Kusitishwa mnada wa mitambo mgodi wa Buzwagi: Serikali imepanic?

Sheria mpya ya madini ya Prof. Kabudi ni kaburi la sekta ya madini. Hakuna atakayefanya uchimbaji wa madini ya Tanzania.

GGM wameomba mazungumzo na serikali. Wasipokubaliana, bila shaka watafuata njia hiyo hiyo ua Acacia

Waliokuwa wanajenga mgodi wa graphite Mtwara, wamefunga.

Waliokuwa wanataka kuanza kuchimba gas, wamefunga na kwenda Mozambique. Tumepoteza uwekezaji wa dola bilioni 30.

Makampuni ya nje yaliyokuwa yanafanya utafiti wa madini mbalimbali, yote yamefunga. Mengine yameondoka kabisa, machache yamesimamisha tafiti na kubakiza watendaji wachache sana kwenye ofisi zao kwaajili ya kusimamia taratibu za kufunga kampuni.

Ile sheria ya Prof. Kabudi haipo mahali popote Duniani. Kuamini kuwa sisi ndiyo wajanja kuwazidi wote, huenda sisi ndiyo tukawa wajinga kuliko wote.

Umesahau Dangote
 
wakati wanauchukia 2009 lifespan kwa mujibu wa watafiti exploration za madini na data kuuhusu ilikuwa ni miaka 10.
Sasa kufunga mining na kumalizia hicho kilichobaki hadi 2019 mwishoni kitaaluma yao wako sahihi.
lkn nilisikia walikuwa na uwezo wa kuendelea, lkn utafiti ambao majibu yalitoka kabla ya ishu za makinikia waliona ni gharama zaidi kuanza kuchimba sehemu mpya (pit mpya) kuliko kufunga.
hapa naona kosa lao ni kama utaratibu wa auction haukuhusisha serikali na kama kulikuwa na ulazima wa kufNya hivyo kwa mujibu wa sheria zetu.

Nyinyi ndiyo mliyosema Mwadui imekauka. Mko tooooo academic

Kwa taarifa yako, GGM ilianza na lifespan ya miaka 8, leo wako mwaka wa 18 na bado wanauwezo wa kuwepo hata baada ya miaka 100
 
Wapendwa tuache mihemuko katika haya mambo ..NCHI HUENDESHWA KWA UTARATIBU ,KANUNI,SHERIA PIA
KUNA MKATABA KATI YA PANDE MBILI NA MKATABA UKO WAZI NINI CHA KUFANYIKA MNAPOFIKIA MWISHO WAKE AIDHA KWA KUMALIZA MALENGO YALIYOKUSUDIWA AMA ....VINGINEVYO..
Ni dharau na utovu wa nidhamu kuamua kufunga mkataba bila kuwasiliana na mliyeingia naye MKATABA
"THIS IS THE COUNTRY AND AM IN FULL SUPPORT OF THE PERMANENT SECRETARY "
Any contract is subject to Breach of the same!

Acacia has decided,full stop!

Your boss should seek for remedies (if any).
 
Mkuu kubaliana na mimi kuwa utaratibu unaoutetea is a petty issue.
Kubwa ni kushindwa kuelewana na hawa watu ili tuwe na a win win situation.
Kutofuata policy ni “petty issue”!!!
Wewe hauoni umuhimu wowote wa “policy”?
Na ipo ndio issue kwako?

Kama kampuni inakuwa hata haifuati policy unategemea ndio watakwambia ukweli kilichoko kwenye makontena??
 
Raha sana hii nchi!

Kwa wafuatiliaji wa sekta ya madini walishafahamu suala la kukaribia kufungwa Buzwagi hata kabla ya Sakata la Makinikia!

Na baadhi ya wafanyakazi wa Buzwagi wamesharudi home for at least 2 months now!

Na hata Bulyanhulu inafahamika imebaki miaka michache tu kufungwa!

Sasa ikiwa mimi kijana wa Tandika nisiye kwenye mfumo rasmi nayafahamu yote haya; how come watu wa serikalini wasifahamu?!
Na kibaya zaidi nguvu/gharama inayotumika kulinda haya makinikia huku bandari itakuja kuwa kubwa kuliko hata thamani ya makinikia yenyewe

- Nguvu nyiiingi akili ndogo
 
Tuna nini cha kuonyesha au kujivunia kilichopatikana kutokana na hiyo migodi kwa miaka yote. Vitu vinavyonekana Kwa macho na sio ngonjera za watu wamepata ajira.mfano tukasema Barabara hii Dar-salaam mpaka Mwanza imejengwa kutokana Fedha za migodi.
 
wakati wanauchukia 2009 lifespan kwa mujibu wa watafiti exploration za madini na data kuuhusu ilikuwa ni miaka 10.

Sasa kufunga mining na kumalizia hicho kilichobaki hadi 2019 mwishoni kitaaluma yao wako sahihi.

lkn nilisikia walikuwa na uwezo wa kuendelea, lkn utafiti ambao majibu yalitoka kabla ya ishu za makinikia waliona ni gharama zaidi kuanza kuchimba sehemu mpya (pit mpya) kuliko kufunga.

hapa naona kosa lao ni kama utaratibu wa auction haukuhusisha serikali na kama kulikuwa na ulazima wa kufNya hivyo kwa mujibu wa sheria zetu.
You talk like Economist or at least Mining Economist!

You're right! Unajua watu wakisikia mgodi unafungwa; wanadhani madini yanakuwa ndo yameshaisha! Kumbe madini yanaweza kuwa bado yapo lakini yakawa not economically and commercially viable for further extraction!! Ni sawa sawa na unapomwingiza sokoni kuku wa mayai! Sio kwamba anakuwa amekoma kutaga bali gharama za kuendelea kumtunza huyu kuku ni kubwa kuliko idadi ya mayai anayotaga over a given time!

So, ningemshauri The Stig ajiongeze kupitia hayo maelezo yako manake naona ni kama atatuletea Case Studies za Geology or Mining Classes!!
 
Kwa kuanzia, wengi wetu wafuatiliaji masuala ya uchumi, tulisituka kuona kwenye luninga na vyombo vingine vya habari juu ya mnada wa mitambo ya uzalishaji mgodini Buzwagi.

Tulisituka kwani maana yake ni uzalishaji kusimama, wananchi kukosa kazi, mapato ya aina yoyote yaliyokuwepo kupotea kabisa.
Kwa maana ya maendeleo hii ni hataua mbili nyuma.

Tunajua kuna mgogoro kati ya Serikali na wanaoendesha mgodi huo kwa muda sasa, lakini hii ndo dalili ya wazi kuwa hakuna muafaka.
Tunajua kuwa kutokana na biashara ya mgodi huo, kuna kodi na madeni mengi yanayoikabili kampuni mama ya Buzwagi ambayo inaitwa Barrick.
Buzwagi (Barrick) wamebwaga manyanga, wanaondoka.

Sasa cha kushangaza, leo gazetini Mwananchi pg 5.
"Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila alisema Buzwagi walitoa tangazo la mnada bila kuwasiliana na Serikali, jambo ambalo ni kinyume na taratibu.
"Tofauti na sekta nyingine, Profesa Msanjila alibainisha utaratibu wa kufunga mgodi wowote nchini kwamba lazima waendeshaji watoe taarifa Serikalini kwa kueleza sababu za kufanya hivyo".

Hapo ndo ninapo changanyikiwa.
Serikali haijui kwa nini mgodi unafungwa!!!

Na habari zilizopo(Mwananchi) ni kwamba watu toka Dubai,Congo DRC, Oman wamejitokeza kununua hivyo vifaa.

Ushauri wangu tu, sekta ya madini ni very sensitive kwa vile ina heavy investments. Tusieendeshe kwa Trial an Error.
Mpayukaji anaua kabisa uhai wa taifa,
 
Migodi inachimbwa na Mining Companies, na siyo na serikali. Hata magari yanaundwa na makampuni ya magari na siyo na serikali. Shida yenu mkishaona udongo, mnafikiri kilaza yeyote anaweza kuchimba migodi.

Kuwaambia serikali iende ikachimbe mgodi umeenda kilomita 5 ardhini, ni sawa na kuwatakia kifo hao wafanyakazi wataohusika. Wachmimbaji watakuwa wanakufa kila siku huko chini wakisubiri dokezo la kuwasha generator lisainiwe na accounting officer. Na hata huwo uuzaji wa dhahabu utakuwa ni kama ule wa kuuza machungwa gengeni, wakati dhahabu inauzwa kitofauti kabisa, ikihusisha hedge books, derivatives na kila aina ya futures trading

Accacia wanaondoka Tanzania badala ya kubaki miaka 120 kwa sababu tumeshindwa kuweka mazingira yanayotabirika kuhusu uwekezaji. Kushindwa kufanya hivyo kunasababisha wanahisa waogope kabisa kuwekeza Tanzania, hata kama kuna utajiri wa kiasi gani
Jomba vp; mbona unaji-quote mwenyewe?! Unamjibu nani hasa kupitia hii post yako?!

Nakumbuka kwenye post niliyokuwa nimekujibu hapo kabla, nami nilizungumzia suala la serikali kutwaa huo mgodi!

Therefore, kama post hii unalenga kunijibu mimi, basi ningekushauri usiwe unakurupuka kujibu bila kufahamu context ya maelezo yangu!!

Maelezo yangu kwenye post ile yalikuwa presented in a gentleman way of telling you ni namna gani maelezo yako yalivyokuwa too schoolish... like referring some Mining/Geology Class Case Studies!!

Sorry Dude!
 
Migodi inachimbwa na Mining Companies, na siyo na serikali. Hata magari yanaundwa na makampuni ya magari na siyo na serikali. Shida yenu mkishaona udongo, mnafikiri kilaza yeyote anaweza kuchimba migodi.

Kuwaambia serikali iende ikachimbe mgodi umeenda kilomita 5 ardhini, ni sawa na kuwatakia kifo hao wafanyakazi wataohusika. Wachmimbaji watakuwa wanakufa kila siku huko chini wakisubiri dokezo la kuwasha generator lisainiwe na accounting officer. Na hata huwo uuzaji wa dhahabu utakuwa ni kama ule wa kuuza machungwa gengeni, wakati dhahabu inauzwa kitofauti kabisa, ikihusisha hedge books, derivatives na kila aina ya futures trading

Accacia wanaondoka Tanzania badala ya kubaki miaka 120 kwa sababu tumeshindwa kuweka mazingira yanayotabirika kuhusu uwekezaji. Kushindwa kufanya hivyo kunasababisha wanahisa waogope kabisa kuwekeza Tanzania, hata kama kuna utajiri wa kiasi gani
Umenichekesha sana ndg. Kwamba sahihi ya kuwasha generator kutoka kwa officer
 
Sheria mpya ya madini ya Prof. Kabudi ni kaburi la sekta ya madini. Hakuna atakayefanya uchimbaji wa madini ya Tanzania.

GGM wameomba mazungumzo na serikali. Wasipokubaliana, bila shaka watafuata njia hiyo hiyo ua Acacia

Waliokuwa wanajenga mgodi wa graphite Mtwara, wamefunga.

Waliokuwa wanataka kuanza kuchimba gas, wamefunga na kwenda Mozambique. Tumepoteza uwekezaji wa dola bilioni 30.

Makampuni ya nje yaliyokuwa yanafanya utafiti wa madini mbalimbali, yote yamefunga. Mengine yameondoka kabisa, machache yamesimamisha tafiti na kubakiza watendaji wachache sana kwenye ofisi zao kwaajili ya kusimamia taratibu za kufunga kampuni.

Ile sheria ya Prof. Kabudi haipo mahali popote Duniani. Kuamini kuwa sisi ndiyo wajanja kuwazidi wote, huenda sisi ndiyo tukawa wajinga kuliko wote.
Kwa wale wanaoishi in a fantasy world lazima wakuone sio mzalendo!! Uzalendo kwenye nchi hii hivi sasa ni kuishi in a fantasy, imaginary world!!

Hadi hii karne ya 21 usishangae wakatokea watu wakakuambia "acha tu waondoke; gas haiozi!"

Sometimes huwa najiuliza hivi hawa jamaa hawadhani kwamba kuna some "crazy scientists" outta there wanaokesha maabara kuangalia ni namna gani free air in the atmosphere can be chemically combined to forma fuel gas!!

Wanasahau tulikuwa tunatamba na katani lakini hivi sasa kuna mbadala wa katani!

Mwarabu anaringia mafuta kwa miongo kadhaa hivi sasa lakini nadhani hivi sasa pressure inapanda wanapoona kasi ya utengenezaji wa electrified cars!
 
Kwa wale wanaoishi in a fantasy world lazima wakuone sio mzalendo!! Uzalendo kwenye nchi hii hivi sasa ni kuishi in a fantasy, imaginary world!!

Hadi hii karne ya 21 usishangae wakatokea watu wakakuambia "acha tu waondoke; gas haiozi!"

Sometimes huwa najiuliza hivi hawa jamaa hawadhani kwamba kuna some "crazy scientists" outta there wanaokesha maabara kuangalia ni namna gani free air in the atmosphere can be chemically combined to forma fuel gas!!

Wanasahau tulikuwa tunatamba na katani lakini hivi sasa kuna mbadala wa katani!

Mwarabu anaringia mafuta kwa miongo kadhaa hivi sasa lakini nadhani hivi sasa pressure inapanda wanapoona kasi ya utengenezaji wa electrified cars!

Watu hawajui kwamba hao jamaa wanaweza hata kuresearch namna ya kuichukua hiyo dhahabu huko chini wakiwa wamebaki huko waliko na sisi tukaendelea na shughuli zetu juu huku tukisubiri tupate akili na siku akili ikija huko chini unakuta kweupe na reserve yoote iko kwao ...

Kweli akili ni nywele.
 
Life span ya huo Mgodi inaisha 2020, na kwa sasa shughuli zote za uchimbaji shimoni zimesitishwa sambamba na punguzo la watu wengi mwaka jana december, Machine chache ndio zimeachwa hasa zile zenye hali nzuri kwa ajili ya kulisha crusher na kwa kutumia akiba ya mchanga ulioachwa mpaka 2020. Ni kawaida kwa Migodi kuuza mali zake hasa pale Mgodi unapokaribia kufungwa au unapokuwa umeamua kubadilisha aina ya Fleet zake na system ya uchimaji labda kutoka open kwenda underground au kutoka undergound kwenda open..
ACACIA bado ni mmiliki wa huo Mgodi mpaka 2020 atakapoamua vinginevyo, ACACIA anamiliki migodi mingine kama Bulyanhulu na North mara, Bulyanhulu uchimbazji umesisimama kwa sababu za rehabilitation lakini hakuna shughuli inayoendelea shimoni na wafanyakazi wengi sana walipunguzwa mwaka jana.. Kwa sasa Mgodi wa North Mara chini ya ACACIA ndio uko kwenye full operation...

Serikali iwe makini na hii migodi maana kinachoonekana ACACIA haihitaji tena kuendelea kuwepo Tanzania na ipo kwenye mazungumzo na Wachina kuwauzia migodi yake yoote ya Tanzania, Umiliki wa hii Migodi chini ya Wachina ni hatari kuliko uwepo wa ACACIA na hapa Serikali ifanye uchunguzi wa kutosha na ikiwezekana iangalie uwezekano wa kuinfluence umiliki usiende kwa mchina.. Ni vizuri pia serikali iangalia uwezekano wa kuinunua na kutafuta mtu wa kumpa afanye operation na management ya hii Migodi with international standard kama migodi mingine yenyewe ikae kusubiri Gawio tu..
 
Na kibaya zaidi nguvu/gharama inayotumika kulinda haya makinikia huku bandari itakuja kuwa kubwa kuliko hata thamani ya makinikia yenyewe

- Nguvu nyiiingi akili ndogo
Pilipili kwenye kidonda!

Kuna cku hapa nilisema moja ya makosa ya JPM ni kutumia nguvu kwenye uchumi wakati ujenzi wa uchumi unahitaji akili!!

Moja ya maswali ambayo sijapata jibu ni nani hasa Wezi Wakubwa wa Tanzanite pale Merelani!

Nikaendelea kujiuliza hivi Wezi Wakubwa wa Tanzanite wanaweza kuzuiwa na ukuta au huu ukuta umelenga kuzuia vibaka wanaoiba mawe ya madini!

Nikajiuliza kama Tanzanite One wana syndicate ya wizi wa Tanzanite; ina maana walikuwa wanatumia vichochoro kutorosha Tanzanite ili ionekane kuwakomoa kwake ni kuwajengea ukuta!

Hadi sasa sijapata jibu na leo ndio mara yangu ya kwanza nahoji hadharani hili suala! Niliamua kufa nalo na tai shingoni kwa sababu sifahamu sawasawa mwizi aliyelengwa na ule ukuta ni yupi na Mwizi Mkuu pale Merelani ni nani... au generally, malengo ya ule ukuta ni yapi hasa!!
 
Kama sheria ndivyo inavyosema, kwanini wakiuke? Kufunga mgodi sio issue, issue ni kufuata sheria. Mwl. Nyerere aliwahi kusema dhahabu haiozi. Waache waende. Inaweza kuchimbwa tena hata baada ya miaka 100!
Technology inakuwa kila siku hiyo miaka 100 ijayo itakuwa imevumbuliwa vitu mbadala ya dhahabu na huenda dhahabu haitakuwa tena na soko kama ilivyonayo leo.
 
Au serikali inataka iwataifishe tuishie kupata hata hivyo vimagari vibovu VIPI GESI JAMANI? CHAMA NA WAGENI WANAJICHOTEA TU NINI MPK SASA
 
Back
Top Bottom