Kupimisha Kiwanja na kupata offer...

Kupimisha Kiwanja na kupata offer...

Labda nitoe mfano ulio hai kabisa na current hapa nilipo;sisi tumejikusanya kama watu 5 na tuna jumla ya ekari 14 na Mara baada ya vipimo vya shamba zima Kwa eneo LA ekari hizo 14 tumepata viwanja 22 na mpimaji amesema kila kiwanja kimoja tumpatie laki mbili unusu je ni sahihi kweli au anatupiga huyu jamaa?

Ni sahihi kabisa hiyo
 
Lol!!! Umevamia Treji Kwa Mbele, Inawezekana Wewe Ni Kanjanja Wa Elimu Ona Wenye Taaluma Wanavyokuumbua, Tuambie Hiyo BSC Ya Geomatic Umeipatia Wapi??

Huyo anayesema amesoma lmv muulize vizuri inawezekana ana certificate. Waliomaliza chuo mwaka 2005 ndio wa kwanza kupata Bsc in Geomatics. Mimi naelewesha na sifanyi ubishi wa kitoto huo.
 
Huyu anayekuambia 800000 kupima kiwanja sidhani kama ni surveyor. Kupima kiwanja hadi unapata plani yako ni kuanzia 2000000,chini ya hapo mtazimiana simu. Kama ni nje ya dsm bei hiyo inawezekana. Ni mimi suryeyor nimemaliza 2005 na Bsc in Geomatics

Tuelimishe bwana, mbona wanasema huwezi kupima kiwanja kimoja kimoja mpaka mjiunge wengi! Is this true? If not process ya kuomba kupimiwa ikoje maana no body tells what actually the process is/or seems to know even those in the field. Msaada tueleweshe
 
Tuelimishe bwana, mbona wanasema huwezi kupima kiwanja kimoja kimoja mpaka mjiunge wengi! Is this true? If not process ya kuomba kupimiwa ikoje maana no body tells what actually the process is/or seems to know even those in the field. Msaada tueleweshe

Kiwanja kimoja kinapimwa,muhimu kiendane na jinsi ramani ilivyo.
 
Uliuliza ramani ipi? Survey ya ramani ya viwanja inaitwa cadastral survey.
 
Kila mtu ana ushuhuda wake hapa, sasa sijui kama tunaweza kumsaidia ndugu yetu au la but upimaji kwa sasa ni biashara kabisa hivyo tukienda kichwa kichwa tutapigwa ile mbaya. Mimi nimeanza process za kwanza, shamba lipo kibaha ekari 4, umbali wa 12kms kutoka barabarani kuu, jamaa kuja kulipima na kuchora mchoro tu amekula laki 8. Ananiambia mchoro sasa unatakiwa kupelekwa Kisarawe wilayani kwa planner naye anakazi yake ataniambia gharama zake lakini zitakuwa sio chini ya milioni 3. Hapo sijui nimepatwa au ndio hiyo sawa tu?
 
Habari za jioni wana Jf.
Nina Kiwanja kidogo around 1000sqm nataka nipime nipate offer, jirani zangu wao swala lakupima hawataki kuliskia sasa nilitaka kujuaa kwa Kiwanja kidogo kama hicho process zinakua vp na gharama inakua aje?
Samahani naomba kueleweshwa hizi law density, medium na high density range zake katika sq. meter zinakwendaje? yaani nikitaka kupima shamba langu zima liwe na viwanja vya low density kwa heka moja nitapata viwanja vingapi?
 
Huyu anayekuambia 800000 kupima kiwanja sidhani kama ni surveyor. Kupima kiwanja hadi unapata plani yako ni kuanzia 2000000,chini ya hapo mtazimiana simu. Kama ni nje ya dsm bei hiyo inawezekana. Ni mimi suryeyor nimemaliza 2005 na Bsc in Geomatics

Umedanganya hapo.........geomatics haikuwepo 2005....labda kama hukusoma tz
 
Kila mtu ana ushuhuda wake hapa, sasa sijui kama tunaweza kumsaidia ndugu yetu au la but upimaji kwa sasa ni biashara kabisa hivyo tukienda kichwa kichwa tutapigwa ile mbaya. Mimi nimeanza process za kwanza, shamba lipo kibaha ekari 4, umbali wa 12kms kutoka barabarani kuu, jamaa kuja kulipima na kuchora mchoro tu amekula laki 8. Ananiambia mchoro sasa unatakiwa kupelekwa Kisarawe wilayani kwa planner naye anakazi yake ataniambia gharama zake lakini zitakuwa sio chini ya milioni 3. Hapo sijui nimepatwa au ndio hiyo sawa tu?

Gharama alizokuambia ni sahihi.
 
Samahani naomba kueleweshwa hizi law density, medium na high density range zake katika sq. meter zinakwendaje? yaani nikitaka kupima shamba langu zima liwe na viwanja vya low density kwa heka moja nitapata viwanja vingapi?

High density=400-600
Medium density=601-999
Low density=1000-
 
Umedanganya hapo.........geomatics haikuwepo 2005....labda kama hukusoma tz

Nimegundua nachat na mtu hatasona UCLAS. Mimi nimeanza chuo 2001-2005,sasa wewe ndio maana niliuliza umesoma enzi za diploma? Nilishakuambia sifanyi ushindani wa kitoto.
 
High density=400-600
Medium density=601-999
Low density=1000-
Asante sana. Shamba la heka moja najua lina 4900 sqm., pakitolewa barabara hapo naweza kubaki na 2000sqm.? Hivyo heka 4 nikapata 8,000 sqm.?
 
Nahisi kuchanganyikiwa hapa, naomba kuelekezwa tena...Kiwanja changu cha 1000sqm kita ni cost bei gani na ipi process ya kuanzia ili nipate hati
 
Nahisi kuchanganyikiwa hapa, naomba kuelekezwa tena...Kiwanja changu cha 1000sqm kita ni cost bei gani na ipi process ya kuanzia ili nipate hati
Pole ndugu yangu, nililiona mwanzo sana hilo, nahisi hakuna jibu la moja kwa moja kuhusu gharama, zinatofautiana kwa mtu na mtu na sehemu uliyopo. Ukipenda kumjaribu huyo jamaa niliyemtumia mimi nitumie ujumbe wa private nikupe namba zake umtafute. But in short changanua katika maongezi hayo yote utapata in avarage ni kiasi gani.
 
Ekari moja ni 4047sqm na si 4900
Ooooooh!!! thanks nimejifunza kitu hapo thanks again. Kila siku najifariji najua kwamba heka moja ni mita 70 kwa 70 hivyo heka moja ni 4,900 sqm. Thanks kamanda.
 
Sasa nyinyi badala ya kuelimisha mnaanza kutisha watu kwa vielimu vyenu .
 
.. CTU Agent ngoja nikupe maelezo labda itakusaidia! Kwanza ningependa kujua Kiwanja chako kipo eneo gani/will ya gani
Nijibu alafu n nitarudi tena mkuu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom