Kutoka ITV: Mjadala kuhusu DOWANS; wachangiaji wataka maandamano nchi nzima

Sitta ndio chanzo cha haya matatizo yote ya Dowans, nani asiyejuwa hilo?


Samwel Sitta si ndiye aliyeshauri/amua kwamba mkataba uvunjwe? Alikuwa hajui sheria ama ilikuwa ubabe tu wa kisiasa? Hapa kwa kweli tusilaumu mahakama yetu inabidi Sitta awaelezee Watanzania ilikuwa aamuru mkataba uvunjwe? Alikuwa ana backing gani ya kisheria hadi kuamuru mkataba wa kisheria kuvunjwa? Watu wanshindwa kuelewa kitu kimoja kwamba tatizo lilikuwa kwenye procurementt process ambayo ilifanywa na serikali/TANESCO Baad ya serikali kufanya procurement process na kumpata mzabuni waliyemtaka ndipo Richmond/DOWANS waliingia mkataba. Kwa hiyo mkataba ulioingiwa ulikuwa halali na walitakiwa kuwajibishwa ni wale waliofanya hayo manunuzi.
 
Wanaharakati wawasha moto malipo ya Dowans
Send to a friend
Friday, 07 October 2011 19:45


Elias Msuya
WANAHARAKATI wa masuala ya sheria na utawala bora, wameanza mkakati wa kuwahamasisha wananchi kuandamana ili kuishinikiza Serikali kuchukua hatua dhidi ya wahusika waliosababisha nchi kuingia mkataba wa kufua umeme wa dharura na Kampuni ya Richmond ambayo baadaye ilirithisha kazi zake kwa Kampuni ya Dowans.

Hatua ya za wanaharakati hao imetokana na uamuzi uliotolewa hivi karibuni na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kuridhia ya malipo ya fidia ya takriban Sh111bilioni kwa Dowans baada ya kusajili tuzo iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC).

Kutokana na uamuzi huo, Tanesco inatakiwa kuilipa Dowans kiasi hicho cha fedha badala ya Sh94 bilioni za awali kutokana na kuongezeka kwa riba ya asilimia 7.5.

Wakizungumza katika Kipindi cha Malumbano ya Hoja kinachoendeshwa na Kituo cha Televisheni cha ITV juzi usiku, wanaharakati hao kwa nyakati tofauti walisema kuna kila dalili kwamba baadhi ya watendaji serikalini walikula njama za kuwezesha kampuni hiyo kulipwa mabilioni hayo ya fedha.

Kutokana na hali hiyo, walipendekeza kwa Watanzania kufanya maandamano ya kushinikiza malipo hayo yasifanyike hadi hapo wahusika waliosaini mkataba huo ulilisababishia nchi hasara kubwa watakapokamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Ofisa mwandamizi kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia ambaye amekuwa akifuatilia kesi hiyo kwa muda mrefu, alisema Serikali ilizembea mahakamani akidai kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali hakupeleka pendekezo lolote la kuipinga kesi hiyo japo alikuwa akifika mahakamani.

"Mimi nilikuwa nikihudhuria kesi ile, Mwanasheria Mkuu hakuwahi kuleta pendekezo la kupinga kesi ile na hii inatokana na jinsi mkataba wenyewe ulivyo, hauruhusu suala hilo kushughulikiwa mahakamani," alisema Sungusia.

Alisema wakati Serikali ikisaini mkataba na Richmond iliweka vipengele ambavyo vinazuia masuala ya kimkataba baina ya pande husika kupelekwa nje ya ICC na kwamba hata kuwekwa kwa pingamizi kulikofanywa na Serikali kilikuwa ni kiini macho.

"Pande mbili hizi ni kama zilikuwa zimekubaliana, wanachokifanya wanakijua, hakuna jinsi wanavyoweza kutengua uamuzi wa ICC, kwa hiyo kwamba eti kulikuwa na pingamizi la Serikali tuzo isitolewe ni jambo ambalo lisingewezekana," alisema Sungusia.

Alisema katika mazingira hayo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), lisingeweza kufanikiwa na kwamba hata hukumu ya Mahakama imeweka wazi kuhusu suala hilo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananilea Nkya alisema Serikali ambayo ni mlinzi wa mali za wananchi ilishindwa kutekeleza wajibu wake na kwamba waliosaini mkataba huo lazima wachukuliwe hatua.

"Sasa katika hili tunaposema tunalipa fedha sijui tunamlipa nani, haiwezekani nadhani hapa kuna tatizo kubwa. La kufanya hapa ni Watanzania kuchukua hatua, tuingie barabarani kwa amani. Kila mtu ajitokeze tuandamane, halafu hao wamiliki wa Dowans wajitokeze mbele yetu ili watuambie wanachotudai."

Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya Utawala bora, Haki za Binadamu na Maendeleo (AFDF), Renatus Mkinga alisema
kwa kuwa wahusika wa ‘madudu' ya mkataba huo wanafahamika, wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria badala ya kuendeleza malumbano ambayo hayana tija na Serikali isikae kimya kuhusu suala hilo.

Alisema Kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond ilitembelea Texas, Marekani na kubaini kuwa hakukuwa na tawi la kampuni hiyo kama ilivyokuwa ikidaiwa na kwamba hata hapa nchini ilikuwa na kiofisi kidogo hivyo taarifa hiyo inaweza kutumika kubaini wahusika.



 
hawa wanaharakati waache kiherehere..........jaji mmoja siyo mwenye uamuzi wa mwisho.....................waende appeals court wakibwagwa huko na hawa mafisadi basi maandamano yatakuwa mwafaka................ushauri wangu wa bwerere ni kuwa ........exhaust the court process please................do not become weary............be patient and I am smelling the victory to the victors...........
 

achana na mkinga ongelea hoja Dowans.
 

Mahakama inatekeleza wajibu wake wa kisheria. Haimaanishi kuwa haki imetendeka!!! Mfano mimi naweza kukuibia wewe lakini nikaweka mwanasheria akaishawishi mahakama kuwa mimi sijakuibia na kisheria ikawa sawa, mahakama ikaniachia huru. Hapo mahakama inakuwa imetekeleza wajibu wake, lakini haki haijatendeka!!
 
wakifanya hivyo waarabu mnawaita magaidi, hiyo ndio demokrasia na uana mapinduzi wa kweli anglia che guavara alovyouawa kwa kupigania haki na demokrasia, hakusita kuua aisee, hapa nimalizie, hakuna cha maandamano wala kupinga ni lazima dowans walipwe hakuna wa kuwazuia, andamana uone nini maana ya 'fanya fyoko uone'. Mi siandamani...
 
Hapo uwa ndo nashindwa kuelewa vizuri na kubaki na conclusive remark kuwa huu ni wizi halali. Hivi Tanesco au serikali iliingia mkataba na nani?
Kama ni Richmond je mbona tume ilisema hakuna kitu kama richmond! Na je hiyo Dowans iliingia na nani kwenye mkataba? Kama iliingia na Richmond je inakuaje inaishitaki serikali?Je wakati richmond na anamuuzia dowans serikali iliusishwa au vipi?
Richmond yawezekana imetengenezwa na hackers na con man kwani haya tumeyaona nchi nyingine ingawa wananchi wa nchi hizo walikuwa wepesi kukemea wizi huo.
 
Ndugu zangu deni lazima litalipwa tu,hata kama haki ipo upande wetu lakini tumeshindwa kisheria kutokana na mkataba wa kimangungo waliosaini viongozi wetu. Muhimu sisi kama wenye nchi tuwawajibishe waliosaini mkataba huu,na hawa akina Sita na Mwakyembe ambao walishupalia Tanesco ivunje mkataba,na sasa tunaishia kulipa fidia ya bilioni 111. Sita na Mwakyembe ni wanasheria,wangekua watu wa mwanzo kujua kwamba kuuvunja mkataba huo kihuni ingesababisha tushitakiwe na tulipishwe fidia kubwa.
 
Tatizo la sisi wabongo ni moja, tunapenda kuongea Sanaa ! Jamani hivi mnajua Nasir tuko saw na viongozi wetu ? Mnajua tunapenda kulalamika ka viongozi wetu??
Hebu tuamke muda wa kuongea umekwisha. Mid napendekeza tr 15/10 kuna mmoja amepedekeza tr14 binafsi sikuipendelea ma'am ni siku ya kumkumbuka mpigaji wetu Nyerere so tutaiharibu siku hiyo na kuiwekea doa, na nawakumbusha kidogo mliowaoga kuharibu nchi kimataifa kwa kugoma kulipa ha Nyerer aliwahi kugoma kulipa Madeni aliokopa nje na akawambia hizo hela wasingekuwa nazo bila kuwaibia waafrika na hakulipo wakamsamehe wenyewe sembuse Hawaii wezi? Kwa hili tutautangazia ulimwengu Kuwa tz wamechoka kuibiwa. Maana tumeibiwa kwa kificho sasa imeanza wazi wazi na kwa kulazimisha.pls TZ amkeni
 

Mkuu kwa hili hata hakimu wa gachacha za Rwanda ataipa tu ushindi DOWANS. Viongozi wetu walishafanya makosa na sasa kitanzi kiko shingoni mwa Watanzania. Hata tukiandamana tutalipa tu labda hao mafisadi watuonee huruma tena kwa huruma yao.
 
Kanifurahisha sana yule mama na hitimisho lake, hayo maandamano ya amani ndo yafanyike haraka iwezekanavyo
tena natamani hizo taasisi zisizo za kiserikali
na vyama vya siasa vishuhurikie suala hili nw tushachoka kufanywa kichwa cha mwendawazimu,
AMA KWELI KUHUSU DOWANS
MWIZI NA MLINZI WAMESHIRIKI KUMUIBIA MWENYE MALI
WENYE MALI WENYEWE NDO SISI WA TZ
 
Jamani nayasubiri hayo maandamani kwa hamu lol!! Nadhani sehemu ya kufanyia mkutano wetu itakuwa viwanja vya Ikulu,ili nasi tuonje harufu ya Ikulu kidogo ha ha ha ha ha!!!
 

Sawa mama Rostam tutawalipa,mimi nimekuelewa sijui watanzania wenzangu....mzee yuko wapi siku hizi? maana hapatikani kabisa bongo kwasasa....
 
Jamani eeeh hapa ni kukomaa kiume,mtu na mtu kivuli na kivuli tuimwage CCM ya mafisadi kwa tank la sivyo watatunyonya mpaka tukonde,HATA UKITISHWA KUFA LEO JUA YA KWAMBA LAZIMA UTAKUFA TU,NA HAO WANAOKUTISHA NAO WATAKUFA TU,alikufa YESU sembuse sisi?
 
Jamani nayasubiri hayo maandamani kwa hamu lol!! Nadhani sehemu ya kufanyia mkutano wetu itakuwa viwanja vya Ikulu,ili nasi tuonje harufu ya Ikulu kidogo ha ha ha ha ha!!!

maandamano yataanzia apa Jf na kuishia facebook.
 

Mkuu unavunja kidogo...plz may you try to check on those red bolded words...Are you taking about she or he? Plz help!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…