Kurudisha 25% ya mkopo HESLB

noel oga

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2015
Posts
277
Reaction score
230
Wapendwa naomba mnisaidie,

Nilipewa mkopo na Bodi nikaacha masomo sababu sikumudu gharama kutokana na kupewa mkopo mdogo. Nilpotaka kuomba tena nikasikia tetesi inatakiwa nirudishe 25 percent ndipo nipewe tena.

Je, kama nilipewa 2,649,000/=, hiyo 25 percent katika hii inarejeshwa kiasi gani?

Msaada mwenye uzoefu au mkasa kama huu.
Ahsanteni..
 
Kweli wamekuchanganya kabisa maana hata pesa uliyoandika ni tabu kuelewa. Ila kanuni ni rahisi: "Chukua pesa ULIYOKOPESHWA zidisha kwa 25 kisha GAWANYA kwa 100" utapata 25% unayotaka kufahamu.
 

Fanya hii hesabu:
25/100x2,649,000/=
 
inamaana kucalculate hujui au tukusaidie kukupa calculator??
 

Aiseee una taabu hata Kupata 25% kwenye 2649 ujui? Alafu ulienda chuo kikuu?
 

Huko la tano ulipitapitaje hadi form four?
Ama ndo kuudhihirishia ulimwengu hesabu ni jipu lingine linahitaji kutumbuliwa?
 
ficha ujinga wako,we hujui hata hesabu ya darasa la nne ulifikaje chuo kikuu
 
25%? tofauti yao nini na kwenye mabenki na ukizingatia akiwa mtumishi atalipa kodi.
 
Utalipa hiyo na wataanza kukufanyia mchakato upya kama upate au ukose mkopo, usijihakikishie ukadhani ukilipa hiyo asilimia wanakupa mkopo upya
 

Mmh!,unatupa wasiwasi kama kweli hii nayo inahitaji kupewa elimu,asilimia 25 ya kiasi ulichopewa inakutatiza.
 
Haya fanya hivi.
Chukua 25 zidisha kwa "mil.2649,000"
halafu jibu utakalolipata ligawe kwa 100.
Jibu utakalolipata ndio pesa utakayolipa.
 
Last edited by a moderator:
sasa mkopo ulipewa wa nini kama hata hesabu za chekechea huziwezi?
 
Elimu yake itakuwa haina maana kama haujui hesabu rahisi kama hiyo. Kila kitu mwanadamu unatumia hesabu. Ila sishangai kutokana na watu wengine wanamaliza chuo hawajui kuandika...
 
Matusi mengine mnajitakia,yaani mwanafunzi wa chuo kikuu hujui kutafuta asilimia 25 ya Tsh 2649000?!Halafu utashangaa huyu Naye anagraduate,Haya ni maajabu ya dunia kwa kweli
 
Huoni Hata aibu kuuliza swali hilo,hizo ni hesabu za darasa la nne,kama umeshindwa mtafute mwanafunzi wa la NNE akusaidie,Mambo ya aibu,ajabu unasomea nn usijue Haya hesabu za kutafuta asilimia,kwa kweli kwa hili,nitashangaa milele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…