KUTUMA PESA KIMAKOSA.

KUTUMA PESA KIMAKOSA.

Kama kweli umeambiwa hivyo basi huyo operator wa siku ni eidha mgeni au atamtafuta mhusika kwa wakati wake wamalizane. Pesa haiwezi potea kwa sasa ktk mitandao ingawa inaweza chelewa kurudi. Labda uwe umetuma ktk namba ambayo 'haijasajiliwa' KAMA hii inawezekana.
Mkuu pesa inapotea vizuri kabisa yani.na kama jamaa ni mjanja pia humpati

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: bbc
Mkuu hapo ushauri wangu,ila maybe kama jamaa ataendelea kuitumia hiyo line kufanyia miamala.

Ongea na customer service au nenda waombe waitegee hiyo line yake mdomo wa mamba.yani akiweka tu mpunga,inakuja kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuipata itawezekana endapo tu sheria ya kuwa na line moja itakuwepo au laa sivyo mitandao ya simu itusaidie kuwapata
 
huku unapoteza muda
hakuna pesa inayopotea katika mitandao kwa sababu wote wameandikishwa na wanajulikana wanakoishi na Mjumbe wao wa mtaa,
ndio maana tunasisitiza kuwasiliana na Operator wa mtandao wako mara mojapesa yako utaipata
Mfano mzuri ni hawa wanaokopesha mfano TIMIZA, Branci, Tala nk hawawajui wateja lkn huwezi waibia kwai kila mmoja ana anwani kamili
MY TAKE
Habari zako si za kweli kwani hujatuwekea no. ya huyo mwizi na mtandao anaotumia
ni sasa hivi tutamnanga na nduguze watamjua na utarudishiwa asubuhi
tafadhali weka namba zake hapa JF
Wewe ndo mjinga zaidi kuliko hata aliyetuma ki-makosa hiyo pesa. Unasema hakuna pesa inayopotea wakati hiyo imepotea!?? Hiyo ni transaction halali imefanyika,na kwenye mtandao hawawezi kujua km umekosea mpaka utoe taarifa km hizo. Km pesa imetolewa hiyo siyo kesi tena ya kampuni ya simu. Ni kwa wewe mteja kwenda police kutoa taarifa na ww ndo ufanye taratibu za kumpata mwizi wako ili police wamkamate. Lkn tukirudi kwa mtumaji,nae pia mjinga,hivi kutuma pesa unakoseaje!?? Unatuma pesa laki 4 halafu hujui unamtumia nani!!!? Maana km unamjua huwezi kukosea,kwa sababu jina linatoka kabla hujaruhusu hiyo pesa! Watanzania tujifunze kuwa makini kwenye issue muhimu hasa zinazohusu pesa...
 
ona mimi nilichokifanya
Sikumoja nilikosea nikatuma Tsh.250,000 kwa *wrong number*, baada ya kuona hilo, niliamua kujaribu kutuma sms ya kutisha alieipokea hela hiyo...

Text hiyo niliiandika hivi,
_*Habari yako rafiki, naitwa Otiko, ni balozi wa kanisa jipya la Shetani hapa Tanzania. Ni tumaini langu umeiona posho yetu uanachama ya Tsh.250,000 tumekutumia TIGOPESA ili kujiunga na kanisa letu la Shetani. Huo ni mwanzo tu wa mambo mazuri yanakuja. Usiku wa leo tuna mkutano ambapo tutachinja watu watatu kwa ajili ya kafara. Tumekubaliana kufanya kafara hii katika viwanja vya nyumbani kwako mida ya saa nane za usiku na unatakiwa uchague mmoja wa watu unawapenda ili tunywe damu yake pia. Lakini kama hungependa kujiunga katika kanisa letu hili la Shetani, rudisha hiyo pesa kwa namba yangu hii hii"*_

Baada kama ya dk 10, nikapokea sms inasema, _*"Oyoo bro, kama vp tuma Tsh.250,000 nyingine kuna mshikaji wangu nae kavutiwa na kanisa lenu"*_

Kidogo nizimie🤣

Yaani watu vyuma vimekaza kiasi kwamba wako tayari kwa lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuu, kweli chuma kimekaza, watu wako tayari kwa lolote!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasema alie pokea kashaitoa tayari, nasiwezi ipata tena.
Ila now naenda police.
Wanajibu only that simple, sasa nini maana ya watu kusajili laini na vitambulisho serious they must be smart than this
pole sana kwa mtu ambaye haijamkuta anaweza akajibu anavyoona yeye ni sawa ila ni jambo ambalo linaumiza hili
 
ona mimi nilichokifanya
Sikumoja nilikosea nikatuma Tsh.250,000 kwa *wrong number*, baada ya kuona hilo, niliamua kujaribu kutuma sms ya kutisha alieipokea hela hiyo...

Text hiyo niliiandika hivi,
_*Habari yako rafiki, naitwa Otiko, ni balozi wa kanisa jipya la Shetani hapa Tanzania. Ni tumaini langu umeiona posho yetu uanachama ya Tsh.250,000 tumekutumia TIGOPESA ili kujiunga na kanisa letu la Shetani. Huo ni mwanzo tu wa mambo mazuri yanakuja. Usiku wa leo tuna mkutano ambapo tutachinja watu watatu kwa ajili ya kafara. Tumekubaliana kufanya kafara hii katika viwanja vya nyumbani kwako mida ya saa nane za usiku na unatakiwa uchague mmoja wa watu unawapenda ili tunywe damu yake pia. Lakini kama hungependa kujiunga katika kanisa letu hili la Shetani, rudisha hiyo pesa kwa namba yangu hii hii"*_

Baada kama ya dk 10, nikapokea sms inasema, _*"Oyoo bro, kama vp tuma Tsh.250,000 nyingine kuna mshikaji wangu nae kavutiwa na kanisa lenu"*_

Kidogo nizimie🤣

Yaani watu vyuma vimekaza kiasi kwamba wako tayari kwa lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha mimi ningerudisha
 
A lot of money, pole chief. Nenda police wataitreat kama Cyber crime kwa ufuatiliaji mzuri utafanikisha kumpata mtu wako ila ndiyo unaweza kukuta kaitumia.
 
Nina uhakika hili ni jukwaa sahihi kwa tatizo lililo nikuta.
Leo mida ya saa 6 na 15 mchana nili tuma pesa kimakosa, haikufika kwa mlengwa, ilienda kwa mtu tofauti.
Nili jaribu kuwa pigia customer service wa mtandao husika ila nika ambiwa kuwa hela imekwisha tolewa tayari, siwezi ipata tena. Ni Tsh 400,000/=.

Hali ya maisha ni ngumu kwa upande wangu.
Nika jaribu kumpigia aliepokea pesa, alipokea na kusema kwa haraka "Nitakupigia badaye" kisha akakata simu.
Nika jaribu kupiga tena simu haikupatikana mpaka sasa.

Najua humu kuna watu wana jua nisiyo yajua. Kama kuna njia nyingine ya kuipata pesa yangu au kumpata mtu nilie mtumia pesa, please tell me.
Report police na tafuta police anayehusikana mambo ya cyber crime mpe hata 50 ili mambo yaende haraka.. baada ya kufanya haya kazi imesha isha. Atawasiliana na customer care kisha ataomba mawasiliano ya watu wa karibu wa yule mtu aliye chukua ile pesa yaan no anazowasiliana nazo mara kwa mara na atawatumia hao watu kuwabana na ukipata hela yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Report police na tafuta police anayehusikana mambo ya cyber crime mpe hata 50 ili mambo yaende haraka.. baada ya kufanya haya kazi imesha isha. Atawasiliana na customer care kisha ataomba mawasiliano ya watu wa karibu wa yule mtu aliye chukua ile pesa yaan no anazowasiliana nazo mara kwa mara na atawatumia hao watu kuwabana na ukipata hela yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushauli mzuri, police wa kitengo hcho hupewa kila details za namba iliyopokea hadi na watu wake wa karibu, hvo n rahisi sana kuwapata watu wake wa karibu hata kama atabadili line.

Sent using [Tecno Camon CX]
 
Mimi nilituma Tsh 20,000.nikapiga simu kitengo chao walinijibu kuwa pesa imetolew hivyo hamna njia nyingine.
 
Fungua kesi ya madai au mtafute mwanasheria akushauri. Mshitakiwa ni huyo mwenye number na shahidi ni huo mtandao wa simu
Hakimu atatoa kibali huyo jamaa atafutwe kwa msaada wa huyo shahidi mpaka apatikane.
 
Nina uhakika hili ni jukwaa sahihi kwa tatizo lililo nikuta.
Leo mida ya saa 6 na 15 mchana nili tuma pesa kimakosa, haikufika kwa mlengwa, ilienda kwa mtu tofauti.
Nili jaribu kuwa pigia customer service wa mtandao husika ila nika ambiwa kuwa hela imekwisha tolewa tayari, siwezi ipata tena. Ni Tsh 400,000/=.

Hali ya maisha ni ngumu kwa upande wangu.
Nika jaribu kumpigia aliepokea pesa, alipokea na kusema kwa haraka "Nitakupigia badaye" kisha akakata simu.
Nika jaribu kupiga tena simu haikupatikana mpaka sasa.

Najua humu kuna watu wana jua nisiyo yajua. Kama kuna njia nyingine ya kuipata pesa yangu au kumpata mtu nilie mtumia pesa, please tell me.

Natabiri kuwa hao customer service wa huo mtandao husika ni tigo!!....kama nimekosea niite mbwa!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walicho nambia hakina matumaini, walisema alie pokea tayari kaitoa.
Mtu yoyote anayemiliki line ya simu lazima awe na vitambulisho sahihi na anapigwa picha ili kuthibitisha kuwa ni yeye hata kama atatumia sura na kitambulisho cha mtu mwingine ni dhahiri kuwa mtu huyo anaukaribu na mtu huyo. Customer care hujibu hivyo ili kuepusha mlolongo wa maswali na kesi zinazohusu masuala ya mtandao. Kwa hali ya sasa ya ukuaji wa Tecknolojia mtu ukipata namba ya simu yake umempata kwa sasabb watu wengi wanatumia vitambulisho vya kupigia kura na wanapiga picha.
Ushauri wangu
Chukulia kama umetoa sadaka (Najua unahitaji pesa na una wakati mgumu kiifedha). Watu kwa sasa wana hali ngumu kifedha kwahiyo utaenda polisi utaandikisha maelezo na pia utaenda kwa tawi la mtandao (Hapa pesa itakutoka kote kote). Zitaanza process za kumtafuta jamaa na atapatikana. Utakuta mtu kajichokea na wengine wameondoka nyumbani muda mrefu na hawasiliani na ndugu. Utamfunga na mwisho wa siku utajikuta umepoteza muda na pesa zako bure. Cha kufanya ongea na customer care vizuri kama mtu huyo ataweka pesa kwenye hiyo line watakurudishia hata kama siyo kiasi husika.
Tahadhari.
Siku nyingine ukitaka kutuma fedha ni vizuri umwambie wakala akutumie kwenye sim card yako na pia mhusika akutajie jina alilosajilia ili kabla ya kupress 1 to confirm liwe jina husika na pia kama una smartphone basi ui-copy na ui-paste namba hiyo katika kibox cha kujaza namba za mtumiwa.
Pole sana (Kilo 4 ni nyingi kwa maisha ya sasa ya wale wa tia mchuzi kwangu pakavu)
 
Nadhani iwekwe Sheria ya pesa inayotumwa kwa njia za simu imfikie mpokeaji ila hasiweze kuzitoa baada ya angalau dakika 30

Ama wakati anataka kutoa hizo hela basi mtumaji apokee SMS ya kumfahamisha kwamba uliyemtumia Pesa mtu x anataka kutoa hiyo hela. Basi mtumaji akikubali mtoaji ataweza kutoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom