Kutengeneza habari potofu kunaweza kukuweka matatizoni kisheria na kijamii

UTENGENEZAJI_WA_HABARI_FEKI_NI_KINYUME_CHA_SHERIA_ZA_NCHI_MBALIMBALI.jpg


Utengenezaji wa taarifa potofu unapingwa katika nchi mbalimbali. Baadhi ya watu katika jamii nyingi wamejikuta matatizoni kwa kuingia vifungoni au kulazimika kulipa fidia kwa sababu ya kutoa taarifa potofu kuhusu watu, kampuni na taasisi mbalimbali.

Tanzania, kama nchi nyingine, ina sheria zinazodhibiti uzalishaji na usambazaji wa habari feki au za uongo. Sheria zinaweza kutofautiana kidogo kulingana na nchi, lakini lengo ni kudhibiti habari ambazo zinaweza kuleta madhara kijamii, kisiasa, au kisheria.

Kwa mfano, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kifungu cha 16 nchini Tanzania inadhibiti matumizi mabaya ya teknolojia ya habari na mawasiliano. Sheria hii inaweza kutumika kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya watu wanaotengeneza na kusambaza habari za uongo kwenye mitandao au njia nyingine za mawasiliano.

Kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ya mwaka 2015 kinasema mu yeyote ambaye anaandika na kuchapisha taarifa au data zilizo katika picha, maandishi, alama au aina nyingine yoyote kwenye mfumo wa kompyuta akiwa anajua kuwa taarifa au data hizo ni za uongo, zenye kudanganya, kufanya hila au hazina ukweli, na kwa nia ya kumchafulia mtu sifa, kumtishia, kumkashifu, au kwa njia nyingine yoyote kudanganya au kudanganya umma au kusaidia kufanya kosa, anatenda kosa, na akithibitishwa kosa hilo, atakuwa na hatia na adhabu yake ni faini isiyopungua shilingi milioni tano au kifungo cha miaka mitatu au vyote pamoja.

Pia, Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 Kifungu cha 50 cha Sheria hii kinaeleza makosa na adhabu kwa kuchapisha habari kwa makusudi, uzembe, ya kutungwa na ya uongo, yenye nia ovu au ya kutungwa na ya uongo; au taarifa iliyokatazwa inayoweza kuhatarisha maslahi ya jamii, na hadhi, haki au uhuru wa watu wengine. Makosa mengine ni pamoja na kuendesha chombo cha habari bila ya kuwa na leseni, kufanya kazi ya uandishi wa habari bila ya kuthibitishwa na mamlaka husika, au kusambaza taarifa za uongo na zisizothibitishwa.

Kulingana na sheria hizi, ukibainika kutengeneza au kusambaza habari feki, unaweza kukabiliwa na mashtaka ya kutoa taarifa za uongo au kuvuruga amani na usalama. Hii inaweza kusababisha adhabu kali ikiwa ni pamoja na faini kubwa au hata kifungo gerezani.

Kwahiyo, ni muhimu kuzingatia kwamba kutengeneza au kusambaza habari feki ni kosa la kisheria na linaweza kusababisha matatizo makubwa ya kisheria. Ni muhimu kuhakikisha kwamba habari unazotengeneza au kusambaza ni za kweli na zenye uhakika ili kuepuka kukiuka sheria na kuepuka madhara kwa wewe na kwa jamii.
 
"Ukifanya wanayofanya serikali unafungwa"
Wanaongeaga uongo mwingi wazi wazi na hawafungwi
Rejea March 2021
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom