Kutoa hela UTT changamoto CRDB

Hapana, liquid fund raha yake ni kuona salio linakua kila siku, na uwezo wa kutoa hela ndani ya siku tatu za kazi basi. Riba zinafanana hiyo mifuko miwili
Ok nimeona nao interest yao pia ni 12%
 
Kwa hiyo hizo za BOT ni mpaka watangaze, huwezi kwenda kujinunulia siku ukiwa na pesa?
Ingia Instagram, tafuta namba ya Solomon Brokers. Wao ni mawakala wa stock market na UTT watakua na majibu ya maswali yako yote. Ukitaja tu jina la kampuni kuna watu huwa wanahisi labda ni tangazo la biashara, kama ni mtu wa kujituma basi hutakuwa na maswali tena. Tafuta any broker, piga simu na utapata msaada.
 
Mkuu hebu dadavua zaidi, nasikia inategemea na kiasi cha fedha unachohitaji kutoa. Kama ni kikubwa wanakusumbua ukate tamaa
 
Pesa za utt hazitoki. Nini kinaendekea wakuuu..au tumepigwa
 
Dunia ya leo mkuu bado unajaza fomu? Kwanini usiwe na app?? Ni rahisi zaidi na hakuna kulipa 23k
 
Ukisema hazitoki unamaanisha nini??
Kwanza app yao haifanyi kazi.. customer care hawapikei simu au wakipokea wanasema tusubiri.. Kifupi hawapo hewani saivi .. ni zaidi ya mwezi nilitakiwa kupewa pesa pia na jamaa wengine wawili wanasema ni mzunguko huu huu..
 
Kama uko mkoa ambao una ofisi, nenda. Lakini nimekua nikifanya transactions kwenye mfumo na inakubali fresh tu.
Mkuu last time kufanya ni lini.. kwa kua hata app haifanyi kazi.. walisema wana update kwa kuleta app mpya toka hapo nikiwauliza wanasema app haipo tayari mpaka iwe tayari ndo watatujuza na transaction hazifanyiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…