NYANGESON
::
Hongera maana karibuni utaitwa baba,umewazidi wagumba,matasa,wauaji wa kushiriki kutoa mimba,,umetimiza agizo la Mungu kwa viumbe wote!
::
Kuhusu kukosa kazi isiwe sababu ya kumtelekeza mkeo,,kwa maana unaweza kuishi nae ingali unatafuta kazi,au ukawaomba kwao wavute subira wakati unatafuta kazi,au ukaomba shangazi,mama au ndugu yako yeyote unaemwamini awe na mkeo kwa muda.
::
Ni kipindi cha mpito hivyo uvumilivu ni jambo la lazima.Usiwe baba kisayansi tu bali kimalezi pia kwa familia yako.
::
Kumbuka,,Mungu atakupunguzia vikwazo vingine ili utimize jukumu hili.Toka jasho mwanaume,ndio amri tuliyopewa.
::
KILA LA KHERI
=