Kushindwa kwa Heche kuongoza BAVICHA

Kushindwa kwa Heche kuongoza BAVICHA

iron finger

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
358
Reaction score
221
Wakuu leo nakuja na mtazamo tofauti juu ya uwezo mdogo unaoonyeshwa na bwana Heche katika kusukuma mbele ajenda za chama na kuimarisha chama kupitia chombo hiki maalumu cha vijana ndani ya chama


Kwa mtazamo wangu Mh. Heche ameshindwa kuwa na ushawishi hasa zaidi kutumia na kuunganisha vijana wengi ambao wameonyesha matumaini na chama hasa wale walioko kwenye taasisi za vyuo na mashule.
Mh Heche amekuwa mtu wa kukaa ofisini tu na kutoa matamko mengi hasa yakiwa ya kwake binasfi na sio maoni ya vijana.

Mh Heche akili yake yote ipo kwenye kupambana na Mwita Mwikabe kwenye ubunge jimbo la Tarime na sio kusimamia baraza la vijana

Mh Heche kama kiongozi wa vijana asipo badilika na kutumika kwa maslahi ya chama na sio yake binafsi tutarajie BAVICHA dhaifu hasa katika kupambana na nguvu mpya ya CCM.

Nawasilisha
 
Mkuu tafuta kazi ya kufanya.Huu ujinga wa kuwa na ID feki zaidi ya kumi hautakusaidia wewe wala hilo kundi lako la kitapeli.
Mnachokijua ni kukimbilia Facebook kila siku na kuwatukana matusi ya nguoni viongozi wakuu wa CDM.Adui yenu mnayemjua ni Mbowe,Dr Slaa na Heche.Mbinu zenu kamwe hazitafanikiwa.
Umeona yale majungu uliyoleta dhidi ya Mbowe hapa jamvini umepuuzwa leo ukaibuka na majungu dhidi ya Heche na kesho utamuibukia Dr Slaa.Pole sana.
 
Mkuu tafuta kazi ya kufanya.Huu ujinga wa kuwa na ID feki zaidi ya kumi hautakusaidia wewe wala hilo kundi lako la kitapeli.
Mnachokijua ni kukimbilia Facebook kila siku na kuwatukana matusi ya nguoni viongozi wakuu wa CDM.Adui yenu mnayemjua ni Mbowe,Dr Slaa na Heche.Mbinu zenu kamwe hazitafanikiwa.
Umeona yale majungu uliyoleta dhidi ya Mbowe hapa jamvini umepuuzwa leo ukaibuka na majungu dhidi ya Heche na kesho utamuibukia Dr Slaa.Pole sana.

tatizo lenu mnaongozwa na mahaba binafsi juu ya chama hamtaki kuambia ukweli kwa halii hii ya kutopenda kuambiwa ukweli hatuwezi kuendelea
 
Mbona JK kashindwa kuongoza nchi hujamuwekea uzi wa kushindwa????? Acha ujuha wewe, huku ni kwa GT, vingivenyo kaa mbali na JF utaabika.
 
Kawadanganye ccm na siyo vijana tunaoona kazi inayofanywa na BAVICHA.
 
natoa maoni yangu kama mwanachadema heche yupo busy kutaka kumharibia mandevu mwita akili yake haiwazi zaidi ya ubunge

amekosa mbinu mbadala za kuimarisha bavicha
naikumbuka bavicha ya mh mnyika
 
Taingia Heche achaguliwe Bavicha kaishatoa matamko zaidi ya 20 ambayo hayana tija yeyote. Kimsingi Heche kashindwa kuwaongoza vijana.
 
tatizo lenu mnaongozwa na mahaba binafsi juu ya chama hamtaki kuambia ukweli kwa halii hii ya kutopenda kuambiwa ukweli hatuwezi kuendelea


wewe ndo una mahaba kama sio una bifu binafsi na Heche, tunamuona mara kwa mara heche anazunguka mikoani na anakusanya watu ambao hata raisi wako akienda mikao hiyo wafiki kiasi hicho, heche ana punch na anapangilia vizuri kuongea leo unasema Heche kashindwa.. we tuambie kashindwa nini.......watu kama ninyi sijui mnatokea wapi
 
Katika Viongozi ambao ninawaona sana kwenye ziara za kujenga chama na M4C ni Heche..! Sasa ninashangaa mleta uzi anasema Heche ni mtu wa kukaa oficini..! Unless kama kuna Heche wawili vinginevyo ninakubaliana na Kamanda Molemo kwamba mmekalia majungu wakati wenzenu wako busy kuleta mapinduzi ya fikra kwa wananchi wa Tanzania.. Hamna tofauti na walowezi wa Rhodesia ya zamani.. Cijui Albert Muzorewa wenu ni nani katika hilo kundi lenu la walowezi but tumewachoka..
 
Kama mleta mada angekuwa ni mwana Chadema wa kweli na ana mapenzi ya dhati na Chama chake, basi thread yake lazima ingekuwa kwamba Bawacha wameshindwa kuwashawishi Wanawake kuiunga mkono Chadema na Ivunjwe mara moja.

Lakini kwakuwa mleta mada anatumia tumbo kufikiri badala ya Ubongo amejifanya kipofu kwa kutokuona kwamba Bavicha iko strong chini ya Heche na Heche anafanya mikutano mingi Vijijini na siyo kukaa ofisini.

Ndio maana hamu ya kuwa Mwanachama wa chama cha siasa inanitoka maana siwezi kuvumilia kukaa na watu wenye njaa kama hawa meza moja. hawa ni wale ambao wamekosa fursa za ulaji CCM sasa wakadhani Chadema watapata fursa hizo matokeo yake ni kupiga filimbi za majungu tu.
 
wakuu leo nakuja na mtazamo tofauti juu ya uwezo mdogo unaoonyeshwa na bwana heche katika kusukuma mbele zajenda za chama na kuimarisha chama kupitia chombo hiki maalumu cha vijana ndani ya chama
unaupima vipi uwezo ama utendaji wa Heche?

kwa mtazamo wangu mh heche ameshindwa kuwa na ushawishi hasa zaidi kutumia na kuunganisha vijana wengi ambao wameonyesha matumaini na chama hasa wale walioko kwenye taasisi za vyuo na mashule
"kuwaunganisha" ki vipi? ama unaota!


mh heche amekuwa mtu wa kukaa ofisini tu na kutoa matamko mengi hasa yakiwa ya kwake binasfi na sio maoni ya vijanamh heche akili yake yote ipo kwenye kupambana na mwita mwikabe kwenye ubunge jimbo la tarime na sio kusimamia baraza la vijana
mpaka sasa kafanya ziara na mikutano mingapi? ok kashatoa matamko mangapi mpaka sasa? unaweza kutukumbusha la mara ya mwisho lini?

mh heche kama kiongozi wa vijana asipo badilika na kutumika kwa maslahi ya chama na sio yake binafsi tutarajie bavicha dhaifu hasa katika kupambana na nguvu mpya ya ccm
hoja yako anafanya kwa maslahi binafsi? andiko lako mbona ndio la kibinafsi zaidi? Jina HECHE umelitaja mara ngapi? RED
 
natoa maoni yangu kama mwanachadema heche yupo busy kutaka kumharibia mandevu mwita akili yake haiwazi zaidi ya ubunge

amekosa mbinu mbadala za kuimarisha bavicha
naikumbuka bavicha ya mh mnyika

Kijana wa kiume acha umbeya utavalishwa kanga.
 
Wakati fulani,tukubali kushindwa,tulishindwa kwenye uchaguzi wa Bavicha,tuache walioshinda wafanye kazi ya chama.tuwaunge mkono inapobidi.
 
Taingia Heche achaguliwe Bavicha kaishatoa matamko zaidi ya 20 ambayo hayana tija yeyote. Kimsingi Heche kashindwa kuwaongoza vijana.

Je zile ahadi za JK zimetekelezwa ngapi? Posho zinakumalizeni nyinyi.....!
 
wewe ndo una mahaba kama sio una bifu binafsi na Heche, tunamuona mara kwa mara heche anazunguka mikoani na anakusanya watu ambao hata raisi wako akienda mikao hiyo wafiki kiasi hicho, heche ana punch na anapangilia vizuri kuongea leo unasema Heche kashindwa.. we tuambie kashindwa nini.......watu kama ninyi sijui mnatokea wapi

Pro-Chadema wakati mwingine mnachekeshana eti Heche anajaza watu kuzidi JK..ha haa haaa.
 
attachment.php
 
UDHAIFU/MAPUNGUFU YA JOHN HECHE M'KITI BAVICHA

2.John Heche akiwa kama wenyekiti wa BAVICHA bila kusuasua napenda kusema kunambo mengi ndani ya Baraza lake yamekwenda kombo. John heche anatakiwa achukue hatua kuhakikisha yeye na makamu wake wanakuwa kitu kimoja.Hivi sasa nakili wazi viongozi hawa wawili wanaongea na kucheka kama binadamu lakini mioyoni mwao wanatofauti/mpasuko kubwa sana ya kiutendaji.

Heche anakambi yake(sitaki kuitaja) naye makamu mwenyekiti anawatu wake.Hii kwa uhai wa Baraza ni hatari sana,lazima Heche ajitambue kwamba yeye ni kiongozi mkubwa basi hana cha kusubiri zaidi ya kuhakikisha mambo yana kaa sawa. Pia Heche tangu aingie madarakani kunajambo amabalo sijajua ama maksudi au kwa bahati mbaya ameamua kulitupa,kuliacha,kulitelekeza na kuto litupia macho kabisa ili hali ndio muhimili wa Vijana wasomi ndani ya chadema,Ndio shamba la kuvuna vijana wasomi wa chadema,Ndio chuo cha kuzalisha viongozi wa somi ndani ya chadema...Swala hilo ni CHASO.

CHASO-CHADEMA STUDENT ORGANIZATION imetelekezwa,haipo pamoja,inajikongoja.Karibia vyo vyote vya juu vya elimu ya kati vina vijana wa chadema ambao wamejikusanya kwa jitihada zao,wanajiongoza wanakiu ya ukombozi kupita maelezo. Lakini baraza la vijana la chadema chini ya John Heche limeshindwa kuwaunganisha vijana hawa.hakuna uongozi wa CHASO kitaifa,Hakuna nayetambua viongozi wa chaso wanaomaliza muda wake wanakenda wapi?Heche hajui yawezekana hata idadi ya matawi ya chaso ndani ya chadema.

JOhn heche hatembelei kufungua matawi ya chaso,Heche hatembelei kuangalia Vijana hawa wa chasso kwenye matawi yao wanakabiliwa na matatizo gani. John heche jitizame kama umekamilika kuhusu hili,CCM wanalia kuna vijana wanaharakati na wanamapinduzi wasomi wote wanakimbilia CHASO.Vijana wa chaso wanatikisa chaguzi mbalimbali za Urais vyuoni mwao.Lakini je wanaandaliwa mazingira gani ya kukua kisiasa ndani ya baraza la Vijana?

Lakini mwisho,John heche naomba tumie akili yako na ya wenzako,Kuna haja gani ya kendekeza makundi ndani ya barza la vijana?kwanini kwenye mikutano yako hutoi nafasi kwa vijana flaniflani ambao wanaonekana hawapo upande unaouamini ndani ya chama?Weweni kiongozi hutakiwi kuegamia upande wowote..Lakini kesi za kugoma kutoa maiki za kuhutubia mikutanoni kwa vijana flani zimekuwa nyingi sana.

Je kuwanyima maiki ndio suruhisho la mogogoro wako na wao?Je BAVICHA inaundwa na vijana wa upande mmoja?
Mwisho HECHE hadi sasa ameshindwa kuandaa Programu ya vijana kitaifa/kuhamasisha,kukutanisha au kuleta vijana pamoja kitaifa.
Heche yupo busy na majukumu ya program za CHAMA kwa ujumla wake,Kilichomuweka madarakani hajui akifanyie nini,hajui kazi yake ni ipi.
asanteni.

Ni hayo tu
 
wanachadema wenzangu sasa ni wakati wa kutafakari bavicha ni taasisi iliyo zaidi ya mtu heche tumempa nafsi asukume mbele gurudumu la bavicha anaposhindwa hatumsemi kama heche ila kama m/kiti wa chama hivyo uzi wangu haujamlenga heche personal ila kama mkuu wa tasisi yetu muhimu if he cnt deliver he should resign leo tunasema ccm inashindwa kwa kuwa na uongozi dhaifu tukiona wa kwetu nao dhaifu tuseme tusiwe waoga wa kusema ukweli
 
Back
Top Bottom