda pia kwenye hadhara ya masheikh ili wamuombee. Sasa kuombea mtu siyo tatizo, lakini hilo suala linapotumika mara kwa mara kiasi cha kuonyesha kuwa huyu mtu anatumia mgongo wa dini ili kufikia malengo ya kisiasa ni tatizo kubwa sana hilo.

Tabia hii ya Makonda bahati mbaya ilirithiwa na Rais Magufuli ambaye naye siku za Karibuni amekuwa akijiweka mbele kwenye mambo ya dini kiasi cha kuonyesha kuwa sasa naye anachanganya dini na siasa, kitu ambacho ni hatari sana kwa umoja na mshikamano na uneutral wa kiserikali pindi ikitakiwa kuwa neutral

Siku hizi Raisi Magufuli hata akienda kwenye Ibada binafsi za jumapili Taifa zima linapewa press release kuwa Magufuli leo kasali wapi na saa ngapi, Sisi kama Taifa kusali kwa Magufuli misa ya saa fulani. katika kanisa fulani inatuhusu nini? -—Mwalimu Nyerere alikuwa akisali kila siku misa za asubuhi na jumapili mbona hatukuwahi. kuona mambo hayo?

Lakini ukiachilia mbali hilo, siku za karibuni rais Magufuli amekuwa akitoa miongozo ya kisera ya serikali makanisani, mfano ni kipindi kile cha korona alipokuwa akitoa misimamo ya serikali juu ya hatua anazofanya au anakusudia kufanya mintaarafu ya suala hilo.

Sasa ukichunguza kwa makini utaona kuwa kuna siasa nyingi ndani ya matendo haya, ni utaratibu wenye lengo la kuifanya jamii ya watanzania ambayo asilimia kubwa ni waamini Mungu waseme "aah, ona kumbe tuna raisi mcha Mungu, aah tuna mkuu wa mkoa mcha Mungu" n. k

Sasa cha kusikitisha zaidi ni kuwa Jina tukufu la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema limekuwa likitumika kwa ajili ya manufaa binafsi ya kisiasa ya baadhi ya wanasiasa wakishirikiana na baadhi ya viongozi wa dini ambao kwa hulka na matendo yao jamii inawajua kuwa ni watu wasanii, hawana usafi wowote wa kimaadili na kimatendo.

Just imagine, Hawa viongozi wanaitisha makongamano repeatedly ndani ya muda mfupi usiozidi siku 10 kuilink serikali na dini.

Hebu cheki hii:
Tarehe 15 TAG wanaitisha kongamano kumpa zawadi Magufuli alivyopambana na Korona

Tarehe 17 Viongozi wa dini wanaitisha kongamano la kusifu utendaji wa serikali wa miaka 5

Tarehe 24 Viongozi wa dini wanaitisha kongamano eti la kuombea uchaguzi litakalohudhuriwa na viongozi kedekede wa serikali wakiongozwa na Magufuli

Waislamu wana kitu kinachoitwa kumshirikisha Mwenyezi Mungu. Maana ya hili jambo siyo tu kwenda kwa waganga na wachawi, bali inamaanisha kulitumia Jina la Mwenyezi Mungu na Utukufu wake kwa mambo binafsi ambayo si ya Kimungu huku ukijifanya kuwa yana baraka za Mungu kumbe kuna uwongo, ulaghai na hila ndani yake.

Tunayo sababu za kuamini kuwa viongozi hawa wa kidini wanasukumwa na masilahi yao binafsi na wala hawana dhati ya Kimungu kwa sababu tunafahamu kuwa baadhi yao wameanza kupata teuzi na wengine wameanza kupitishwa na vysma vya siasa kugombea nyadhifa za kisiasa.

Nawatahadharisha Wanasiasa na viongozi wa Dini wenye kutumia Jina La Mwenyezi Mungu kisiasa na ndivyosivyo, kuwa Mwenyezi Mungu anawaona, Hadhihakiwi, na ana uwezo wa kuwachapa kiboko wasijue kimetoka wapi!

Mwalimu alitahadharisha sana kuhusu suala la mtawala na ishu za dini, alisema hivi si vizuri mtawala kujiweka mbali na mambo ya dini lakini si vizuri mtawala kuegemea huko!

Tusimtanie Mungu, Kiboko chake ni kikali!
 
Anatafuta kura za waumini kilaini!Kura za waumini wa hivyo hazihitaji sera,wao ukienda kusali kanisani kwao tayari unazoa kura zao!
 
Umeandika "Mwalimu Nyerere alikuwa akisali kila siku misa za asubuhi na jumapili mbona hatukuwahi. kuona mambo hayo? "

Wewe jamaa unafurahisha sana!

Wewe inawezekana ni wale watoto wa DOT.COM ambao hawajui vizuri historia ya nchi hii!

Hujui kama wakati wa utawala wa Mwl. Nyerere kuwa na television ilikuwa ni kosa la jinai.

Sasa wananchi wangeona wapi wakati hata kuwa ma Tv ilikuwa ni hairuhusiwi?

Hata redio vijijini zilikuwa zinapatikana kwa wenyeviti wa vijiji achilia mbali kila kaya!
 
Ndugu Mtoa Mada!

Soma Hadithi ya Sauli na Daudi kwenye Biblia utakuwa umemaliza kila kitu kwenye tafakuri yako!!

Hakuna tofauti kati ya Sauli na Jiwe, na kati ya Mfalme Daudi na Tundu Lissu

1. Sauli aliteuliwa na Mungu kuwa Mfalme baada ya Watoto wa Eli na Baba yao kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu na wana israel kudai sasa wanataka mfalme, rejea kipindi cha kampeni 2015 watanzania kudai diktekta, na Jiwe kuwa Raia namba 1

2. Sauli baada ya kupata ufalme akaanza kukengeuka. Rejea mambo aliyoanza kufanya Jiwe baada ya kuchukua uongozi

3. Mungu alivyoona Sauli nae anakengeuka akaamua kumnyanyua Daudi, Rejea kunyanyuka kwa nguvu kwa Tundu Lissu baada ya Jiwe kuanza udiktekta uchwara!

4. Sauli alipoona Daudi anataka kuwa mfalme akajaribu kumuua ila Mungu akamponya Daudi, Rejea jaribio la mauaji la Tundu Lissu na kuponywa kimiujiza kwenye risasi 16

5. Wana Israeli walianza kumpenda Daudi badala ya Sauli na Sauli alianza kuwatesa wana Israel, Rejea upendo wa watanzania ulivyozidi kuwa maradufu kwa Lissu na jinsi Jiwe anavyowatesa wakosoaji wake Mf. Erick Kabendera, Tito Magoti na Mdude Nyangali

6. Sauli kukimbilia kwa manabii wa uongo baada ya kuachwa na Mungu( Hadi mwisho kwenda kwa mganga wa kienyeji), Rejea jiwe anavyojiweka karibu na kuambatana na watu wanaojiita viongozi wa dini kumbe ni manabii wa uongo, Rejea pia Mganga wa Kienyeji I Sheikh Sharif Majini anavyomtabiria Jiwe na kujiweka karibu nae.

7. Mungu kumkataa Rasmi Sauli na kumfanya Daudi kuwa Mfalme!

Hili ndo jambo la mwisho linaloenda kutokea hapo October 2020. Sababu kuu aliyotumia Mungu ni kwa Sauli kutegemea nguvu zake pamoja na za waganga wa kienyeji, Kuna mtu anawategemea viongozi wa dini pamoja na waganga wa kienyeji kama Sheikh Sharif Majini ili wamfanye kuwa Raisi, Sasa Mungu hapendi hili na anaenda kujibu kwa hasira hapo October kwa kumthibitisha ikulu Tundu Antipas Lissu( Mfalme Daudi)

Tukutane October!!!
 
Ndugu Mtoa Mada!

Soma Hadithi ya Sauli na Daudi kwenye Biblia utakuwa umemaliza kila kitu kwenye tafakuri yako!!

Hakuna tofauti kati ya Sauli na Jiwe, na kati ya Mfalme Daudi na Tundu Lissu

1. Sauli aliteuliwa na Mungu kuwa Mfalme baada ya Watoto wa Eli na Baba yao kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu na wana israel kudai sasa wanataka mfalme, rejea kipindi cha kampeni 2015 watanzania kudai diktekta, na Jiwe kuwa Raia namba 1

2. Sauli baada ya kupata ufalme akaanza kukengeuka. Rejea mambo aliyoanza kufanya Jiwe baada ya kuchukua uongozi

3. Mungu alivyoona Sauli nae anakengeuka akaamua kumnyanyua Daudi, Rejea kunyanyuka kwa nguvu kwa Tundu Lissu baada ya Jiwe kuanza udiktekta uchwara!

4. Sauli alipoona Daudi anataka kuwa mfalme akajaribu kumuua ila Mungu akamponya Daudi, Rejea jaribio la mauaji la Tundu Lissu na kuponywa kimiujiza kwenye risasi 16

5. Wana Israeli walianza kumpenda Daudi badala ya Sauli na Sauli alianza kuwatesa wana Israel, Rejea upendo wa watanzania ulivyozidi kuwa maradufu kwa Lissu na jinsi Jiwe anavyowatesa wakosoaji wake Mf. Erick Kabendera, Tito Magoti na Mdude Nyangali

6. Sauli kukimbilia kwa manabii wa uongo baada ya kuachwa na Mungu( Hadi mwisho kwenda kwa mganga wa kienyeji), Rejea jiwe anavyojiweka karibu na kuambatana na watu wanaojiita viongozi wa dini kumbe ni manabii wa uongo, Rejea pia Mganga wa Kienyeji I Sheikh Sharif Majini anavyomtabiria Jiwe na kujiweka karibu nae.

7. Mungu kumkataa Rasmi Sauli na kumfanya Daudi kuwa Mfalme!

Hili ndo jambo la mwisho linaloenda kutokea hapo October 2020. Sababu kuu aliyotumia Mungu ni kwa Sauli kutegemea nguvu zake pamoja na za waganga wa kienyeji, Kuna mtu anawategemea viongozi wa dini pamoja na waganga wa kienyeji kama Sheikh Sharif Majini ili wamfanye kuwa Raisi, Sasa Mungu hapendi hili na anaenda kujibu kwa hasira hapo October kwa kumthibitisha ikulu Tundu Antipas Lissu( Mfalme Daudi)

Tukutane October!!!

Uchambuzi mzuri sana huu
 
Umeandika "Mwalimu Nyerere alikuwa akisali kila siku misa za asubuhi na jumapili mbona hatukuwahi. kuona mambo hayo? "

Wewe jamaa unafurahisha sana!

Wewe inawezekana ni wale watoto wa DOT.COM ambao hawajui vizuri historia ya nchi hii!

Hujui kama wakati wa utawala wa Mwl. Nyerere kuwa na television ilikuwa ni kosa la jinai.

Sasa wananchi wangeona wapi wakati hata kuwa ma Tv ilikuwa ni hairuhusiwi?

Hata redio vijijini zilikuwa zinapatikana kwa wenyeviti wa vijiji achilia mbali kila kaya!

Redio Tanzania (RTD), Magazeti ya Uhuru, Mzalendo, Mfanyakazi, Dailynews yalikuwepo
 
Mungu huwa hadhihakiwi, kila mtu atapokea kulingana na matendo yake.
 
Mungu huwa hadhihakiwi, kila mtu atapokea kulingana na matendo yake.
Huyu Jiwe anaenda kupigwa pigo kuu na Mungu mwaka huu ndugu yangu.
Kwa aliyoyafanya tu kwa Erick Kabendera mpaka mama yake akafa kifo cha mateso namna ile, tungekuwa na viongozi wa dini wa kweli, hakuna hata mmoja ambaye angemuunga mkono Jiwe leo.

Hii nchi wameinajisi sana ila mwisho wa haya yote ni October mwaka huu!!

Twende na Lissu

Twende na Chadema!
 
Back
Top Bottom