Kura ya maoni Liberia

Kura ya maoni Liberia

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,026
Reaction score
20,511
Wapiga kura nchini Liberia wameukataa mpango wa kurefusha kipindi cha uchaguzia hadi Novemba. Maafisa wamesema uchaguzi huo utafanyika katika tarehe iliyopangwa Oktoba 11. WabungeÂ* nchini humo walipendekezaÂ* kubadiliÂ* tarehe hiyo iliÂ* kuhakikisha uchaguzi haufanyiki katika kipindi cha msimu wa mvua, kuepusha matatizo ya usafiri na matatizo mengine.

Mpango huo ulitakiwa kuidhinishwa na wapiga kura katika kura ya maoni lakini haukuungawa mkono. Kushindwa kwa mpango huo kunaangaliwa kuwa ni pigo kwa rais aliye madarakani Ellen Johnson Sirleaf ambaye chama chake kilipigania kubadilishwa tarehe ya uchaguzi. Chama cha upinzani Congress for Democratic Change kikiungwa mkono na mchezaji kandanda wa zamani wa kimataifa George Weah kiliendesha kampeni ya kuyapinga mabadiliko hayo.
 
Vipi George Weah atagombea tena?
 
Back
Top Bottom