Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Habari za kuaminika kutoka kampuni ya uchapishaji wa magazeti ya New Habari inayomilikiwa na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz zinasema kwamba gazeti la kila siku la Mtanzania limeporomoka mauzo kiasi kwamba mhariri wake Danny Mwakiteleko ameondolewa katika mabadiliko makubwa yaliyotangazwa mapema mwezi huu.
Kwa wanaomfahamu Mwakiteleko, kuporomoka kwa Mtanzania kimauzo hakuingii akilini kabisa -- hasa kutokana na umahiri wake – ikikumbukwa kwamba miaka kadha iliyopita alipokuwa mhariri wa gazeti la Majira aliweza kuliboresha gazeti hilo hadi kufikia kiwango cha kuwa mpinzani mkubwa wa gazeti la Nipashe la Reginald Mengi.
Mwakiteleko sasa kapewa wadhifa wa kuwa Naibu mhariri Mkuu wa magazeti ya New Habari, hatua inayoonekana kama kumpandisha cheo. Lakini habari za uhakika ni kwamba kaondolewa kwa agizo kutoka kwa mmiliki, Rostam, baada ya kuona mauzo yanaporomoka sana tangu ashike gazeti hilo takriban miaka miwili iliyopita.
Ilikuwa ni wakati Rosemary Mwakitwange akiwa CEO wa kampuni na alimuajiri kutokana na umahiri wake na kwa mshahara mkubwa sana. Kuna baadhi wanasema Mwakiteleko alibadilika baada ya kuondoka kwa Rosemary ambaye alikosana na Rostam kuhusu suala la mwelekeo na sera za magazeti ya New Habari hasa katika masuala ya kundika habari za ufisadi.
Habari zinasema kwamba Rostam alimwambia Mhariri Mtendaji Muhingo Rweyemamu amuondoe Mwakiteleko kama mhariri wa Mtanzania na atafute pa kumweka, hivyo akaamua kumweka kuwa naibu wake.
Gazeti hilo, lililojijengea sifa kubwa miaka ya nyuma sasa linapitwa na karibu magazeti yote ya Kiswahili ya kila siku na sasa hivi meza nyingi za kuuzia magazeti hapa Dar halionekani. Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana.
Kuporomoka kwa Mtanzania (kama ilivyo kwa gazeti la kila wiki la RAI) linatokana na msimamo wake kuhusu masuala ya ufisadi – lilikuwa linajitambulisha sana na wale wote wanawatetea mafisadi – kwa bayana, lakini mara nyingi kwa ujanjaujanja tu. Inadaiwa kuwa stori nyingi za ukurasa wa mbele zilikuwa zinatokana na agizo la Rostam mwenyewe au washauri wake -- kama vile Salva Rweyemamu.
Mara nyingine stori hizo huwa zinaletwa nzima nzima dakika za mwisho kabla ya kwenda mtamboni na hubandikwa zilivyo. Mwakiteleko alikuwa akiridhia hivyo kwa sababu mbili – agizo kutoka juu, na kulinda mshahara wake mkubwa.
Kwa hivyo ni kitu cha kushangaza kuona Rostam amemgeuka Mwakiteleko ili hali yeye mwenyewe ndiyo sababu ya uzorotaji wa gazeti.
Lakini kuna maelezo mengine tofauti – kwamba wahariri wengi wa magazeti ya New Habari, hususan Mtanzania, Mtanzania Jumapili na RAI (kama vile Balile, Manyerere, Munyunku, Matinyi, Sarah Mosi, Mayage n.k.) hujipendekeza tu kwa Rostam katika kuandika stori wanazofikiria zitampendezesha yeye na zile wanazoona zinaweza kumsafisha katika matatizo yake yanayomuandama – hata kama ni kuwachafua watu wengine.
Kwa vyovyote vile, hali hii imeathiri sana magazeti hayo. Nafasi ya Mwakiteleko, Muhingo kamteua Balile kuwa mhariri wa Mtanzania, katika hatua ambayo wengi wanaona ni kuzidi kulididimiza gazeti hilo.
Habari zinasema kwamba kama Mwakiteleko alikuwa anatetea mafisadi kiujanjajanja, basi Balile atafanya hivyo kwa bayana kabisa.
Tungoje tuone.
Kwa wanaomfahamu Mwakiteleko, kuporomoka kwa Mtanzania kimauzo hakuingii akilini kabisa -- hasa kutokana na umahiri wake – ikikumbukwa kwamba miaka kadha iliyopita alipokuwa mhariri wa gazeti la Majira aliweza kuliboresha gazeti hilo hadi kufikia kiwango cha kuwa mpinzani mkubwa wa gazeti la Nipashe la Reginald Mengi.
Mwakiteleko sasa kapewa wadhifa wa kuwa Naibu mhariri Mkuu wa magazeti ya New Habari, hatua inayoonekana kama kumpandisha cheo. Lakini habari za uhakika ni kwamba kaondolewa kwa agizo kutoka kwa mmiliki, Rostam, baada ya kuona mauzo yanaporomoka sana tangu ashike gazeti hilo takriban miaka miwili iliyopita.
Ilikuwa ni wakati Rosemary Mwakitwange akiwa CEO wa kampuni na alimuajiri kutokana na umahiri wake na kwa mshahara mkubwa sana. Kuna baadhi wanasema Mwakiteleko alibadilika baada ya kuondoka kwa Rosemary ambaye alikosana na Rostam kuhusu suala la mwelekeo na sera za magazeti ya New Habari hasa katika masuala ya kundika habari za ufisadi.
Habari zinasema kwamba Rostam alimwambia Mhariri Mtendaji Muhingo Rweyemamu amuondoe Mwakiteleko kama mhariri wa Mtanzania na atafute pa kumweka, hivyo akaamua kumweka kuwa naibu wake.
Gazeti hilo, lililojijengea sifa kubwa miaka ya nyuma sasa linapitwa na karibu magazeti yote ya Kiswahili ya kila siku na sasa hivi meza nyingi za kuuzia magazeti hapa Dar halionekani. Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana.
Kuporomoka kwa Mtanzania (kama ilivyo kwa gazeti la kila wiki la RAI) linatokana na msimamo wake kuhusu masuala ya ufisadi – lilikuwa linajitambulisha sana na wale wote wanawatetea mafisadi – kwa bayana, lakini mara nyingi kwa ujanjaujanja tu. Inadaiwa kuwa stori nyingi za ukurasa wa mbele zilikuwa zinatokana na agizo la Rostam mwenyewe au washauri wake -- kama vile Salva Rweyemamu.
Mara nyingine stori hizo huwa zinaletwa nzima nzima dakika za mwisho kabla ya kwenda mtamboni na hubandikwa zilivyo. Mwakiteleko alikuwa akiridhia hivyo kwa sababu mbili – agizo kutoka juu, na kulinda mshahara wake mkubwa.
Kwa hivyo ni kitu cha kushangaza kuona Rostam amemgeuka Mwakiteleko ili hali yeye mwenyewe ndiyo sababu ya uzorotaji wa gazeti.
Lakini kuna maelezo mengine tofauti – kwamba wahariri wengi wa magazeti ya New Habari, hususan Mtanzania, Mtanzania Jumapili na RAI (kama vile Balile, Manyerere, Munyunku, Matinyi, Sarah Mosi, Mayage n.k.) hujipendekeza tu kwa Rostam katika kuandika stori wanazofikiria zitampendezesha yeye na zile wanazoona zinaweza kumsafisha katika matatizo yake yanayomuandama – hata kama ni kuwachafua watu wengine.
Kwa vyovyote vile, hali hii imeathiri sana magazeti hayo. Nafasi ya Mwakiteleko, Muhingo kamteua Balile kuwa mhariri wa Mtanzania, katika hatua ambayo wengi wanaona ni kuzidi kulididimiza gazeti hilo.
Habari zinasema kwamba kama Mwakiteleko alikuwa anatetea mafisadi kiujanjajanja, basi Balile atafanya hivyo kwa bayana kabisa.
Tungoje tuone.