Kuporomoka kwa magazeti ya Rostam

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Habari za kuaminika kutoka kampuni ya uchapishaji wa magazeti ya New Habari inayomilikiwa na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz zinasema kwamba gazeti la kila siku la Mtanzania limeporomoka mauzo kiasi kwamba mhariri wake Danny Mwakiteleko ameondolewa katika mabadiliko makubwa yaliyotangazwa mapema mwezi huu.

Kwa wanaomfahamu Mwakiteleko, kuporomoka kwa Mtanzania kimauzo hakuingii akilini kabisa -- hasa kutokana na umahiri wake – ikikumbukwa kwamba miaka kadha iliyopita alipokuwa mhariri wa gazeti la Majira aliweza kuliboresha gazeti hilo hadi kufikia kiwango cha kuwa mpinzani mkubwa wa gazeti la Nipashe la Reginald Mengi.

Mwakiteleko sasa kapewa wadhifa wa kuwa Naibu mhariri Mkuu wa magazeti ya New Habari, hatua inayoonekana kama kumpandisha cheo. Lakini habari za uhakika ni kwamba kaondolewa kwa agizo kutoka kwa mmiliki, Rostam, baada ya kuona mauzo yanaporomoka sana tangu ashike gazeti hilo takriban miaka miwili iliyopita.

Ilikuwa ni wakati Rosemary Mwakitwange akiwa CEO wa kampuni na alimuajiri kutokana na umahiri wake na kwa mshahara mkubwa sana. Kuna baadhi wanasema Mwakiteleko alibadilika baada ya kuondoka kwa Rosemary ambaye alikosana na Rostam kuhusu suala la mwelekeo na sera za magazeti ya New Habari hasa katika masuala ya kundika habari za ufisadi.

Habari zinasema kwamba Rostam alimwambia Mhariri Mtendaji Muhingo Rweyemamu amuondoe Mwakiteleko kama mhariri wa Mtanzania na atafute pa kumweka, hivyo akaamua kumweka kuwa naibu wake.

Gazeti hilo, lililojijengea sifa kubwa miaka ya nyuma sasa linapitwa na karibu magazeti yote ya Kiswahili ya kila siku na sasa hivi meza nyingi za kuuzia magazeti hapa Dar halionekani. Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana.

Kuporomoka kwa Mtanzania (kama ilivyo kwa gazeti la kila wiki la RAI) linatokana na msimamo wake kuhusu masuala ya ufisadi – lilikuwa linajitambulisha sana na wale wote wanawatetea mafisadi – kwa bayana, lakini mara nyingi kwa ujanjaujanja tu. Inadaiwa kuwa stori nyingi za ukurasa wa mbele zilikuwa zinatokana na agizo la Rostam mwenyewe au washauri wake -- kama vile Salva Rweyemamu.

Mara nyingine stori hizo huwa zinaletwa nzima nzima dakika za mwisho kabla ya kwenda mtamboni na hubandikwa zilivyo. Mwakiteleko alikuwa akiridhia hivyo kwa sababu mbili – agizo kutoka juu, na kulinda mshahara wake mkubwa.

Kwa hivyo ni kitu cha kushangaza kuona Rostam amemgeuka Mwakiteleko ili hali yeye mwenyewe ndiyo sababu ya uzorotaji wa gazeti.

Lakini kuna maelezo mengine tofauti – kwamba wahariri wengi wa magazeti ya New Habari, hususan Mtanzania, Mtanzania Jumapili na RAI (kama vile Balile, Manyerere, Munyunku, Matinyi, Sarah Mosi, Mayage n.k.) hujipendekeza tu kwa Rostam katika kuandika stori wanazofikiria zitampendezesha yeye na zile wanazoona zinaweza kumsafisha katika matatizo yake yanayomuandama – hata kama ni kuwachafua watu wengine.

Kwa vyovyote vile, hali hii imeathiri sana magazeti hayo. Nafasi ya Mwakiteleko, Muhingo kamteua Balile kuwa mhariri wa Mtanzania, katika hatua ambayo wengi wanaona ni kuzidi kulididimiza gazeti hilo.

Habari zinasema kwamba kama Mwakiteleko alikuwa anatetea mafisadi kiujanjajanja, basi Balile atafanya hivyo kwa bayana kabisa.

Tungoje tuone.
 
Hii habari mbona ipo ipo tu?, Rosemary Mwakitwange bado ni CEO wa New Habari cop.
 
Hii habari mbona ipo ipo tu?, Rosemary Mwakitwange bado ni CEO wa New Habari cop.


After all, hata yakiporomoka, who cares!.

Kuna magazeti mbadala meengi sana, ambayo yamejenga Heshima kubwa ya uandishi uliotukuka!

Hatutaki magazeti ya kuwapamba watu fulani na kuwaponda wengine, na yanayoandikwa kwa maelekezo ya MMILIKI! Shame on them!
 
Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana.

Mbona hii kidogo inanipa wasi wasi.....?
 
Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana

Hiki ndicho ulichotaka kukifikisha kwa wakulu naona umezunguka sana bwana jambo leo. Wabongo kwa usanii tu.
 
Hiki ndicho ulichotaka kukifikisha kwa wakulu naona umezunguka sana bwana jambo leo. Wabongo kwa usanii tu.
Yeah yeah,

Jamaa kaja kulitangaza gazeti la Jambo Leo ambalo JK ana hisa na kina Ben Kisaka na crew yake. Si mchezo
 
Hii kweli imekuja kutangaza Jambo Leo on expense ya Mtanzania. Uliyeleta hoja hujatulia na una-kaunafiki au unajifunza unafiki. Hata magazeti yakiporomoka, who cares? Ungekuja na hoja kuwa Watanzania hawapati habari hapo tungekuelewa na pia ungetuambia ni kwa vipi.
 
Habari za kuaminika kutoka kampuni ya uchapishaji wa magazeti ya New Habari inayomilikiwa na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz zinasema kwamba gazeti la kila siku la Mtanzania limeporomoka mauzo kiasi kwamba mhariri wake Danny Mwakiteleko ameondolewa katika mabadiliko makubwa yaliyotangazwa mapema mwezi huu.

Kwa wanaomfahamu Mwakiteleko, kuporomoka kwa Mtanzania kimauzo hakuingii akilini kabisa -- hasa kutokana na umahiri wake – ikikumbukwa kwamba miaka kadha iliyopita alipokuwa mhariri wa gazeti la Majira aliweza kuliboresha gazeti hilo hadi kufikia kiwango cha kuwa mpinzani mkubwa wa gazeti la Nipashe la Reginald Mengi.

Mwakiteleko sasa kapewa wadhifa wa kuwa Naibu mhariri Mkuu wa magazeti ya New Habari, hatua inayoonekana kama kumpandisha cheo. Lakini habari za uhakika ni kwamba kaondolewa kwa agizo kutoka kwa mmiliki, Rostam, baada ya kuona mauzo yanaporomoka sana tangu ashike gazeti hilo takriban miaka miwili iliyopita.

Ilikuwa ni wakati Rosemary Mwakitwange akiwa CEO wa kampuni na alimuajiri kutokana na umahiri wake na kwa mshahara mkubwa sana. Kuna baadhi wanasema Mwakiteleko alibadilika baada ya kuondoka kwa Rosemary ambaye alikosana na Rostam kuhusu suala la mwelekeo na sera za magazeti ya New Habari hasa katika masuala ya kundika habari za ufisadi.

Habari zinasema kwamba Rostam alimwambia Mhariri Mtendaji Muhingo Rweyemamu amuondoe Mwakiteleko kama mhariri wa Mtanzania na atafute pa kumweka, hivyo akaamua kumweka kuwa naibu wake.

Gazeti hilo, lililojijengea sifa kubwa miaka ya nyuma sasa linapitwa na karibu magazeti yote ya Kiswahili ya kila siku na sasa hivi meza nyingi za kuuzia magazeti hapa Dar halionekani. Linaanza pia kutishiwa na gazeti jipya la Jambo Leo ambalo ninakuja juu kwa kasi sana.

Kuporomoka kwa Mtanzania (kama ilivyo kwa gazeti la kila wiki la RAI) linatokana na msimamo wake kuhusu masuala ya ufisadi – lilikuwa linajitambulisha sana na wale wote wanawatetea mafisadi – kwa bayana, lakini mara nyingi kwa ujanjaujanja tu. Inadaiwa kuwa stori nyingi za ukurasa wa mbele zilikuwa zinatokana na agizo la Rostam mwenyewe au washauri wake -- kama vile Salva Rweyemamu.

Mara nyingine stori hizo huwa zinaletwa nzima nzima dakika za mwisho kabla ya kwenda mtamboni na hubandikwa zilivyo. Mwakiteleko alikuwa akiridhia hivyo kwa sababu mbili – agizo kutoka juu, na kulinda mshahara wake mkubwa.

Kwa hivyo ni kitu cha kushangaza kuona Rostam amemgeuka Mwakiteleko ili hali yeye mwenyewe ndiyo sababu ya uzorotaji wa gazeti.

Lakini kuna maelezo mengine tofauti – kwamba wahariri wengi wa magazeti ya New Habari, hususan Mtanzania, Mtanzania Jumapili na RAI (kama vile Balile, Manyerere, Munyunku, Matinyi, Sarah Mosi, Mayage n.k.) hujipendekeza tu kwa Rostam katika kuandika stori wanazofikiria zitampendezesha yeye na zile wanazoona zinaweza kumsafisha katika matatizo yake yanayomuandama – hata kama ni kuwachafua watu wengine.

Kwa vyovyote vile, hali hii imeathiri sana magazeti hayo. Nafasi ya Mwakiteleko, Muhingo kamteua Balile kuwa mhariri wa Mtanzania, katika hatua ambayo wengi wanaona ni kuzidi kulididimiza gazeti hilo.

Habari zinasema kwamba kama Mwakiteleko alikuwa anatetea mafisadi kiujanjajanja, basi Balile atafanya hivyo kwa bayana kabisa.

Tungoje tuone.


Pia kuna maelezo mengine ya kuondolewa kwa Mwakiteleko. Ni intrigue za Muhingo rweyemamu, Managing Editor. Kwa kuwa anamzidi mshahara ameona ni bora amtafutie njia ya kutokomea. Kampa ka-unaibu ka-geresha tu nafasi ambayo haina kazi pale mbali na kujisomea magazeti -- ili aondoke mwenyewe, ikishindikana ataondolewa tu.
 
Udaku siyo udaku, ukweli ni kwamba mabadiliko yametokea pale New habari, kampuni ambayo haijatulia tangu Rosemary aondoke kama CEO last year. na kuteuliwa kwa Balile kumrithi Mwakiteleko ni kama vile kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi. Huyo jamaa ni mlamba viatu ile mbaya!
 
Nyote mliochangia mada hii, pamoja na mtoa mada mwenyewe mnashangaza kweli kweli! Hivi nani aliwaambia kwamba Rostam aliinunua habaro Corporation kwa ajili ya kuongeza mauzo ya magazeti?
 
hii imekaa kuudaku zaidi.hapa sio mahali pake

Sawa kabisa. Hili ndilo tatizo la kuandika habari za hisia nakuzilemba kwa "habari zinasema" au "wachambuzi wa mambo ...." wakati mwandishi, mchambuzi na habari ni mtu yule yule. Tanzania Daima Jumapili katika ukurasa wake wa kwanza (lead strory) ni hivyo hivyo yaani ina habari za kiudaku.

Hata hivyo haishangazi Magazeti ya Rostam yakiporomoka. Hata katika barua ndefu toka kwa Salva Rweyemamu kwenda kwa Rostam (iliwekwa JF) ilionya hivyo. Mimi nina marafiki zangu ambao kamwe hawanunui magazeti ya New Habari Corporation kwa vile ni ya Rostam.
 
Hiki ndicho ulichotaka kukifikisha kwa wakulu naona umezunguka sana bwana jambo leo. Wabongo kwa usanii tu.

Naona vigumu kukubaliana nawe, pamoja na wachangiaji wengine, kwamba aim ya thread hii ni kulikweza Jambo Leo. Hivi Jambo Leo ndiyo mbaya mkuu wa Mtanzania? Au mnamaananisha kwamba kwa kuwa JK ana hisa ktk gazeti hilo la Jambo Leo (kitu cha tetesi tu kisicho na uthibitisho) basi ndiyo sasa anampiga vita 'king maker' wake?

Tuwe makini tunapojibu hoja, tusikurupuke tu.
 
After all, hata yakiporomoka, who cares!.

Kuna magazeti mbadala meengi sana, ambayo yamejenga Heshima kubwa ya uandishi uliotukuka!

Hatutaki magazeti ya kuwapamba watu fulani na kuwaponda wengine, na yanayoandikwa kwa maelekezo ya MMILIKI! Shame on them!

I totally agree with you PJ 101 % -- who cares if we are to see the last of those papers?
 
Hatuna independent journalists miaka yote!ndio maana tuna hali hii mpaka leo.Nchi zenye demokrasia ,magazeti yana play part vizuri sana hasa kama opposition parties ni weak.I guess wote hawa walisoma TSJ ,ambacho kilikuwa chuo cha propaganda cha TANU na SISIEM.Siwaamaini wa akina Tido Mhando,Makwaia wa Kuhenga na wengi wao.Hakuna investigative journalism,tangu lini mfisadi Rostam akaandikwa na magazeti yake?Hawa waandishi wake ni shame kwa wazawa watanzania
 
Udaku siyo udaku, ukweli ni kwamba mabadiliko yametokea pale New habari, kampuni ambayo haijatulia tangu Rosemary aondoke kama CEO last year. na kuteuliwa kwa Balile kumrithi Mwakiteleko ni kama vile kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi. Huyo jamaa ni mlamba viatu ile mbaya!

Rosemary Mwakitwange bado ni CEO wa habari cop. mpaka leo.
 
Back
Top Bottom