Kupungua Mizigo Bandarini: Je, Kuna Uwezekano Waziri Mkuu amelidanganya Bunge?, Kadanganywa Au ?!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,554
113,736

Wanabodi,
Jana Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa aliliambia Bunge kuwa kupungua kwa mizigo bandarini Dar, kumechangiwa, pamoja na mambo mengine, na mdororo wa uchumi wa dunia, na chaguzi za majirani zetu wanaotumia bandari ya Dar es Salaam; hivyo wafabiashara walipunguza kuagiza mizigo! .

Katika kuwahakikishia Watanzania kuwa bandari ya Dar es Salaam itarejea katika hali yake ya kawaida ya kumhudumia mizigo mingine, Waziri Mkuu amesema serikali ya Tanzania imepokea barua kadhaa kutoka serikali za nchi majirani zetu waliokuwa wakipitisha mizigo yao bandari ya Dar es Salaam kuwa sasa wataendelea kupitishia mizigo yao yote bandari ya Dar es Salaam! .

Jee ni kweli barua hizo zipo, na jee kama hakuna tatizo lolote, iweje nchi hizo zilete barua?!. Kwani zilisimamisha kupitishia mizigo yao bandari ya Dar es Salaam hadi zile teacher barua kuwa sasa zitaendelea kupitishia? !. Kuna Uwezekano wa Bunge kuwa limedanganywa tuu ili kuwahadaa Watanzania kuwa there is nothing wrong with kupungua mizigo bandari ya Dar es Salaam, and serikali ya Tanzania has nothing to do with that situation bali ni mdororo wa uchumi na siasa za nchi Jirani?!.

Tena wabunge makini waombe barua hizo ziletwe bungeni ili na sisi akina Tomaso, tuzione! .
Bandari ni moja za pillars za uchumi wa taifa na mapato ya nchi hii, hivyo suala la kupungua kwa mizigo bandarini ni very serious, sensitive na critical issue inayohitaji majibu serious na credible na sio majibu rahisi kwa maswali magumu huku majibu mengine yakiwa ni majibu ya kisiasa tuu!.

Hoja kuu ya kupungua kwa mizigo bandarini Dar ni wasafirishaji wa mizigo waliokuwa wakipitishia mizigo yao bandari ya Dar es Salaam, kuamua kuihama bandari ya Dar es Salaam na kupitishia mizigo yao bandari ya Mombasa na bandari nyingine hadi Beira kwa "sababu fulani! " ambayo haitajwi au inakwepwa! .

Wakati sisi bandari yetu mizigo inapungua, bandari za wenzetu mizigo inaongezeka!, sababu ingekuwa ni mdororo wa uchumi wa dunia, then kote mizigo ingepungua direct proportional na mdororo wa uchumi! .

Kubwa kuliko ambao ni kama uongo wa mchana kweupe ni hizo barua zinazodaiwa kuandikiwa na serikali jirani kutoa hakikisho kuwa mizigo yao yote itapitia bandari ya Dar es Salaam! .
Maswali ni. ..Hiyo mizigo iliyopungua ni mizigo ya serikali hizo hivyo serikali hizo zimeiandikia serikali ya Tanzania kuihakikishia kuendelea kupitishia mizigo yao yote bandari ya Dar es Salaam? !.

Kama mizigo ni ya wasafirishaji binafsi, watu, mashirika na makampuni ambao wanafanya cost/benefits assessment na kuamua kukimbia bandari ya Dar es Salaam na kutumia bandari nyingine!, hivyo hizo barua za serikali zao, zitawalazimisha wasafirishaji hao kuitumia bandari ya Dar es Salaam kwa lazima hata kama sio cost effective?!.

Kwanini viongozi wa Serikali wanakwepa ku deal na chanzo halisi na kisababishi cha kupungua kwa mizigo bandarini Dar na badala yake wanatafuta visingizio vya mdororo wa uchumi wa dunia na hadi ahadi hewa?!.

Kama mizigo imepungua kwa mdororo wa uchumi wa dunia, hiyo mizigo kutoka hizo nchi walizotuandikia barua itatokea wapi?!, au wao ndio uchumi wa dunia waliamua uchumi wa dunia udorore sasa wameurekebisha hivyo wametuhakikishia mizigo? !.

Kama hatuta deal na chanzo halisi (the root cause) ya kushuka kwa mizigo bandarini Dar na kuukata huo mzizi wa fitna, muda wa sababu za visingizio utapita bila mizigo kuongezeka!, muda huo ukifika, viongozi wetu watatueleza nini? ! .

Hitimisho.
Hili ni swali la uwezekano (posibility) wa Bunge letu tukufu kudanganywa na tafadhalini sana msiojua lugha, sijasema Bunge letu limedanganywa! . Mawazo yangu yananiambia sababu za kupungua mizigo bandarini Dar zipo na zinaeleweka na sio hizi zinazoelezwa!, na hata mashaka ya kuwepo barua toka nchi hizo!.

Kwa hivyo kama ikitokea hizo sababu zilizotolewa bungeni ndizo sababu zenyewe halisi na barua hizo pia zipo, then itakuwa Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, hajalidanganya Bunge letu tukufu bali Pasco wa JF ndie aliyedhania tuu kuwa Waziri Mkuu Amelidanganya Bunge kutokana na sababu alizoelezwa huyu Pasco ni tofauti na zilizoelezwa bungeni hivyo itakuwa Pasco ndiye alidanganywa na Waziri Mkuu kasema ukweli! .

Hili likifanyika Pasco atarejea na uzi mwingine wa sababu alizoelezwa yeye za kupungua kwa mizigo bandarini Dar es Salaam na sababu hizo zitalinganishwa na zile zilizotolewa bungeni kisha "the time will judge the truth! ".

Nawatakia Furahi Dei Njema! .
Ijumaa Karim !.
Pasco.
NB. Wataalam wa sheria, hivi kuuliza swali kama kuna uwezekano wa kiongozi fulani amedanya, ikitokea kiongozi huyo hajadanganya! linaweza kuwa ni kosa kwa muuliza swali? !.
Pasco
Pasco raisi wa chama cha maafisa forodha Tanzania
 
Honeymoon imesha sasa ndio wameingia rasimi kwenye ndoa hivyo wameanza kuonja shubiri ya ndoa.

Kipindi kile cha honeymoon walituaminisha mambo mengi na kwakweli hata kuwakosoa ilioneka ni kosa kubwa ila sasa maisha ya ndoa yanawaumbua.
 
Waziri Mkuu anajibu swali kama vile haishi Tanzania haoni hata hali ilivyokuwa mbaya. Tumeshazoea majibu mepesi mepesi kwa mazito kama hayo. Unahitaji utafiti gani kugundua hali ya uchumi imeshuka? Huoni hata picha hata umedanganywa?
 
Tatizo kubwa tuna wabunge wanaofikili matumbo yao hata kwenye Ukweli wanajitia upofu ni bunge kibogoyo ni bunge la wachumia tumbo wao kwao posho ni bora na kushangilia kwa manufaa ya vyama vyao hawako tayari kuhoji mambo ya msingi awako tayari kufa kwaajili ya watanzania mungu anawaona ndio maana wakikosa ubunge Ndani ya miezi 6 wanasikitisha mpaka basi
 
Mwisho wa uongo ni aibu narudia tena tumbueni majipu tani yenu,
Futeni kazi watu kwanguvu zote
Hamieni dodoma kwa spidi kubwa,

Lakini kumbukeni maisha ya watu yataangalia wameboreshewa maisha yao kwa kiasi gani kama wakijua ni gilba tuu
Watawageuka nanyi mtaitwa wamoja na wale nafisadi na wanaojifanya chama na nchi hii mali yao...

Yangu macho nasubiri..
 
Wanabodi,
Jana Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa aliliambia Bunge kuwa kupungua kwa mizigo bandarini Dar, kumechangiwa, pamoja na mambo mengine, na mdororo wa uchumi wa dunia, na chaguzi za majirani zetu wanaotumia bandari ya Dar es Salaam; hivyo wafabiashara walipunguza kuagiza mizigo! .

Katika kuwahakikishia Watanzania kuwa bandari ya Dar es Salaam itarejea katika hali yake ya kawaida ya kumhudumia mizigo mingine, Waziri Mkuu amesema serikali ya Tanzania imepokea barua kadhaa kutoka serikali za nchi majirani zetu waliokuwa wakipitisha mizigo yao bandari ya Dar es Salaam kuwa sasa wataendelea kupitishia mizigo yao yote bandari ya Dar es Salaam! . Jee ni kweli barua hizo zipo, na jee kama hakuna tatizo lolote, iweje nchi hizo zilete barua?!. Kwani zilisimamisha kupitishia mizigo yao bandari ya Dar es Salaam hadi zile teacher barua kuwa sasa zitaendelea kupitishia? !. Kuna Uwezekano wa Bunge kuwa limedanganywa tuu ili
kuwahadaa Watanzania kuwa there is nothing wrong with kupungua mizigo bandari ya Dar es Salaam, and serikali ya Tanzania has nothing to do with that situation bali ni mdororo wa uchumi na siasa za nchi Jirani?!. Tena wabunge makini waombe barua hizo ziletwe bungeni ili na sisi akina Tomaso, tuzione! .

Bandari ni moja za pillars za uchumi wa taifa na mapato ya nchi hii, hivyo suala la kupungua kwa mizigo bandarini ni very serious, sensitive na critical issue inayohitaji majibu serious na credible na sio majibu rahisi kwa maswali magumu huku majibu mengine yakiwa ni majibu ya kisiasa tuu!.

Hoja kuu ya kupungua kwa mizigo bandarini Dar ni wasafirishaji wa mizigo waliokuwa wakipitishia mizigo yao bandari ya Dar es Salaam, kuamua kuihama bandari ya Dar es Salaam na kupitishia mizigo yao bandari ya Mombasa na bandari nyingine hadi Beira kwa "sababu fulani! " ambayo haitajwi au inakwepwa! .

Wakati sisi bandari yetu mizigo inapungua, bandari za wenzetu mizigo inaongezeka!, sababu ingekuwa ni mdororo wa uchumi wa dunia, then kote mizigo ingepungua direct proportional na mdororo wa uchumi! .

Kubwa kuliko ambao ni kama uongo wa mchana kweupe ni hizo barua zinazodaiwa kuandikiwa na serikali jirani kutoa hakikisho kuwa mizigo yao yote itapitia bandari ya Dar es Salaam! .
Maswali ni. ..
Hiyo mizigo iliyopungua ni mizigo ya serikali hizo hivyo serikali hizo zimeiandikia serikali ya Tanzania kuihakikishia kuendelea kupitishia mizigo yao yote bandari ya Dar es Salaam? !.

Kama mizigo ni ya wasafirishaji binafsi, watu, mashirika na makampuni ambao wanafanya cost/benefits assessment na kuamua kukimbia bandari ya Dar es Salaam na kutumia bandari nyingine!, hivyo hizo barua za serikali zao, zitawalazimisha wasafirishaji hao kuitumia bandari ya Dar es Salaam kwa lazima hata kama sio cost effective?!.

Kwanini viongozi wa Serikali wanakwepa ku deal na chanzo halisi na kisababishi cha kupungua kwa mizigo bandarini Dar na badala yake wanatafuta visingizio vya mdororo wa uchumi wa dunia na hadi ahadi hewa?!. Kama mizigo imepungua kwa mdororo wa uchumi wa dunia, hiyo mizigo kutoka hizo nchi walizotuandikia barua itatokea wapi?!, au wao ndio uchumi wa dunia waliamua uchumi wa dunia udorore sasa wameurekebisha hivyo wametuhakikishia mizigo? !.

Kama hatuta deal na chanzo halisi (the root cause) ya kushuka kwa mizigo bandarini Dar na kuukata huo mzizi wa fitna, muda wa sababu za visingizio utapita bila mizigo kuongezeka!, muda huo ukifika, viongozi wetu watatueleza nini? ! .

Hitimisho.
Hili ni swali la uwezekano (posibility) wa Bunge letu tukufu kudanganywa na tafadhalini sana msiojua lugha, sijasema Bunge letu limedanganywa! . Mawazo yangu yananiambia sababu za kupungua mizigo bandarini Dar zipo na zinaeleweka na sio hizi zinazoelezwa!, na hata mashaka ya kuwepo barua toka nchi hizo!. Kwa hivyo kama ikitokea hizo sababu zilizotolewa bungeni ndizo sababu zenyewe halisi na barua hizo pia zipo, then itakuwa Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, hajalidanganya Bunge letu tukufu bali Pasco wa JF ndie aliyedhania tuu kuwa Waziri Mkuu Amelidanganya Bunge kutokana na sababu alizoelezwa huyu Pasco ni tofauti na zilizoelezwa bungeni hivyo itakuwa Pasco ndiye alidanganywa na Waziri Mkuu kasema ukweli! .

Hili likifanyika Pasco atarejea na uzi mwingine wa sababu alizoelezwa yeye za kupungua kwa mizigo bandarini Dar es Salaam na sababu hizo zitalinganishwa na zile zilizotolewa bungeni kisha "the time will judge the truth! ".

Nawatakia Furahi Dei Njema! .
Ijumaa Karim !.
Pasco.
NB. Wataalam wa sheria, hivi kuuliza swali kama kuna uwezekano wa kiongozi fulani amedanya, ikitokea kiongozi huyo hajadanganya! linaweza kuwa ni kosa kwa muuliza swali? !.
Pasco
kudanganya ni kawaida yetu
 
Katika kuwahakikishia Watanzania kuwa bandari ya Dar es Salaam itarejea katika hali yake ya kawaida ya kumhudumia mizigo mingine, Waziri Mkuu amesema serikali ya Tanzania imepokea barua kadhaa kutoka serikali za nchi majirani zetu waliokuwa wakipitisha mizigo yao bandari ya Dar es Salaam kuwa sasa wataendelea kupitishia mizigo yao yote bandari ya Dar es Salaam!
Jambo moja nina uhakika nalo! Mamlaka ya Bandari wametengeneza tangazo la kuwabembeleza (kuwavutia?) wafanya biashara waje kuitumia bandari ya Dar es salaam na kwamba hivi sasa iko poa ile mbaya!! Kwenye tangazo lile, kuna sauti ya JPM nayo ikihamasisha wafanyabiashara wajitokeze!!!

So, it's funny kuona Mamlaka ya Bandari inatumia mapesa mengi kutengeneza matangazo wakati kumbe hao watu wanaowahamasisha tayari wameshaanza kujileta wenyewe tena kwa kuandika barua za maombi!!! Hivi tutaweza kweli kulihudumia nyomi la hawa wanaojileta wenyewe tena kwa kutuma maombi na wengine tunaowahamasisha wenyewe!!!!

I love my country!!!
 
Pasco hili swala la mizigo kupungua kwenye bandari yetu linajadiliwa kwa hisia za kiasiasa sana kiasi kwamba tunaukwepa ukweli...
Kwa nilivyosoma taarifa huko nyuma ni kwamba ili kupunguza ukwepaji kodi, serikali iliamua hata mizigo iendayo nchi jirani ilipiwe VAT na wakala wa uondoshaji mizigo lakini wanaidai baada ya mizigo kuthibika kuwa ilikwenda nchi husika. Siku za nyuma wafanya biashara wasiopenda nchi yetu waliingiza bidhaa na kusema zaenda DRC au Burundi lakini zinaishia Kariakoo.

Sasa VAT on transit ni kama kuweka bond ili endapo mzigo hautavuka border serikali haipotezi mapato. Hakuna mfanyabiashara yuko tayari kufungia pesa [cash flow] yake kwa ahadi ya kurejeshewa endapo kuna mtoa huduma mwingine hana sharti hilo.
Jambo hili lina athari kwa wadau wenye kutegemea bandari kuanzia mama lishe anayeuza chai kwa wabeba mizigo bandarini, wasafirishaji, TPA na wengine wengi.

Kwa hiyo hata ongezeko la makusanyo ya kodi yanayotangazwa kila mwezi yana mchango wa VAT on transit ambayo kimsingi sio hela yetu.

Tunapoweka tu siasa kwenye hili tunapoteza mwelekeo
 
Jambo moja nina uhakika nalo! Mamlaka ya Bandari wametengeneza tangazo la kuwabembeleza (kuwavutia?) wafanya biashara waje kuitumia bandari ya Dar es salaam na kwamba hivi sasa iko poa ile mbaya!! Kwenye tangazo lile, kuna sauti ya JPM nayo ikihamasisha wafanyabiashara wajitokeze!!!

So, it's funny kuona Mamlaka ya Bandari inatumia mapesa mengi kutengeneza matangazo wakati kumbe hao watu wanaowahamasisha tayari wameshaanza kujileta wenyewe tena kwa kuandika barua za maombi!!! Hivi tutaweza kweli kulihudumia nyomi la hawa wanaojileta wenyewe tena kwa kutuma maombi na wengine tunaowahamasisha wenyewe!!!!

I love my country!!!
Watu wa dizaini yako ndio wanaipoteza tanzania kwenye ramani ya mafanikio.

Poor empty mind
 
Back
Top Bottom