Kupimisha Kiwanja na kupata offer...

Kupimisha Kiwanja na kupata offer...

[QUO TE=CTU Kn t;11858986]Habari za jioni wana Jf.
Nina Kiwanja kidogo around 1000sqm nataka nipime nipate offer, jirani zangu wao swala lakupima hawataki kuliskia sasa nilitaka kujuaa kwa Kiwanja kidogo kama hicho process zinakua vp na gharama inakua aje?[/QUOTE]
Mimi siyo saveya lakini Kuna taratibu laZima upate,lazima uandike barua serikali ya mtaa ya kuomba upimiwe eneo lako, serikali ya mtaa nao wataandika barua kuthibitisha kuwa wee Ndiyo mmiliki wa eneo hilo wao wata sign, kwa mtandao wa kata pia wanafanya hivyo hivyo na wata sign....barua hizo zote utawasidia mkurugenzi wa manispa kuomba upimiwe.
Utamtafuta saveya atakuja na gps kuchukua coordinates ya hilo eneo ili ajue kwenye mchoro kuna nini...Kama mambo eneo safi
Un andika barua kutaka kupima. ..unaanza serikali ya mtaa hadi kwa mtandao na unaandika barua ya maombi kwa mkurugenzi wa manispa ....
Kuhusu bei ya Mali po ya saveya usiogope mtaelewana tu
 
Nahisi kuchanganyikiwa hapa, naomba kuelekezwa tena...Kiwanja changu cha 1000sqm kita ni cost bei gani na ipi process ya kuanzia ili nipate hati

Ndo madhara ya kukimbilia kuja kuulizia JF! Kuwa mpole! Ulishindwa nini kwenda kuulizia kwa watu ARDHI hapo mjini kwako? Hapa umekumbana na ma-solovea unaona sasa? Wengi wanaokushauri si watumishi Wa halmashauri ni watu waliosoma maswala ya ARDHI lakini wakabaki mitaani, hivyo wamebaki kudandia tu wakisikia MTU anataka kupimiwa kiwanja wanadanganya inawezekana! Ukweli ni kwamba ardhi wanapima kwa kufuata blocks. Hivyo utakavyowaendea kuhusu kupimiwa watakuuliza mko wangapi kwenye block yenu? Mimi huu nakupa maelekezo niliyopewa na Afisa ARDHI!!
 
Upimaji wa viwanja sekta husika ni ipo? Ardhi au manispaa? Mimi hapa ndipo nachanganyikiwa. Pesa analipwa mtu anayepima au ni pesa ya sekta husiika?? Wengi tuna shida na hii kitu ya kupima viwanja tunashindwa kujua nani ni mhusika halali wa upimaji wa viwanja maana nilishawahi Pima kiwanja na kumlipa pesa mtu wa ardhi lakini kwenda wizarani kulikuwa hakuna hati ya kiwanja wala faili. Matapeli wa viwanja ni mlolongo kuanzia upimaji uuzaji ununuaji umiliki nk Msaada tafadhali mwenye kujua suluhu la jambo hili.
 
Huyu anayekuambia 800000 kupima kiwanja sidhani kama ni surveyor. Kupima kiwanja hadi unapata plani yako ni kuanzia 2000000,chini ya hapo mtazimiana simu. Kama ni nje ya dsm bei hiyo inawezekana. Ni mimi suryeyor nimemaliza 2005 na Bsc in Geomatics

Nakubaliana na wewe,mimi mpaka sasa nimebwagiwa mawe hapa nyumbani huu mwezi wa sita sielewi kinachoendelea. Nchi hii ina vituko sijapata ona.
 
Upimaji wa viwanja sekta husika ni ipo? Ardhi au manispaa? Mimi hapa ndipo nachanganyikiwa. Pesa analipwa mtu anayepima au ni pesa ya sekta husiika?? Wengi tuna shida na hii kitu ya kupima viwanja tunashindwa kujua nani ni mhusika halali wa upimaji wa viwanja maana nilishawahi Pima kiwanja na kumlipa pesa mtu wa ardhi lakini kwenda wizarani kulikuwa hakuna hati ya kiwanja wala faili. Matapeli wa viwanja ni mlolongo kuanzia upimaji uuzaji ununuaji umiliki nk Msaada tafadhali mwenye kujua suluhu la jambo hili.

Survexor yeyote anaweza kupima kiwanja. Yeye anafuata taratibu zilizowekwa,ardhi na manispa kote kuna surveyors,hata kama anayepima ni kutoka ardh au private ni lazima apate ruhusa toka manispaa au halmashauri. Kila sehemu kuna mtapeli TRA,polisi,mahakamani,n.k si sekta ya ardh tu,muhimu ni wewe uwe makini na watu unaodeal nao
 
Nakubaliana na wewe,mimi mpaka sasa nimebwagiwa mawe hapa nyumbani huu mwezi wa sita sielewi kinachoendelea. Nchi hii ina vituko sijapata ona.

Manispaa gani. Surveyor gani. Unaweza kuwa umemchukua mtu wa mtaani tu. Anaweza akawa pale ardh au manispaa kumbe si surveyor.
 
Ndo madhara ya kukimbilia kuja kuulizia JF! Kuwa mpole! Ulishindwa nini kwenda kuulizia kwa watu ARDHI hapo mjini kwako? Hapa umekumbana na ma-solovea unaona sasa? Wengi wanaokushauri si watumishi Wa halmashauri ni watu waliosoma maswala ya ARDHI lakini wakabaki mitaani, hivyo wamebaki kudandia tu wakisikia MTU anataka kupimiwa kiwanja wanadanganya inawezekana! Ukweli ni kwamba ardhi wanapima kwa kufuata blocks. Hivyo utakavyowaendea kuhusu kupimiwa watakuuliza mko wangapi kwenye block yenu? Mimi huu nakupa maelekezo niliyopewa na Afisa ARDHI!!

Nimekuambia sibishani kitoto,mimi ni surveyor nafanya kazi serikalini,ofisa ardh hausiki na gharama za upimaji,bali anahusika na garama za umilikishaji ambazo ni ndogo sana,unapoongea ujinga wakati watu wanataka kujua inaonesha how iliterate you are. Kupima kiwanja bei ya serikali kwa hapa dar ni 2000@sqm. Kama umemuuliza huyo kishoka wako mbona hutuelezi wanafanyaje.
 
Gharama za upimaji zina tegemea mambo makuu mawili
1. Kama Eneo lako lipo kwenye ramani ya mipango miji

2. Ukubwa wa eneo lako

Kama eneo ambapo kiwanja kipo Hakuna city plan Au ramani ya mipango miji basi ujue gharama itakuwa si chini ya 3M, sababu itabidi ulipie mchoro wa mipango miji uchorwe na kupitishwa ardhi. Gharama za kuchora huo mchoro ni 4M Sababu inabidi uhonge. Kama eneo lina city plan then Hiyo gharama unakuwa umeiepuka

Ukishapata mchoro ndio zoezi la kugawa eneo lako na kuweka mawe linafuata, hili zoezi hufanywa na surveyor yoyote na bei yake inategemea na ukubwa wa eneo lako. Kama eneo lako Ni kubwa litatoa viwanja vingi bei inakuwa ndongo kwa kila Kiwanja Lakini kama eneo dogo basi bei kwa kiwanja inakuwa kubwa. Kwa kawaida bei ina tofautiana kati ya surveyor na surveyor

NB: Hizo estimate za bei ni kwa dar kwahiyo mikoani zinaweza kuwa tofauti.
 
Stesheni 2005 kulikuwa hakuna Bsc in Geomatics Bali Land Surveying. Wakati huo tuliwaita LS mi nilikuwa LMV.

Umemkamata vibaya!!.Ha ha ha aaah!!
Mimi nilimaliza 2005 B Arch! Geomatics ilikuwa bado!
 
Nchi hii kupima viwanja ni anasa....

Nina ekari 40 mkuranga hapo nataka pima viwanja ...

Baada ya kuleta surveya wa halmashauri bei waliyonipa.....nimepumzisha akili kidogo!!! Na zoezi nalitafakari upya.

Ndio maana squatters nchi hii hazitoisha
 
Mimi naomba kuuliza ma surveyor. Kuna eneo langu nilitaka kulipima na nimwashajenga. Ila baada ya kuchukua vipimo linaonyesha lipo kwenye OPEN SPACE. Niliongea na surveyor akanambia kuliondoa kwenye open space inawezekana ila ni gharama kubwa. Je ilo swala linawezekana?
 
Gharama za upimaji zina tegemea mambo makuu mawili
1. Kama Eneo lako lipo kwenye ramani ya mipango miji

2. Ukubwa wa eneo lako

Kama eneo ambapo kiwanja kipo Hakuna city plan Au ramani ya mipango miji basi ujue gharama itakuwa si chini ya 3M, sababu itabidi ulipie mchoro wa mipango miji uchorwe na kupitishwa ardhi. Gharama za kuchora huo mchoro ni 4M Sababu inabidi uhonge. Kama eneo lina city plan then Hiyo gharama unakuwa umeiepuka

Ukishapata mchoro ndio zoezi la kugawa eneo lako na kuweka mawe linafuata, hili zoezi hufanywa na surveyor yoyote na bei yake inategemea na ukubwa wa eneo lako. Kama eneo lako Ni kubwa litatoa viwanja vingi bei inakuwa ndongo kwa kila Kiwanja Lakini kama eneo dogo basi bei kwa kiwanja inakuwa kubwa. Kwa kawaida bei ina tofautiana kati ya surveyor na surveyor

NB: Hizo estimate za bei ni kwa dar kwahiyo mikoani zinaweza kuwa tofauti.

Kama kiwanja kiko kwenye surveyed area, gharama zinazobaki ni zipi?
 
Mimi naomba kuuliza ma surveyor. Kuna eneo langu nilitaka kulipima na nimwashajenga. Ila baada ya kuchukua vipimo linaonyesha lipo kwenye OPEN SPACE. Niliongea na surveyor akanambia kuliondoa kwenye open space inawezekana ila ni gharama kubwa. Je ilo swala linawezekana?

Pole ndugu hilo swali halihitaji surveyor kujibu.Open space lazima iwepo eneo husika, wakitoa kwako watapata wapi kwingine pakueka open space? Maanake wamnyanganye mwingine kiwanja.Subiri kulipwa fidia ya nyumba yako.Kama nyumba haijaisha sitisha process za kujenga.
 
Mimi naomba kuuliza ma surveyor. Kuna eneo langu nilitaka kulipima na nimwashajenga. Ila baada ya kuchukua vipimo linaonyesha lipo kwenye OPEN SPACE. Niliongea na surveyor akanambia kuliondoa kwenye open space inawezekana ila ni gharama kubwa. Je ilo swala linawezekana?

Kama vile surveya anataka kukuingiza mjini...
 
Pole ndugu hilo swali halihitaji surveyor kujibu.Open space lazima iwepo eneo husika, wakitoa kwako watapata wapi kwingine pakueka open space? Maanake wamnyanganye mwingine kiwanja.Subiri kulipwa fidia ya nyumba yako.Kama nyumba haijaisha sitisha process za kujenga.

Ameniambia uo mchoro bado haujapitishwa na mkurugenzi wa halmashauri. Na iyo open space anaweza akaamisha kwa mwingine. Nyumba ndio naifanyia finishing
 
Nimekuambia sibishani kitoto,mimi ni surveyor nafanya kazi serikalini,ofisa ardh hausiki na gharama za upimaji,bali anahusika na garama za umilikishaji ambazo ni ndogo sana,unapoongea ujinga wakati watu wanataka kujua inaonesha how iliterate you are. Kupima kiwanja bei ya serikali kwa hapa dar ni 2000@sqm. Kama umemuuliza huyo kishoka wako mbona hutuelezi wanafanyaje.

Wewe ni mjinga huna lolote, inakuwaje unamdanganya kwamba anaweza kupimiwa kiwanja chake peke yake? Unafikri serikali ni mataahira kama Wewe waruhusu usumbufu kama huo unaotaka kumpatia huyo mdau? Nimekwambia hizo gharama unazompa ni za kupima block nzima pumb.a mkubwa!!
 
Umemkamata vibaya!!.Ha ha ha aaah!!
Mimi nilimaliza 2005 B Arch! Geomatics ilikuwa bado!

Kuna watu humu wana mtindio. Nitatoa ushahidi kwamba Bsc in GM imeanza kutoka 2005.
 
Nina eneo la miguu 43 kwa 23, nilicheki mchoro katikati kuna barabara imepita, upande mmoja open space na upande mwingine makazi ya watu, hapo vipi?
 
Kama kiwanja kiko kwenye surveyed area, gharama zinazobaki ni zipi?

Kupata kibali cha halmashauri na Kuweka mawe, kwahiyo ni gharama Kidogo za halmshauri na za surveyor kwa ajili ya kugawa na kuchora eneo lako.
 
Back
Top Bottom