KURA YANGU URAIS TZ 2015, ntampigia HUYU HAPA

Pamoja na yote, lakini simply unamaanisha kura utampa Dr.Slaa, kulingana na issues ambazo umezi-list. Ni sawa na kusema nataka nikasome elimu bora ya Sheria, maana yake unataka ukasome UDSM Kitivo cha Sheria
 
Najua mnataka niseme ntampigia:
MEMBE

SLAA

ZITTO

LOWASSA

MIGIRO

MBOWE

WASSIRA NK

Hapana. Kura ntampatia mgombea yeyote na wa chama chochote atakaye ahidi kunihakikishia yafuatayo:
(1) MAKAZI BORA, SIKUBALI KUENDELEA KUISHI KWENYE TEMBE

(2) AJIRA

(3) ELIMU BORA KWA WANANGU

(4) HUDUMA BORA ZA AFYA

(5) KUTOKOMEZA RUSHWA NA UFISADI

(6) KUHAKIKISHA HAKI KWA KILA MMOJA

(7) ATAKAYEACHA KUBEMBELEZA WAZENJ KUKAA KWENYE MUUNGANO, WAENDE WAKITAKA

(8) ATAKAYEUNDA "INDEPENDENT POLICE COMPLAINTS COMMISSION"

Kama ndio vigezo vyako, ambavyo kwa kweli ni vizuri na vya msingi, basi hakuna mgombea wa CCM atapata kura kwa sababu;

1 -kwenye sera za CCM makazi bora kwa kila mtanzania si kipaumbele. ndio maana hawashushi bei au kuondoa kodi kwenye vifaa vya ujenzi kama cement. Ndio maana hata nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba bei zake zinaanzia mamia ya mamilioni!

2 -CCM haitekelezi sera ya ajira kwa vitendo isipokuwa inazalisha wachuuzi; imeua viwanda na imeuza kila kitu kwa wageni Na ajira nzuri zote ni kwa wageni na watoto wao mfano angalia kwenye mabenki, makampuni ya insurance nk

3 -CCM imeua elimu Na imeendekeza bora elimu. wanaopata elimu bora ni wenye pesa na sasa chuo kikuu au vyuo vya juu kama mzazi hana pesa utapasikia tu. Na hao watoto wako kama huna pesa ukichagua CCM chuo watapasikia tu!

4 -hapa sina comment, We mwenyewe unajionea na kusikia

5 -CCM imeshakiri haiwezi kutokomeza rushwa na Ufisadi kwa sababu nchi itatikisika. Na umejionea mwenyewe uchaguzi Mkuu wa CCM wajumbe karibu wote wa NEC na viongozi wa jumuia wakipita kwa rushwa na mwemyekiti wa chama kubariki. Tunashuhudia wafisafi na wezi wa mabilioni wakiwekwa hadharani lakini serikali ya CCM ikishindwa kuchukua hatua zozote!

6 -CCM tayari imeshindwa kuhakikisha haki kwa kila mmoja. haki iko kwenye makararasi lakini kivitendo mwenye haki ni yule mwenye pesa!

7 -CCM imeshakuwekea wazi muungano ni lazima na wa serikali mbili; muungano na Zanzibar bila Tanganyika. Na hili usilijadili!

8 -katika serikali ya CCM Polisi ni ya watawala, Hakuna cha independence commission

Upo hapo? kwa haya sema tu ukweli usione haya kujadili vyama Au personalities, CCM si chama chako kwa sababu hakitakupa kiongozi atakayeweza masharti yako.
 
Lakini iwapo uzi huu ungekuwa unajadili PERSONALITIES fulani fulani ndio zinafaa, hakika mjadala ungefana, lakini kwa sababu unajadili ISSUES tunazotarajia wateule waje kuzifanyia kazi kama njia ya kutatua matatizo ya wananchi, wengi hawaupi mjadala huu uzito unaotakiwa; Lakini ni hawa hawa wenye hoja za personalities ndio wapo mstari wa mbele kusakama viongozi wasiofaa kwa hoja kwamba kuna masuala hawasimamii vizuri; sasa kwanini mnanunulika kuwaunga mkono kama hamjui watakuja kusimamia masuala yepi?
Suala la biashara ya demokrasia (hapa kuuza na kununua wapiga kura) ndiyo imeshika kasi Tanzania. Huu nu ugonjwa sugu ambao ni lazima wapiga kura waelimishwe sana. Kuna mwana falsafa mmoja alisema kuwa wafanye wapiga kura maskini ili mosi watawaliwe na elite class ambao kwa sasa ni watoto wa viongozi wetu, pili waweze kurubuniwa kirahisi kupitia matatizo yao ili wapige kura kwa chama hasa tawala. Kwa mantiki hii tumeona mosi ikifanya kazi kwa kasi sana na namba mbili umaskini unalazimu wapiga kura kuuza shahada kwa 5,000/= au kwa kanga na kofia kwa kuangalia tatizo la usoni bila kuona makubwa yajayo. Ni wakati sasa elimu itolewe na kuaswa kabisa kuuza demokrasia na kama ni rushwa wapokee ila siku ya uchaguzi anachagua anayefaa maana anayepigiwa kura hawezi kukulaumu maana hajui kama ni yupi aliyempigia kura. Kazi ipo Mchambuzi. Endela kutuchambulia tu.
 
Hata hizo issue zikiangaliwa wanasiasa wetu wote ni waongo! Wataongopa kama wimbo wa prof. J lakini mwisho wa siku ni kujineemesha wao, familia zao, marafiki zao na wapambe wao. wengine tutaishia kukumbuka issues na kunyong'onyea tu.

KWA hiyo vipi? Tumekubali kushindwa, tuwaache waendelee kuongopa tuuuuuuuuuuu: HAPANA. Tuwawajibishe, na uongo unaendelea kwa sababu hatuwalazimishi wafanye siasa za issue, na kuachana na siasa za sura, urefu, nani kaoa nani na upuuzi mwingine kibao.
 
Suala la biashara ya demokrasia (hapa kuuza na kununua wapiga kura) ndiyo imeshika kasi Tanzania. Huu nu ugonjwa sugu ambao ni lazima wapiga kura waelimishwe sana. Kuna mwana falsafa mmoja alisema kuwa wafanye wapiga kura maskini ili mosi watawaliwe na elite class ambao kwa sasa ni watoto wa viongozi wetu, pili waweze kurubuniwa kirahisi kupitia matatizo yao ili wapige kura kwa chama hasa tawala. Kwa mantiki hii tumeona mosi ikifanya kazi kwa kasi sana na namba mbili umaskini unalazimu wapiga kura kuuza shahada kwa 5,000/= au kwa kanga na kofia kwa kuangalia tatizo la usoni bila kuona makubwa yajayo. Ni wakati sasa elimu itolewe na kuaswa kabisa kuuza demokrasia na kama ni rushwa wapokee ila siku ya uchaguzi anachagua anayefaa maana anayepigiwa kura hawezi kukulaumu maana hajui kama ni yupi aliyempigia kura. Kazi ipo Mchambuzi. Endela kutuchambulia tu.

SULUHISHO. Kila mtu na alipe kodi, ni kodi pekee iliyowaamusha wenzetu ULAYA NA AMERICA miaka ya 1800 NA KUANZA kudai huduma bora kutoka kwa watawala na haki, kwani walizilipia. SISI hapa watawala wetu wamewakwepa wananchi, hawawtozi kodi moja kwa moja, wamewakwepa kwa kupitia MICHANGO kibao, kwa hiyo wananchi hawako aggressive. KILA MTU ALIPE KODI, nakuhakikishia atakataa kuhadaiwa na kitenge, kanzu, kofia, ubwabwa nk
 
"... masuala nyeti ya taifa" MCHANGO WAKO NI UPI SASA kwenye hayo masuala nyeti?

huyo slaa kama familia imemshinda nchi ataiweza? Kama halmashauri chache zinazoongozwa na cdm zimeongoza kwa migogoro nchi ataiweza? Acheni mzaha inapofika suala la kujadili masuala nyeti ya taifa
 
MKUU njia zipo: (1) recall, kama ya wa-AMERICA, hapa kwetu sheria hairuhusu; (2) bunge kuiwajibisha serikali kupitia KURA YA KUTOKUWA NA IMANI na PM (ARTICLE 53A TZ constitution 1977); na (3) (sovereignty) wananchi kutumia ukuu wao (artile 8 TZ 1977 CONST) kuiwajibisha serikali kwa mujibu wa KATIBA hiyo.

KIBOL, hizi blah2 zinaendelea kwa sababu si2 wananchi TUNACHEZA NGOMA YA WANASIASA BADALA YA WANASIASA KUCHEZA NGOMA YETU: si2 tutengeneze ajenda then wao waje na progaramu za kuzitekeleza, siyo kama sasa ambao wao wanafanya vyote - wanaseti ajenda wao hao2 na wanatengeza programu wao hao2, hapo hatuwezi kuambulia kitu ..

mkuu nimeipenda hii,ila swala hapa nikuwa uchaguzi unafanyika kabla ya hayo yote,halafu wengi wa wanasiasa wanayazungumza sana haya kabla ya uchaguzi,swali mkuu,hakuna namna ya kuwawajibisha hawa wanasiasa pindi watakaposhindwa kutekeleza kile walichoahidi kuliko kukaa chini na kusubiria duru nyingine ya uchaguzi tena baada ya miaka 5?hilo unalizungumziaje kaka?
 
Post yako ni nzuri ila kama ni Ahadi na Kukuhakikishia hata mimi na kila mtu au Mgombea wanaweza kufanya hivyo.
Kikubwa hapa ni Uwezo, Mikakati, na Mipango haswa ndio tunataka kuona na kusikia kutoka kwa Wagombea Urais aka Taasisi ya Urais.

HAPO kwenye underline, hapo sasa. KWANZA tupate vipaumbele kama vilivyotajwa; PILI wenye uwezo, mikakati na mipango.
 
Mimi nitamchagua huyu
asiyependa ufisadi
asiye mnafiki
asiye muoga
asiyefumbia macho mafisadi
mwenye kuwapenda watanzania kuliko chama
asiye fikiri chama ni muhimu kuliko nchi
asiyetoa hongo wakati wa uchaguzi na kusema ni takrima
asiye subiri kuwatembelea wananchi wake wakati wa uchaguzi
ambaye anawataja wala rushwa waziwazi
asiye zunguka kwenye matamasha na nyumba za ibada kuomba kura
asiyefumbia macho wahujumu uchumi
ambaye hazungumzii udini kwenye mambo ya siasa
 
Back
Top Bottom