Kurudisha kitu kibovu duka la game

Kurudisha kitu kibovu duka la game

new generation

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2012
Posts
815
Reaction score
1,721
Habari wakuu? Nimatumaini mko salama..

Ngoja niingie kwenye mada: wakuu jana (15/05/2016) nimenunua home theatre pale game baada ya kuvitiwa na sample iliyowekwa. Ndugu, nilivochagua hyo bidhaa nkaletewa mpya iliyo kwenye box then taratibu za malipo zikafanyika.. Nikaomba kutest wakasema haina haja maana mpya.. Sasa nkafika home kufungua na kuunga kila kitu(install) ndo nkagundua majanga. Product inaquality tofauti na ile iliyokua sample, functions zilipo kwenye manual hazipo kwenye bidhaa mfano AUX, pia hdmi, usb, dvd hazifanyi kazi, sasa hapa naona imekua changamoto..hvo naomba kuuliza kwa wale wenyeji na wazoefu, hawa jamaa wanakubali kupokea bidhaa ikirudishwa kama ina matatizo, au wanakubali pia kurudisha pesa ikitokea hakuna product hyo?.. Naombeni mwongozo wadau.. Aksanten.

NB : risiti zote za manunuzi ninazo.
 
Lazima wana warranty, nenda nayo watajua cha kufanya ,ila hawawezi kukataa kama ina warranty na haija expire warranty!!
 
Wewe rudisha warranty si umepewa watakubadilishia tu
 
Mkuu Hapo Rudisha Mengine Utayajua Hapo Hapo!!!
 
Back
Top Bottom