Kutoa Factory Reset Protection (FRP) bila kompyuta

Ramlis

JF-Expert Member
Aug 22, 2013
597
494
Baada ya toleo la android lollipop na kuendelea kumewekwa security patch kwenye simu za android. Hii inafanya kazi pale utakapofanya hard reset kwenye simu iliyo na account ya google. Simu inapomaliza ku-reset ukaiwasha itaomba Wi-Fi na ukifanikiwa kuunganisha kwenye WI-FI itakuomba uingize anuani ya akaunti iliyokuwemo awali. Hapa ndo kuna kizazaa kama haukutunza kumbukumbu za anuani na neno la siri.

Njia hii ya ku-baypass bila kompyuta itahitaji vitu vifuatavyo:
1} Akaunti ya google iliyohai
2} Simu yoyote yenye uwezo wa kuunga hotspot na salio la kupiga ( na yenye app ya xender ''hii siyo muhimu kwani itafaa kama simu yenye frp ina Xender app ndani yake''), Kama una simu ya kawaida usijali pia.
3} Quick Shortcut Maker.Apk
4} Salio la internet kwenye simu nzima au yenye FRP

Hatua za kufuata ili kufanikisha zoezi letu :
1: Weka laini ya simu inayofanya kazi kwenye simu yenye FRP halafu iwashe

2: Ikiwaka iache laini isome ionyeshe mtandao baada ya hapo ipigie, usipokee bali gusa kuelekea kwenye icon ya sms, chagua sehemu iliyoandikwa "Write your own".

3: kwenye sehemu ya kuandika namba ya mpigaji kuna sehemu pameandikwa "call" au alama ya kupiga, bonyeza hapo itakupeleka kwenye sehemu pa kupigia simu. kama simu yako yenye FRP ina Xender ukiwa bado kwenye sehemu ya kupigia simu bonyeza sehemu ya majina, chagua jina mojawapo halafu share kwenye Xender, baada ya hapo Xender itafunguka. Katika simu nyingine fungua Xender halafu tuma file la Quick Shortcut Maker.Apk kwenye simu yenye FRP ikimaliza install.

4: Kama hauna simu yenye uwezo wa kuinstall Xender app au simu yenye FRP haina Xender ukifanikiwa kufika sehemu ya kupigia simu bonyeza *#*#4636#*#* itakupeleka kwenye "phone test" au ikikataa tafuta code no ya "phone test" itakayokubali kwenye simu yako.

5: Ukifanikiwa kufika kwenye ''Phone test" chagua Battery au Usage Statistics, ikifunguka upande wa juu kuna mshale wa kurudi nyuma, bonyeza kwenye huo mshale utakupeleka kwenye setting.

6: Kama simu yako ina Touchpal kama default keyboard hapa ni rahisi, utakapoiwasha simu yako ikifika sehemu ya kuunganisha na WI-FI bonyeza sehemu yenye option ya "add network" kama haipo washa hotspot kwenye simu nyingine, likionanekana jina la WI-FI bonyeza kuunganisha itatokea Touchpal keyboard, usiandike chochote nenda kwenye setting ya keyboard yako, kuna sehemu imeandikwa "Cloud" utaona sehem imeandikwa "login with google+ au facebook" bonyeza hapo, itakwambia kuwa hakuna network itakuomba uwashe mobile network ukibonyeza hapo itafungua setting.

7: Baada ya kufika kwenye setting unganisha simu yako kwenye internet, baada ya hapo nenda kwenye apps chagua browser yoyote, ukiichagua kwa kuibonyeza utaona sehemu imeandikwa "go to app au launch " ikifunguka ingia google tafuta Quick Shortcut Maker.Apk halafu install halafu ifungue (hii ni kwa wale wasio na Xender kwenye simu zao).

8: Baada ya kuifungua app kuna sehemu imeandikwa "Imput Keyword to filter" hapo andika neno "Google Account Manager" itakokea halafu expand hapo utaona option nyingi ndani ya google account manager angalia kwa umakini utaona sehemu yenye maandishai "Google Account Manager" chini yake imeandikwa "Type Email and Password", chagua hapo ikifunguka bonyeza "try" itakuletea sehemu ya kuandika password usiandike chochote. Kwa juu utaona sehemu ya vidoti vitatu au sehemu ya chini ya simu yako ya option, bonyeza hapo utaona "Browser Sign-in" baada ya kuchagua utaona sehemu ya kuandika email yako kama ni valid itakuja sehemu ya kuandika password. Baada ya ku-verify akaunti yako itarudi sehem ya awali, ondoa shaka izime simu halafu iwashe

8.1: Kama kwenye google account manager hautapata sehemu ya kuandika email na password jaribu kudownload Google Account Manager.Apk kulingana na toleo la OS ya simu yako na install harafu jaribu tena.

Mwisho:
Siyo simu zote zinazokubali njia hii...... Kuna mbinu mbadala zinatumika ku-bypass.
 
Sasa mkuu kuna hizi cm tecno j8 Kuna mdaa apps Kama insta na whatsapp zina goma kufanya kazi na mb zipo za kutosha mpaka ni reset hii tokea baada mdaa apo shida uwaga nini
Sio tecno J8 tu, simu karibia zote za tecno zenye android lollipop na baadhi ya marshmallow zina bugs, baadhi wametoa update ya kufix bugs hata hiyo J8 wametoa update. Jaribu kufanya update simu hiyo tatizo litaisha. Kama hauna network yenye nguvu ni nadra kupata OTA update.

*********
UPDATE.

Ikitokea baadhi ya apps hazikonect kwenye internet wakati una kifurushi katika simu za tecno fanya hivi, fungua app ya hi manager katika simu yako, Nenda Data traffic management >Network management, weka vema kwenye kiboksi mbele ya all online apps.
 
Frp kwa simu zote za W3 zinatoka kwa njia ya kompyuta tu.
 
Asante kijana, tecno hizi zina shida sana
J8
W3
Wx3 yan kuna access ya internet lakin wasap inazingua sana
 
Back
Top Bottom