KUTUMA PESA KIMAKOSA.

KUTUMA PESA KIMAKOSA.

Snowden E

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2018
Posts
1,703
Reaction score
3,011
Nina uhakika hili ni jukwaa sahihi kwa tatizo lililo nikuta.
Leo mida ya saa 6 na 15 mchana nili tuma pesa kimakosa, haikufika kwa mlengwa, ilienda kwa mtu tofauti.
Nili jaribu kuwa pigia customer service wa mtandao husika ila nika ambiwa kuwa hela imekwisha tolewa tayari, siwezi ipata tena. Ni Tsh 400,000/=.

Hali ya maisha ni ngumu kwa upande wangu.
Nika jaribu kumpigia aliepokea pesa, alipokea na kusema kwa haraka "Nitakupigia badaye" kisha akakata simu.
Nika jaribu kupiga tena simu haikupatikana mpaka sasa.

Najua humu kuna watu wana jua nisiyo yajua. Kama kuna njia nyingine ya kuipata pesa yangu au kumpata mtu nilie mtumia pesa, please tell me.
 
Peleka namba kituo cha Polisi na taarifa zako muhimu za miamala kuna kitengo cha IT kule watakusaidia
N.B ili suala lako liende haraka ongea nao kwa HERUFI KUBWA

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
 
Ni ujinga wako mwenyewe
Kanla ys kutuma unahakiki jina na # kishs unathibitisha...labda ew kipofu
 
huku unapoteza muda
hakuna pesa inayopotea katika mitandao kwa sababu wote wameandikishwa na wanajulikana wanakoishi na Mjumbe wao wa mtaa,
ndio maana tunasisitiza kuwasiliana na Operator wa mtandao wako mara mojapesa yako utaipata
Mfano mzuri ni hawa wanaokopesha mfano TIMIZA, Branci, Tala nk hawawajui wateja lkn huwezi waibia kwai kila mmoja ana anwani kamili
MY TAKE
Habari zako si za kweli kwani hujatuwekea no. ya huyo mwizi na mtandao anaotumia
ni sasa hivi tutamnanga na nduguze watamjua na utarudishiwa asubuhi
tafadhali weka namba zake hapa JF
 
Peleka namba kituo cha Polisi na taarifa zako muhimu za miamala kuna kitengo cha IT kule watakusaidia
N.B ili suala lako liende haraka ongea nao kwa HERUFI KUBWA

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
Thanks
 
huku unapoteza muda
hakuna pesa inayopotea katika mitandao kwa sababu wote wameandikishwa na wanajulikana wanakoishi na Mjumbe wao wa mtaa,
ndio maana tunasisitiza kuwasiliana na Operator wa mtandao wako mara mojapesa yako utaipata
Mfano mzuri ni hawa wanaokopesha mfano TIMIZA, Branci, Tala nk hawawajui wateja lkn huwezi waibia kwai kila mmoja ana anwani kamili
MY TAKE
Habari zako si za kweli kwani hujatuwekea no. ya huyo mwizi na mtandao anaotumia
ni sasa hivi tutamnanga na nduguze watamjua na utarudishiwa asubuhi
tafadhali weka namba zake hapa JF
Umeanza vizuri ila umeharibu mwisho.
 
Umeanza vizuri ila umeharibu mwisho.
acha hadithi za Shigongo
weka namba za huyo aliyechukua 400,000.00 tumuombee, tupige kipapayu, tumlaani, tumuaibishe
Laki nne si mchezo kwa usawa huu unashindwa kumripoti
 
Pole sana mkuu,mhudumu wa mtandao wako kakuambia nini kifanyike ili upate pesa yako..!?kwasababu wao ndio wenye taarifa za aliyepokea pesa kimakosa

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanasema alie pokea kashaitoa tayari, nasiwezi ipata tena.
Ila now naenda police.
 
Walicho nambia hakina matumaini, walisema alie pokea tayari kaitoa.
Kama kweli umeambiwa hivyo basi huyo operator wa siku ni eidha mgeni au atamtafuta mhusika kwa wakati wake wamalizane. Pesa haiwezi potea kwa sasa ktk mitandao ingawa inaweza chelewa kurudi. Labda uwe umetuma ktk namba ambayo 'haijasajiliwa' KAMA hii inawezekana.
 
acha hadithi za Shigongo
weka namba za huyo aliyechukua 400,000.00 tumuombee, tupige kipapayu, tumlaani, tumuaibishe
Laki nne si mchezo kwa usawa huu unashindwa kumripoti
Yaani aweke namba hapa ya huyo mtu ili iweje? Acha ujanja wako wewe. Umeshaona fursa.
 
Nina uhakika hili ni jukwaa sahihi kwa tatizo lililo nikuta.
Leo mida ya saa 6 na 15 mchana nili tuma pesa kimakosa, haikufika kwa mlengwa, ilienda kwa mtu tofauti.
Nili jaribu kuwa pigia customer service wa mtandao husika ila nika ambiwa kuwa hela imekwisha tolewa tayari, siwezi ipata tena. Ni Tsh 400,000/=.

Hali ya maisha ni ngumu kwa upande wangu.
Nika jaribu kumpigia aliepokea pesa, alipokea na kusema kwa haraka "Nitakupigia badaye" kisha akakata simu.
Nika jaribu kupiga tena simu haikupatikana mpaka sasa.

Najua humu kuna watu wana jua nisiyo yajua. Kama kuna njia nyingine ya kuipata pesa yangu au kumpata mtu nilie mtumia pesa, please tell me.
Hela imeshatolewa mkuu kuipata ni ngumu, ingekuwa bado ipo kwenye simu ingewezekana lakini kwa hapo ni kumuombea tu huyo uliyemtumia apate moyo wa huruma ili akurudishie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ona mimi nilichokifanya
Sikumoja nilikosea nikatuma Tsh.250,000 kwa *wrong number*, baada ya kuona hilo, niliamua kujaribu kutuma sms ya kutisha alieipokea hela hiyo...

Text hiyo niliiandika hivi,
_*Habari yako rafiki, naitwa Otiko, ni balozi wa kanisa jipya la Shetani hapa Tanzania. Ni tumaini langu umeiona posho yetu uanachama ya Tsh.250,000 tumekutumia TIGOPESA ili kujiunga na kanisa letu la Shetani. Huo ni mwanzo tu wa mambo mazuri yanakuja. Usiku wa leo tuna mkutano ambapo tutachinja watu watatu kwa ajili ya kafara. Tumekubaliana kufanya kafara hii katika viwanja vya nyumbani kwako mida ya saa nane za usiku na unatakiwa uchague mmoja wa watu unawapenda ili tunywe damu yake pia. Lakini kama hungependa kujiunga katika kanisa letu hili la Shetani, rudisha hiyo pesa kwa namba yangu hii hii"*_

Baada kama ya dk 10, nikapokea sms inasema, _*"Oyoo bro, kama vp tuma Tsh.250,000 nyingine kuna mshikaji wangu nae kavutiwa na kanisa lenu"*_

Kidogo nizimie🤣

Yaani watu vyuma vimekaza kiasi kwamba wako tayari kwa lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huku unapoteza muda
hakuna pesa inayopotea katika mitandao kwa sababu wote wameandikishwa na wanajulikana wanakoishi na Mjumbe wao wa mtaa,
ndio maana tunasisitiza kuwasiliana na Operator wa mtandao wako mara mojapesa yako utaipata
Mfano mzuri ni hawa wanaokopesha mfano TIMIZA, Branci, Tala nk hawawajui wateja lkn huwezi waibia kwai kila mmoja ana anwani kamili
MY TAKE
Habari zako si za kweli kwani hujatuwekea no. ya huyo mwizi na mtandao anaotumia
ni sasa hivi tutamnanga na nduguze watamjua na utarudishiwa asubuhi
tafadhali weka namba zake hapa JF
mkuu hapa sijakuelewa..umesema wale Timiza ,branch na wengine huwezi waibia??

kwa mfano ukawakopa kisha ukamute ,vipi wanawezaje kukufyatilia??



Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom