Kusajiri Private Open University ya Online Tu

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,573
19,455
Je kuna soko la online Open University ya binafsi Tanzania? Nilikuwa na maongezi na kiongozi wa foundation moja ya kimarekani tukaja na idea ya kusajili Tanzania chuo kikuu cha online kwa ajili ya kutoa mafunzo ya shahada za kwanza katika nyanja za Telecommunications, Electronics, Computer Science, na Entrepreneurship kwa nchi za maziwa makuu Afrika. Lengo kuu liwe ni kuwafundisha wanafunzi kuwa wabunifu na kuwa tayari kubuni na kuuza biadhaa zao wenyewe kama wajasiliamali badala ya kuwa waajirwa. Je mradi huo unaweza kuwa na soko Tanzania kweli? Karo zake ziwe chini kabisa ya zile za On-campus au hata za Open-university ya sasa kwani kila kitu kitakuwa online na tutakuwa na overhead ndogo sana. Mitihani yote itakuwa inasimamiwa kwa video conference au tutakuwa na maajenti wa kuisimamia ikilazimika.

Niko kwenye mchakato wa soko kwanza kabla sijaweka proposal kamili na kuanza kuvaana na TCU. Nakaribisha maoni, critique na maswali.
 
First and foremost jaribu kubuni curriculum kwanza itakayo fit na mazingira ya Tanzania na muundo wa TCU utakaokubalika katika ushindani wa elimu na taasisi nyingine hapa nchini, ziwe binafsi pamoja na za serikali. This is the most critical phase utapata kwenye usajili na kukubaliwa ku operate.
 
First and foremost jaribu kubuni curriculum kwanza itakayo fit na mazingira ya Tanzania na muundo wa TCU utakaokubalika katika ushindani wa elimu na taasisi nyingine hapa nchini, ziwe binafsi pamoja na za serikali. This is the most critical phase utapata kwenye usajili na kukubaliwa ku operate.
Asante sana; swala la mitaala tulishalifanyia kazi kwa kutumia model iliyotumia na Taiwan pamoja na Hong Kong miaka ile ingawa hatujui kama itakubalika TCU, ndiyo maana nikasema niangalie soko kwanza kabla ya kuvaana TCU. Taiwan ilijikwamua haraka sana kwa kutumia viwanda vidogo vya electronics vya mtu mmoja mmoja kutokea chumbani mwake na model ile ilifanya kazi vizuri sana. Kwa ssa hivi swala la telecommunications na computer science ndiyo mwelekeo wa dunia, na tuliioona Electronics ndiyo kama baba lao wote, kwa hiyo tukaunganish yote. Lengo kubwa ni kujenga ubunifu katika Telecommunications na Computer Science na kutumia ubunifu huo kibiashara.
 
Back
Top Bottom