Kupenda ni mara moja tu, haya mahusiano mengine nikuigiziana tu!

Attelan

JF-Expert Member
Oct 12, 2023
434
700
Habari kwa wanajukwaa wote. Tukiwa tunaugulia matokeo yaliyopatikana katika mchezo wa mpira wa miguu kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zambia tuliangazie hili jambo kwa ufupi kidogo.

Japo wengi watabisha ila ukweli ni kwamba moyo unapenda mara moja tu (tena humpenda mtu fulani tu), baada ya hapo hata ukimpata mtu mwingine na mkaanzisha mahusiano ambayo yanaonekana kuwa yenye afya mnaishia kuigiziana tu.

Kuna watu wengi wapo katika mahusiano lakini karibia robo tatu ya mioyo yao imegoma kutoka kwa watu waliowapenda kwa dhati hapo awali na wanajikuta wanavumilia tu ili kusongesha maisha.
 
Habari kwa wanajukwaa wote. Tukiwa tunaugulia matokeo yaliyopatikana katika mchezo wa mpira wa miguu kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zambia tuliangazie hili jambo kwa ufupi kidogo.

Japo wengi watabisha ila ukweli ni kwamba moyo unapenda mara moja tu (tena humpenda mtu fulani tu), baada ya hapo hata ukimpata mtu mwingine na mkaanzisha mahusiano ambayo yanaonekana kuwa yenye afya mnaishia kuigiziana tu.

Kuna watu wengi wapo katika mahusiano lakini karibia robo tatu ya mioyo yao imegoma kutoka kwa watu waliowapenda kwa dhati hapo awali na wanajikuta wanavumilia tu ili kusongesha maisha.
Tayar kishalia huko
 
Hakuna upendo unaojengwa muda mfupi, ile hali uliyojisikia kwa mpenzi wako wa kwanza mkatoana bikira au maumivu ya kuachwa na mpenzi wako aliyekukosha ambaye mmekuwa pamoja chini ya miaka 3 sio upendo, ni kemikali za mvuto za kihisia zilizoambatana na urafiki.
 
Kwa msichana, mtu aliyeondoa usichana wake ndiye mpenzi wake wa dhati. Hata akiolewa na mtu mwingine pendo lake bado lipo kwa yule wa mwanzo. Ndio maana kuna usemi kuwa "wanaume wengi tunaoa wake za watu" kama hukumkuta bikira basi basi ujue sio mke wako.
Ts not about sex. Ts about responsibilities plus utii wa kiapo plus hofu ya MUNGU.

Yaani hivi vikiwepo hata ukioa ambaye ameshazaa hiyo ndoa itadumu. Visipokuwepo hata ukioa bikra ndoa itavunjika.
 
Kwa msichana, mtu aliyeondoa usichana wake ndiye mpenzi wake wa dhati. Hata akiolewa na mtu mwingine pendo lake bado lipo kwa yule wa mwanzo. Ndio maana kuna usemi kuwa "wanaume wengi tunaoa wake za watu"kama hukumkuta bikira basi basi ujue sio mke wako.[/COLOR]

Na hapo ndipo kwenye tatizo
 
Kwa msichana, mtu aliyeondoa usichana wake ndiye mpenzi wake wa dhati. Hata akiolewa na mtu mwingine pendo lake bado lipo kwa yule wa mwanzo. Ndio maana kuna usemi kuwa "wanaume wengi tunaoa wake za watu" kama hukumkuta bikira basi basi ujue sio mke wako.
Hii sio kweli mkuu.

Kuna wengine walijikuta tu wamebikiriwa na hawakuwai rudia tena hayo mambo na hao watu

Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
 
Kwa msichana, mtu aliyeondoa usichana wake ndiye mpenzi wake wa dhati. Hata akiolewa na mtu mwingine pendo lake bado lipo kwa yule wa mwanzo. Ndio maana kuna usemi kuwa "wanaume wengi tunaoa wake za watu" kama hukumkuta bikira basi basi ujue sio mke wako.
Hujui chochote .mademu weng wanatolewa bikra sabab wamechoka kuwa nayo na wanataka kuanza mizagamuo haraka iwezekanavyo..so weng wanatolewa na random people..

Ila kuna wale ambao wanajitunza kusubiria the right person..hao nikwel akipata mtu anataka awe amempenda kwel na ndo anampa tunda hao ni kwel huwa hawamsahau huyo mtu .

Mim nilibahatika kuwa na huyo mtu niliemtoa bikra akiwa na miaka 20 chuo kikuu na ni pisi kal kwel..tulidum kwenye mahusiano karibia miaka 4 na tulikua tunavimbwanga kwelkwel..tunaachana na kurudiana kila siku..wivu uliopitiliza baina yetu...
Mwisho wa siku long distance ilikuja kutuachanisha..karibia miaka 11 imepita sasa tuko mbal mbal sana ila tunawasiliana mpaka leo na ukiona chat zetu unaweza hisi ni wapenz..na hajaolewa na mim sijaoa na umri wetu umekwenda kwel kwel.nakila mmoja ana mpenz wake..ila yeye ananambia anapitia mahusiano mabovu maisha yake yote tokea niachane nae na hana raha..ila ndo hvyo hatuwez tena kuwa pa1..tuko mbal mbal sana..different continents.
Ni hayo
 
Kwa msichana, mtu aliyeondoa usichana wake ndiye mpenzi wake wa dhati. Hata akiolewa na mtu mwingine pendo lake bado lipo kwa yule wa mwanzo. Ndio maana kuna usemi kuwa "wanaume wengi tunaoa wake za watu" kama hukumkuta bikira basi basi ujue sio mke wako.
Nakataa,mpenz wa mwanzo mkishaachana na habari yake inaisha....ex ni ex tu...hakuna cha baba mtoto au mtoa damu...wengine walibakwa na wajomba zao na kuondolewa bikra...msikariri maisha....MTU sahihi ni yule uliyenae mpaka muda huu ninaondika,mkiachana imeisha hiyo
 
Nakataa,mpenz wa mwanzo mkishaachana na habari yake inaisha....ex ni ex tu...hakuna cha baba mtoto au mtoa damu...wengine walibakwa na wajomba zao na kuondolewa bikra...msikariri maisha....MTU sahihi ni yule uliyenae mpaka muda huu ninaondika,mkiachana imeisha hiyo
Naunga mkono hoja
 
Back
Top Bottom