Kuongea na Watoto Wetu kuhusu Misuko suko ya Mapenzi. . . .

Kuongea na Watoto Wetu kuhusu Misuko suko ya Mapenzi. . . .

Kongosho

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2011
Posts
35,987
Reaction score
24,233
Narejea uzi huu
Mwanafuni UDSM ajinyonga leo asubuhi.

Kuna sehem nineona sababu ya kujiua ni kuachwa na mpenzi.
Najariu kuvaa viatu vya mzazi, natetemeka, naona giza, nachanganyikiwa, nakiri siviwezi, vimenishinda.

Na-imagine first born, mzazi ana matumaini ya kuanza kula matunda ya jasho lake
Na-imagine labda anaanza kuwaza kubeba wajukuu wa kijana wake
Mara ghafla anampokea mwanaye kwenye jeneza kwa kujiua sababu ya mapenzi?

Je, angepata wasaa wa kuongea naye kabla ya hajajitundika, angeongea vingapi?
Ni aje angejaribu to make sense kwenye kichwa cha mtoto wake kuwa at some point mapenzi yanaumiza, bila kujali anayekuumiza unampenda kiasi gani?
Ni aje angejaribu kumwelewesha kuwa siku moja he will get over it?


Labda niulize,
Kuna haja ya kuongea na watoto wetu kuhusu hisia za mapenzi?? NAjua wengi tunakazania upande wa kiafya zaidi tunasahau hisia

Na je, kumweleza mtoto siku moja anaweza umizwa itamsaidia ku-cope siku akiumizwa?

Jamani mie nimeguswa sana na hilo, sijui sababu i have them boyz tu.
Msaada wadau
 
kuhusu kutndwa na kumudu au kuongoza hisia ni tofauti kwaa kila mtu kuna wengine wanaweza na kuna wengine hawawezi kuhusu kuongea nao itabidi pia kuwa muangalifu na mienendo yake pia itaweza kukusaidia nini kifanyike..
 
watoto wa siku hizi wanajua mambo mapema.....heri kuzungumza nao...zaidi mfundishe wajithamini wenyewe kwanza
 
kuna haja tena haja kubwa ila pia vizuri kuruhusu watoto wajimix na wenzao wanaone dunia inaendaje. watoto wa kiume unawafungia ndani kisa??? ndo maana wengine wanakuwa malonya lonya. yaani kwa wazazi wanaaoona noma watafute hata maconsultant wa nje.
 
Hao wasioweza sio kwamba wanakuwa hawana nyenzo sahihi za kujilinda??

kuhusu kutndwa na kumudu au kuongoza hisia ni tofauti kwaa kila mtu kuna wengine wanaweza na kuna wengine hawawezi kuhusu kuongea nao itabidi pia kuwa muangalifu na mienendo yake pia itaweza kukusaidia nini kifanyike..
 
Consultant siamini sana

Huwa naamini neno la mzazi linadumu sana kichwani mwa mtoto

Hasa unapompa case study zinazokuhusu wewe mwenyewe

kuna haja tena haja kubwa ila pia vizuri kuruhusu watoto wajimix na wenzao wanaone dunia inaendaje. watoto wa kiume unawafungia ndani kisa??? ndo maana wengine wanakuwa malonya lonya. yaani kwa wazazi wanaaoona noma watafute hata maconsultant wa nje.
 
Kabla hajaanza wewe anza kumweleza kwa dozi inayomtosha

Usi-over do

watoto wa siku hizi wanajua mambo mapema.....heri kuzungumza nao...zaidi mfundishe wajithamini wenyewe kwanza
 
Labda niulize,
Kuna haja ya kuongea na watoto wetu kuhusu hisia za mapenzi?? NAjua wengi tunakazania upande wa kiafya zaidi tunasahau hisia

Ndiyo, haja ipo tena sana tu. Na hii inatekelezeka zaidi kama umejenga uhusiano mzuri na mwanao/wanao.

Kwa uhusiano mzuri namaanisha huyo mwanao au hao wanao wakuone wewe mzazi kama a close/trusted confidant ambaye wanaweza kuja kwako na kuongea na wewe kuhusu chochote kile kinachowasibu hususan mambo ya kidunia/ mapenzi (wakishafikisha umri wa ku-date).

Mimi mshua ndiyo alikuwa confidant wangu. Na ameniongoza kwenye mambo mengi sana. Na mimi sasa hivi kama mzazi ndivyo ninavyofanya - ingawa kiddo wangu bado hajafikia wakati wa kuanza kuwa na vi-boyfriend.

Naamini kabisa mzazi ukianza kujenga mahusiano ya karibu na wanao utaweza kuwapa miongozo mizuri, kuwatia moyo pale wanapokuwa wamevunjika moyo, na kuwajaza imani ya wao kujiamini katika uwezo wao wa kukabiliana na masahibu ya dunia hii.

Na je, kumweleza mtoto siku moja anaweza umizwa itamsaidia ku-cope siku akiumizwa?

Ndiyo, nadhani inasaidia sana hususan kama huyo mtoto anakuamini wewe kuwa ni mtu ambaye una uzoefu na tajiriba nyingi kuhusu maisha.

Kwa sababu, kama akikujia na tatizo la kuachwa na mpenziye, kwa mfano, utamwambia tu 'mama, hiyo ni moja tu ya changamoto za kibinadamu. Hata mimi daddy'ako nimeyapitia pia lakini sikukata tamaa na maisha. Ndiyo, nilivunjika moyo, tena sana tu. Lakini nikapiga moyo konde na kusonga mbele. Hata wewe princess unaweza pia. When life hands you lemons you make lemonade out of them and at the end of the day, with the passage of time, you'll be fine. Trust what I'm telling you sweetheart. I've been there and done that. If I did it, you can do it too.'

Na kama mwanao anajua bila ya shaka kwamba you are always there for him/her. And that you'll listen, empathize, guide, encourage, and above all love unconditionally, basi imani yangu ni kwamba wewe kama mzazi utakuwa msaada mkubwa sana kwake.
 
Imefika kipindi tuwafanye watoto wetu waelewe kuwa they are unique and very special.
Hakuna chochote chenye thamani zaidi ya maisha yake for any how.
Tukiwa specific sana kwenye kumwelimisha juu ya hisia za mapenzi, unaweza ukaletewa akiwa kwenye jeneza kajiua kisa amefeli mitihani yake. u see!!
 
so sad kwa kweli!
ila sasa mawasiliano kati ya mzazi na kijana hayaanzii juuu!
mawasiliano ni pamoja na mzazi kujenga urafiki na kuaminiwa na mtoto!
kiasi anakuwa wazi ahata kushare some of her/his secrets!
ni ngumu ukiiweka kihalisia but kwa aina ya watoto na dunia tuliyopo wazazi ni lazima tufanya mhamo wa ruwaza wa kimalezi pia!
sijui tunalimudu na kulitekeleza hili vipi as for now majumbani kumekuwa kama changing room ya wazazi!
sijui i see tuna changamoto nying sana kama wazazi!
wakati mwingine watoto wetu wanaingia kwenye mahusiano mapema na kwa devoteness kubwa hiv kujazia magap amabyo sisi kama wazazi tumeyaweka!

kijana/binti anakuwa hajawahi hata kuambiwa anapendwa na mzazi wake
hajui hata maana ya kuridhika kwa mzazi kwa jema alilofaanya kunafananaje
hajui hata kuwa disappointed ni kupi(si tunafukia mashimo kwa kutoa pesa hata birthday tu za watoto tunawapeleka kwenye event organaizas sasa lini huyu mtoto atajua uzuri wa kuletewa maua?

sijui nawaza tu kwa sauti!
wazazi hili linatuhusu sana,tunasaka sana hela na kusahau kuwa mwisho wa siku hata hizo hela hazitakuwa na wa kuzitumia since hata kama watoto wetu hawatakubwa na majanga ya aina hii watakumbwa na janga lingine na KUTUONA SISI NI WATU BAKI!

ah!inaumiza i see!
nisameheni sana wanangu nawapenda sana lakn nahs mahala fulani nawadisappoint as a mother!
 
Nyani Ngabu, nimekupata

Kweli kujenga uaminifu kwa mtoto ni muhimu, na inasaidia kunwelewesha.

Ila nilichojifunza ni kuwa, wakati mwingine tunadhani watoto bado ni wadogoo sana, lakini huko duniani kuna wengine wanawaona wakubwa wenzao.

Umri wa kuanza kumweleza ni tricky sana, dunia haiko fair kabisa.

Asante kwa mchango wako, umeshiba.
 
Last edited by a moderator:
Nimekupata point yako, changamoto ni nyingi kwa kweli

Imefika kipindi tuwafanye watoto wetu waelewe kuwa they are unique and very special.
Hakuna chochote chenye thamani zaidi ya maisha yake for any how.
Tukiwa specific sana kwenye kumwelimisha juu ya hisia za mapenzi, unaweza ukaletewa akiwa kwenye jeneza kajiua kisa amefeli mitihani yake. u see!!
 
snowhite umeona eeh!

Tunakimbizana na hela na tunasahau jukumu kuu, mtu hapimwi kwa pesa zake bali kwa aina ya familia aliyotengeneza.

Itabidi nifanye mapinduzi makubwa!
 
Last edited by a moderator:
snowhite umeona eeh!

Tunakimbizana na hela na tunasahau jukumu kuu, mtu hapimwi kwa pesa zake bali kwa aina ya familia aliyotengeneza.

Itabidi nifanye mapinduzi makubwa!
we acha tu!
jana binti zangu walinityt mahali nilikomaje!walihakikisha natumia siku nzima kwa ajili yao,full madai yaso na kichwa wala miguu na demand za ajabu kabisa!plus kulala nao!
niliisoma kimya kimya kuwa heee mum ur not seen jamani!hebu kuja hapa!tupikie hiki,tunyoshee nguo,twende tukanunue vitumbua sijui wapi ,mimi daftar zangu hazina covers,sijui hebu soma hii insha yangu,kubwa kuliko leo tunalala wote chumbani kwetu!
niliwaelewa kwa kweli!mweh!
ngoja na mi nifanye mapinduzi manake unamissika na watoto mpka aibu!
 
Mie kuna wakati nilifululiza rudi home night

Siku moja akaniambia, leo tunaenda wote huko unakokwenda. Eti naona siku hizi hutupendi tena, nlikuwa mdogo kama pirton.

we acha tu!
jana binti zangu walinityt mahali nilikomaje!walihakikisha natumia siku nzima kwa ajili yao,full madai yaso na kichwa wala miguu na demand za ajabu kabisa!plus kulala nao!
niliisoma kimya kimya kuwa heee mum ur not seen jamani!hebu kuja hapa!tupikie hiki,tunyoshee nguo,twende tukanunue vitumbua sijui wapi ,mimi daftar zangu hazina covers,sijui hebu soma hii insha yangu,kubwa kuliko leo tunalala wote chumbani kwetu!
niliwaelewa kwa kweli!mweh!
ngoja na mi nifanye mapinduzi manake unamissika na watoto mpka aibu!
 
ila Kongosho kuwa
mwanamke
mke
mama
mfanyakazi
mkamwana
wifi
shemeji
dada
ni kazi sana ujue ,tunapaswa sana kumuomba Mungu sana!MNO ili tunaposhindwa kwa nguvu zetu aweke tu mkono wake!
kuna sala moja hiv kwenye katekisimu zile za zamaani nilkuwa namskia mamangu akiisali tukiwa tunaslai usiku home

''..................................................uwaangazie watoto wetu tunaposhindwa kuwatazama kwa macho na kuwasiki kwa masikio yetu.................................................................''

BTW umesali na watoto mara ya mwisho lini konnie?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom