GE2025 Kurudisha fomu kwa Samia bado kitendawili

GE2025 Kurudisha fomu kwa Samia bado kitendawili

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Julias Vimvinyira

Senior Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
155
Reaction score
205
Kwa muda sasa Watanzania wameshuhudia wagombea mbalimbali wakichukua na hata kurudisha fomu zao za kugombea urais kupitia vyama vyao.

Lakini jambo la kushangaza ni ukimya mzito ndani ya CCM kuhusu lini Mwenyekiti wao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atarudisha fomu yake.

Kwa nini chama tawala hakitoi ratiba wala taarifa yeyote juu ya tukio hili kubwa linalogusa mustakabali wa taifa?

Au kimya hiki ni mkakati wa makusudi kutengeneza “surprise” kubwa ya kisiasa?

Je, mafukuto ya ndani ndio sababu ya kuchelewesha mchakato huu?

Wakati wagombea wengine wakisonga mbele, urudishwaji wa fomu ya Samia unaendelea kubaki kitendawili.

Wananchi tusubiri hadi lini kupata majibu?

Pia soma >> GE2025 - Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu achukua Fomu ya Urais Oktoba 2025
 
Kwa muda sasa Watanzania wameshuhudia wagombea mbalimbali wakichukua na hata kurudisha fomu zao za kugombea urais kupitia vyama vyao.

Lakini jambo la kushangaza ni ukimya mzito ndani ya CCM kuhusu lini Mwenyekiti wao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atarudisha fomu yake.

Kwa nini chama tawala hakitoi ratiba wala taarifa yeyote juu ya tukio hili kubwa linalogusa mustakabali wa taifa?

Au kimya hiki ni mkakati wa makusudi kutengeneza “surprise” kubwa ya kisiasa?

Je, mafukuto ya ndani ndio sababu ya kuchelewesha mchakato huu?

Wakati wagombea wengine wakisonga mbele, urudishwaji wa fomu ya Samia unaendelea kubaki kitendawili.

Wananchi tusubiri hadi lini kupata majibu?
Kwani una taarifa za kitakachojiri tarehe 28/08/2025 pale Tanganyika Packers Kawe?
 
Wanajipanga mkuu, kumbuka kuna kuratibu kusomba watu kutoka pande zote za nchi....usichukulie poa!!.
 
Back
Top Bottom