Jinsi ya kuondoa password kwenye iphone! !

Jinsi ya kuondoa password kwenye iphone! !

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
1,285
Reaction score
2,595
Je umechoka Kila mara kuweka password kwenye iphone yako pale unapotumia kwenye app store ?? Yani Kila unapotaka kupakua kitu app store inakudai password [emoji360] kuweka.

IMG_20231112_121742_089.jpg


Okay kampuni ya apple wameweka huo mfumo kwa watumiaji wa simu za iphone ili kuongeza usalama wa watu kupakua pakua Kila program na kuweka kwenye simu bila muhusika kujua.

Kuna option mbili uwa zinatokeaga ambazo ni,
  • always required, hii ni Kila Mara unapotaka kupakua app ya kulipia au yoyote inakuhitaji uweke password
  • Required after 15 minutes, hii itakuomba uweke password Kila baada ya dakika 15 pale unapotaka kupakua kitu kwenye app store hivyo ukiweka mara Moja haitakudai password mpaka baada ya dakika 15 kupita.

Lakini Apple wameweka option ya kuondoa huo mfumo ikiwa mtu hataki Kila mara kuweka password unapotaka kupakua kitu kwenye app store.

View attachment 2811372

Fanya hivi kuondoa password [emoji116]
[emoji362] Ingia setting kwenye iphone yako
[emoji362] Gusa kwenye email yako Jina lako
[emoji362] Gusa Sehemu ya Media & purchase
[emoji362] Gusa Sehemu ya Password chini utaona neno free download gusa Sehemu ya require password
[emoji362] Weka password zako utaweza off.

Ikitokea unaingia kwenye app store kupakua kitu haitaweza tena kukudai password [emoji736]
 
Back
Top Bottom