kutokutoka jasho

Kiresua

JF-Expert Member
May 13, 2009
1,184
259
Wanajamii, pongezi kwa kazi za kila siku. jamani nina muda sasa karibu miaka 4, huwa sitoki jasho hata nikipanda milima wakati wa jua kali. natoka jasho jembamba ambalo hata tisheti hailowi.

Niliona poa tu lakin rafiki yangu akaniambia nina tatizo. lakini ajabu ni kwamba nikiwa kwenye chumba chenye joto, kama nikiwa dar wakati wa joto, huwa mpaka nachuruzika jasho. mfano nimefyeka sana leo lakin wapi bwana, jasho chamtoto. nakunywa maji hadi lita 2 kwa siku, ila si siku zote.


Naona maji yanaweza yasiwe sababu kwani sijampunguza kunywa maji.naombeni msaada wa kitabibu kama ni pore space zimeziba nazifumuaje.

Asanteni wajameni
 
Back
Top Bottom