Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,573
- 19,455
Je kuna soko la online Open University ya binafsi Tanzania? Nilikuwa na maongezi na kiongozi wa foundation moja ya kimarekani tukaja na idea ya kusajili Tanzania chuo kikuu cha online kwa ajili ya kutoa mafunzo ya shahada za kwanza katika nyanja za Telecommunications, Electronics, Computer Science, na Entrepreneurship kwa nchi za maziwa makuu Afrika. Lengo kuu liwe ni kuwafundisha wanafunzi kuwa wabunifu na kuwa tayari kubuni na kuuza biadhaa zao wenyewe kama wajasiliamali badala ya kuwa waajirwa. Je mradi huo unaweza kuwa na soko Tanzania kweli? Karo zake ziwe chini kabisa ya zile za On-campus au hata za Open-university ya sasa kwani kila kitu kitakuwa online na tutakuwa na overhead ndogo sana. Mitihani yote itakuwa inasimamiwa kwa video conference au tutakuwa na maajenti wa kuisimamia ikilazimika.
Niko kwenye mchakato wa soko kwanza kabla sijaweka proposal kamili na kuanza kuvaana na TCU. Nakaribisha maoni, critique na maswali.
Niko kwenye mchakato wa soko kwanza kabla sijaweka proposal kamili na kuanza kuvaana na TCU. Nakaribisha maoni, critique na maswali.