Kutoongezeka kwa mapato bandarini Dar: Serikali yawahamisha watumishi wa TRA waliokaa muda mrefu

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Waziri wa Fedha Philip Mpango ameiagiza TRA kufanya mabadiliko makubwa kwa watumishi wake waliopo bandarini baada ya kubainika wanahusika na upotevu wa mapato.

Dk. Mpango alitoa maagizo hayo baada ya kufanya ziara yakushtukiza kitengo cha forodha bandarini Dar Es Salaam na kutoa siku 7 kwa TRA kumpa majibu juu ya utekelezaji wa agizo hilo.

Amesema watakao bainika waondolewe kabisa kwani kuna vijana wengi waliohitimu ambao wapo tayari kufanya kazi.

Dk. Mpango alisema akisikia juu ya upotevu wa mapato tena atawatimua wakuu wa kitengo hicho.

''Sasa next time nikija nikiyasikia tena haya ina maana hamjapiga jicho la kutosha, na mimi subira Mungu hakunipa, sina.Nitakutazameni usoni nitawatimueni''



------------
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, amefanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Forodha Bandarini, na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kufanya mabadiliko ya watumishi walioko katika idara ya upimaji na ukaguzi wa mizigo.

Akiwa kwenye ziara hiyo Dk Mpango alisema imebainika kwamba kuna baadhi ya watumishi wanaojihusisha na upotevu wa mapato ya Serikali.

Waziri huyo alitoa siku saba kwa TRA kumpa taarifa kamili ya utekelezaji wa maagizo hayo, ikiwamo kuwahamisha watumishi wote waliokaa muda mrefu kwenye eneo hilo la upimaji na ukaguzi wa mizigo ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato ya Serikali katika bandari hiyo.

Waziri huyo alishangazwa na kitendo cha mapato bandarini kutoongezeka licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali kuiboresha akisema inatokana na baadhi ya watumishi kushirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kodi ya Serikali.

“Pamoja na kuwepo kwa mitambo ya kukagua mizigo (scanners), baadhi ya bidhaa zinakadiriwa kodi ndogo ikilinganishwa na thamani ya mizigo huku mizigo mingine ikiwa si ile iliyotajwa kuwamo kwenye makontena na hupitishwa na watumishi wasio waaminifu” alisema Waziri Mpango.

Aliuagiza uongozi wa TRA kuhakikisha unaongeza mapato katika Bandari ya Majahazi kutoka wastani wa mapato ya Sh3.5 bilioni kwa mwezi hadi Sh5 bilioni kuendana na malengo yaliyowekwa baada ya kubainika kwamba kuna ukwepaji mkubwa wa mapato ya Serikali katika eneo hilo.

Pia, Dk Mpango ambaye aliwahi kuwa Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo kabla ya kuteuliwa kuwa mbunge na kisha waziri, aliutaka uongozi huo wa TRA kuhakikisha kuwa Bandari ya Majahazi inaanza mara moja kutumia mfumo wa kukusanya mapato ujulikanao kama Tansis ili kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi.

Aidha, aliviagiza vyombo vya dola kuwachunguza watumishi wote wakiwamo wa ngazi za juu katika idara ya forodha bandarini na kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vyovyote vinavyoikosesha Serikali mapato.

Ofisa Habari Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Leonard Magomba alitoa tahadhari kwa watu wote ambao wana tabia ya kuingia maeneo ya bandari kwa lengo la kuiba mali za wateja akiwataka kuacha mara moja kwani vifaa vya ulinzi na usalama vilivyopo hivi sasa ni vya kisasa na vina uwezo wa kubaini wezi katika maeneo yote ya bandari.

Hivi karibuni, Rais John Magufuli alitembelea TPA na kuiagiza mamlaka hiyo kununua mashine nne za kukagulia mizigo inayoingia bandarini hapo.

Pia, Rais Magufuli aliagiza mkataba wa kampuni ya Kimataifa ya Kuhudumia Shehena za Kontena Bandarini (Ticts), ufanyiwe marekebisho ili kulinufaisha Taifa kutokana na oparesheni zake bandarini.

Rais aliitaka TPA kujenga bandari kavu Mlandizi na kutozitumia binafsi zilizopo kwa kuwa zinatumika kukwepa kodi.

Itakumbukwa kwamba, Novemba 2015 muda mfupi baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alifanya ziara ya ghafla TRA na bandarini na kuwasimamisha kazi maofisa watano na watumishi watatu kutokana na upotevu wa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya Sh80 bilioni.

Desemba 2015, Waziri Mkuu alifanya ziara nyingine ya kushtukiza bandarini na kukagua mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo na utozaji wa malipo baada ya kupewa taarifa kwamba kuna makontena 2,431 yametolewa bila kulipiwa ushuru.

Alisema kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa bandari ya kuanzia Machi hadi Septemba 2014, makontena hayo yalipita bila kulipiwa kodi kupitia bandari kavu nne (ICD).

“Mmeamua kuwasimamisha kazi watu wadogo na kuwaacha wakubwa wanaendelea na kazi. Hatuwezi kuendelea kuikosesha Serikali mapato namna hii,” alisema Waziri Mkuu.

Akiwa kwenye chumba cha scanner, Waziri Mkuu alikuta manifest ikisema kontena limejaa diapers, lakini picha ya kompyuta ya scanner ilionyesha ndani ya kontena hilohilo likiwa na vitu kama vifaa vya umeme.


-Mwananchi-
 
Waziri wa Fedha Philip Mpango ameiagiza TRA kufanya mabadiliko makubwa kwa watumishi wake waliopo bandarini baada ya kubainika wanahusika na upotevu wa mapato.
Dk. Mpango alitoa maagizo hayo baada ya kufanya ziara yakushtukiza kitengo cha forodha bandarini Dar Es Salaam na kutoa siku 7 kwa TRA kumpa majibu juu ya utekelezaji wa agizo hilo
Amesema watakao bainika waondolewe kabisa kwani kuna vijana wengi waliohitimu ambao wapo tayari kufanya kazi


Bora, maana wanajiona miungu watu...
 
..watahaha sana kufukuza watumishi na hata kuwakamua raia hadi pesa yao ya mwisho....lakini wanasahau kuwa pesa pale hazina wanazitumia hovyo kujenga kwao....bila hata kuidhinishwa Na bunge....na nyingine wanafanya matumizi ya kipuuzi Na wanapohojiwa wanataka kuuwa watu....

...pesa haitawahi kujaa kwa serikali hii dhalimu.... Hata wafukuzane wamalizane....hadi watakapojirudi na kuona wanachowafanyia RAIA si vema Na haki....hii ni karma at its best.....
 
..watahaha sana kufukuza watumishi na hata kuwakamua raia hadi pesa yao ya mwisho....lakini wanasahau kuwa pesa pale hazina wanazitumia hovyo kujenga kwao....bila hata kuidhinishwa Na bunge....na nyingine wanafanya matumizi ya kipuuzi Na wanapohojiwa wanataka kuuwa watu....

...pesa haitawahi kujaa kwa serikali hii dhalimu.... Hata wafukuzane wamalizane....hadi watakapojirudi na kuona wanachowafanyia RAIA si vema Na haki....hii ni karma at its best.....
Bwana/bibi Nderingo,
Umesahau nyinyi mlivyokuwa mnajenga kwenu kwa kuiba hela za umma!?
Chuki ya ukabila ndio inayowamaliza kwa sasa. Vumilieni bado miaka Nane. Ukiona inachoma sana hamia Nairobi mkuu.
 
Hizi ajira tupeane kwa kupokezana unafanyakazi miezi sita wanaingia wengine manake kila kona imekuwa fukuza, ajira pekee imekuwa kutoa makontena ya rwanda bandarini
 
...ona huyu shoga mwingine na ukabila....hii dhana ya kuanza kuangalia mambo kwa ukabila ndio anayojenga mkuu wenu wa nchi....ndio maana amewajaza watu wa kwao kwenye utawala wake....

....akili yako ni sawa Na ya unayemtetea...maana ndio mmeifikisha hii nchi hapa....aliyekudanganya mi natoka Kili nani???BTW upofu unakunyima hekima ya hata kutambua jina kwa dhana yako ya ukabila...maana ungeiona ngosha kwenye hilo jina....lakini kwa vile mnawachukia watu wa Kili umabaki Na nderingo.....unaonyesha akili Na fikra ya watawala...

Bwana/bibi Nderingo,
Umesahau nyinyi mlivyokuwa mnajenga kwenu kwa kuiba hela za umma!?
Chuki ya ukabila ndio inayowamaliza kwa sasa. Vumilieni bado miaka Nane. Ukiona inachoma sana hamia Nairobi mkuu.
 
...ona huyu shoga mwingine na ukabila....hii dhana ya kuanza kuangalia mambo kwa ukabila ndio anayojenga mkuu wenu wa nchi....ndio maana amewajaza watu wa kwao kwenye utawala wake....

....akili yako ni sawa Na ya unayemtetea...maana ndio mmeifikisha hii nchi hapa....aliyekudanganya mi natoka Kili nani???BTW upofu unakunyima hekima ya hata kutambua jina kwa dhana yako ya ukabila...maana ungeiona ngosha kwenye hilo jina....lakini kwa vile mnawachukia watu wa Kili umabaki Na nderingo.....unaonyesha akili Na fikra ya watawala...
Matusi ndio mtaji wenu. Nderingo ni jina la wapi? Unajichetua ukifikiri kila mtu ni hayawani kama wewe.
Mlivyokuwa mkiibia Watanzania ilikuwa ni sawa kwa kuwa nyinyi ndio bora kuliko MTANZANIA yoyote.
Wewe ni kiumbe wa ajabu sana siwezi hata kukuita binadamu. Na hata kukutukana haitoshi. Maana maisha yako na Roho yako ni matusi tosha kwa nafsi yako kila jua linapochomoza.
Shame on you! Pathetic Creature.
 
Hilo ndio linavyopaswa kuwa kwa watumishi wa TRA na baadhi ya maeneo mengine kama UHAMIAJI, POLISI, watumishi wa kwenye mizani za kupima magari nk nk..

Lazima wawe wanabadilishwa (rotation) kila baada ya kipindi fulani..

Hili wala sio suala la Waziri kusema..

Alipaswa tu kuwachukulia hatua viongozi wa TRA kwa kutolisimamia hili.
 
Bandari ikitumika vzr ilitosha kuhost nchi zooote ambazo haina bandari lkn, nchi yangu inateketea kwa kukosa uzalendo.
 
...mbwa nyie...hii nchi si yenu....ukabila mnaojenga iko siku utawatokea puani...wauwaji Na watesaji nyie...dogs....

Matusi ndio mtaji wenu. Nderingo ni jina la wapi? Unajichetua ukifikiri kila mtu ni hayawani kama wewe.
Mlivyokuwa mkiibia Watanzania ilikuwa ni sawa kwa kuwa nyinyi ndio bora kuliko MTANZANIA yoyote.
Wewe ni kiumbe wa ajabu sana siwezi hata kukuita binadamu. Na hata kukutukana haitoshi. Maana maisha yako na Roho yako ni matusi tosha kwa nafsi yako kila jua linapochomoza.
Shame on you! Pathetic Creature.
 
...mbwa nyie...hii nchi si yenu....ukabila mnaojenga iko siku utawatokea puani...wauwaji Na watesaji nyie...dogs....
Kwanza, sijawahi kuwa mbwa na haitatokea hata siku moja. Kwa sababu mimi ni binadamu Mwenye hekima na busara ya kuweza kuwavumilia viumbe kama wewe ambao mnatukana na kukejeli watu kwenye mitandao bila sababu za msingi. Utakuwa una matatizo makubwa sana ya kisaikolojia kufikia kumuita binadamu usiyemjua mbwa.

Pili, niweke hili wazi....mimi ni mzaliwa wa Kanda ya Kaskazini ni Mmasai to be exact. Kwa hiyo nawaelewa sana watu wa aina yako na kitabia, kimazingira, kiupeo n.k.
Usilazimishe mimi na wewe tuwe na fikra na mawazo sawa. Haitawezekana hata siku moja.

Tatu, wewe una Sumu ya Chuki na Ukabila ambayo inakutafuna kupita maelezo. Unahitaji msaada haraka sana, bila hivyo utaishia pabaya.
Endelea na matusi na kuniita majina yote, haitanisumbua kwa sababu inadhihirisha ya kwamba wewe sio Binadamu bali ni kiumbe (Creature). Na ulimwenguni kuna viumbe wa aina nyingi sana. Kwa hiyo nakutakia kila la kheri katika mapambano yako yaliyojaa chuki, ukabila na UZANDIKI. Ila utaishia pabaya sana. Mungu akusamehe.
 
Tukulinganisha kati ya mizigo ya Rwanda,DRC, Burundi, Zambia, Malawi na Uganda ni nani mwenye kubeba bandari ya dar kwa maana ya wingi wa mizigo. Tunaweza kuziorodhesha nchi ya kwanza mpaka ya mwisho
 
Watavamia kila sehemu ila wajue mapato haya anguki kutoka mbinguni yanapandwa na kutiliwa mbolea kukua na kunawiri
 
...kumbe inakuuma eh....idiot..ukabila Na chuki umeleta we ulipoanza kuchambua jina mtu hapa....siku nyingine jifunze kuchangia mada...achana na ukabila....maana mmepandikizwa chuki ya ukabila....na mmekua vipofu.....kenge wa kimasai we...changia hoja ya kwanini hela mnakusanya kila kona lakini hazitoshi!!...Na mnapoambiwa mnatumia hovyo hela zetu mnabaki kuuwa watu.....

Kwanza, sijawahi kuwa mbwa na haitatokea hata siku moja. Kwa sababu mimi ni binadamu Mwenye hekima na busara ya kuweza kuwavumilia viumbe kama wewe ambao mnatukana na kukejeli watu kwenye mitandao bila sababu za msingi. Utakuwa una matatizo makubwa sana ya kisaikolojia kufikia kumuita binadamu usiyemjua mbwa.

Pili, niweke hili wazi....mimi ni mzaliwa wa Kanda ya Kaskazini ni Mmasai to be exact. Kwa hiyo nawaelewa sana watu wa aina yako na kitabia, kimazingira, kiupeo n.k.
Usilazimishe mimi na wewe tuwe na fikra na mawazo sawa. Haitawezekana hata siku moja.

Tatu, wewe una Sumu ya Chuki na Ukabila ambayo inakutafuna kupita maelezo. Unahitaji msaada haraka sana, bila hivyo utaishia pabaya.
Endelea na matusi na kuniita majina yote, haitanisumbua kwa sababu inadhihirisha ya kwamba wewe sio Binadamu bali ni kiumbe (Creature). Na ulimwenguni kuna viumbe wa aina nyingi sana. Kwa hiyo nakutakia kila la kheri katika mapambano yako yaliyojaa chuki, ukabila na UZANDIKI. Ila utaishia pabaya sana. Mungu akusamehe.
 
Back
Top Bottom