uungwana classic
JF-Expert Member
- Jun 9, 2014
- 2,324
- 2,079
Nliwahi kusingiziwa nkiwa darasa la tatu nlilia sana hase, ilikuwa siku yangu ya kwanza kufika shule hiyo nlihamia kutoka kijijini nlipokuwa naishi kwa bibi,asubuhi siku ya kwanza nlipelekwa na kaka yangu akaninunulia kalamu njiani maana tulihisi watakuwa wameshaanza kutumia kalamu ya wino, sa nne muda wa mapumziko nikiwa nimekaa kivulini nachorachora ili kujizoesha kutumia kalamu akaja jamaa moja ananiambia hiyo kalamu ni yake et nimeiba akaanza kuonesha na alama zake tena akanipeleka kwa mwalimu nlibisha sana mwisho alinizidi kiswahili ukiongeza na kutoka kijijini sikuwa na uwezo wakujieleza vizuri kufupisha story ikabidi nikubali kuwa nimeiba, na story ikaanza kusambaa kuwa yule mwanafunzi mgeni ni mwizi yaani siku ya kwanza kuja kashaiba kalamu hase iliniuma sana nlitamani kuacha shule nlimlaumu sana huyo mwalimu(apumzike kwa amani)nashukuru Mungu hiyo story haikudumu kwa sababu tulikuwa watoto na nlianza kutengeneza marafika kama kawaida tu ila iliniuma sana nachukia sana kusingiziwa yaani mwalimu anaweza nichapa hata fimbo kumi kwa kosa nlilofanya nisilie lakin fimbo moja au hata neno tu kwa kosa la kusingiziwa itanifanya nlie mpaka kichwa kiume, mpaka leo kama kosa nimefanya huwa nakuwa mdogo kuliko hata priton lakin ka sijafanya patachimbika