Kushukuru ni uungwana na kujali pia!

Kushukuru ni uungwana na kujali pia!

ubwabwa na pombe tuna Kula wapi ndio kilicho baki hii ni Sherehe yetu wote platnum sio mchezo ukiachana na ya diamond ya kizushi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]...
Poapoa
IMG-20191013-WA0123.jpeg
 
Usitusahau kwenye ufalme wako, na utuombee nasisi uliotuacha huku uwezo kufika huko platinum.
 
Huu ni mwaka wangu wa tisa hapa Jamvini. Kwahiyo naingia kwenye wakongwe wa kati wa JamiiForums.. Kama tukiamua kuvigawa vizazi vya JamiiForums basi tunaweza kufanya hivi kwa kipimo cha miaka kumi kumi

Kizazi cha kwanza 2000-2010.....
Hapo mnamo 2006 ndio JamiiForums ilizaliwa rasmi.. Hivyo kwa mpangilio wa vizazi.... Members wote wa kwanza mpaka 2010 hawa ndio kizazi cha kwanza cha JF... Pongezi nyingi kwao....

Kizazi cha pili 2011- 2020....
Hapa ndio nilipo mimi na wengine wengi sana... Sisi ni mapokeo ya kizazi anzilishi... Kizazi cha kwanza... Kwa jina lingine kizazi endelezi... Sura mpya nyingi na maboresho pamoja na mabadiliko mengi yamefanyika hapa... Pongezi kwa wote... Baada ya 2020 kitakuja kizazi cha tatu na cha nne na kuendelea....

Mfumo wa JamiiForums ni tofauti na mifumo ya mitandao mingine ya kijamii.. Hapa kuna mfumo wa kutambuliwa pia michango yako ndani ya forum hii.... Yani kuna madaraja kulingana na ukongwe pia... Mimi nilifikia daraja la SENIOR EXPERT MEMBER... yaani Mwanachama mkomavu mbobezi... Madaraja mengine ni junior member, member, na senior member (naweza kurekebishwa) madaraja haya ni bure.....

Aina nyingine ya madaraja ni yale ya kulipia yani kuna viwango tofauti vya tozo ambazo hukufanya upate daraja fulani... Haya sio ya bure... Na mojawapo ya madaraja hayo ni Gold member na platinum member... Nadhani ndio daraja la juu kabisa kwenye malipo

Wiki hii kuna mwanajamii mwenzetu bwana Mazigazi kwa kipekee kabisa aliguswa na mada na michango yangu hapa na kwa moyo wake mkuu wa upendo na bila shuruti akawiwa kuniombea kwa uongozi wa JamiiForums nipate daraja la PLATINUM bure bila kulipia.... Hisia zilikuwa tofauti kwenye hili toka kwa member wengine... Lakini alisimamia alichoamini

Kwa upendo wa dhati kabisa na kutoka moyoni... Uongozi uliridhia ombi la Mazigazi na nimetunukiwa rasmi daraja la PLATINUM Member bila kulipa chochote..

Nimefarijika sana na hili na napenda kuchukua nafasi hii kutoa shukrani za dhati kwa uongozi wa JamiiForums kupitia mwanzilishi wake Bwana Maxence Melo, Mazigazi aliyechagiza na kumshawishi pamoja na wana JF wote waliounga mkono na hata kupinga pia...

Nasema asanteni sana kwa heshima hii... Sitawaangusha....
CC : Maxence Melo, Paw, Invisible, Mhariri na moderators wote pamoja na wanajamii wote kwa ujumla wao... Itifaki imezingatiwa....

Jr[emoji769]
Mbona hili la maraja haliko wazi sana kwa members. Liko kama chaguzi za nchi hii.
Naomba liwekwe wazi. Yaani ni nini mtu afanye ili aingie daraja husika au ni sifa zipi za kuwa kuwa daraja fulani
Hongera kwa daraja ulilopewa ingawa hata wewe hujui maana ya kuwa huko 😂 😂 😂
 
Mbona hili la maraja haliko wazi sana kwa members. Liko kama chaguzi za nchi hii.
Naomba liwekwe wazi. Yaani ni nini mtu afanye ili aingie daraja husika au ni sifa zipi za kuwa kuwa daraja fulani
Hongera kwa daraja ulilopewa ingawa hata wewe hujui maana ya kuwa huko [emoji23] [emoji23] [emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kweli wewe ndiyo ulifanya nijiunge rasmi Jf ,mada zako zilikuwa zinanivutia sana ila siyo zile za ndumba😀😀,nilikuwa wakusoma tu napita....

Hongera sana bro Mshana.
 
Sema ukweli, uliwaroga hukuwaroga? Haiwezekani bwana, hivi hivi tu.
 
Back
Top Bottom