Kuna wakati nilikuwa nazungumza na
Mr Rocky hapa na nilimuambia kuwa kwenye ndoa kunahitajika kila mtu ajue majukumu yake,hapo ndoa itakwenda angalau salama kidogo
Siku hizi watu hawajui hata ni kwanini wanaolewa na haya maswali yako yanadhihirisha hilo na sijui kama ukiolewa na mtazamo wako huu hiyo ndoa itakuwaje
Masuala ya kindoa ni magumu hasa kwenye ulimwengu huu usiokuwa na kiasi wala mipaka
Wakati Mungu alipomaliza kuwaumba hawa viume aliwapa majukumu na aliwaambia namna ya kuishi,najua na nye alijua kuwa hakuna maisha ambayo yataweza kwenda hivi tu bila kugawana majukumu miongoni mwa wale wanaoishi pamoja
Pia hakuna pahala popote ambapo watu wanakwenda tu bila kuwa na mtu mwenye kauli ya mwisho,yaani hakuna mahali ambapo watu wanaishi pamoja halafu kila mtu anaamua jambo kama vile atakavyo,haipo na haitakuja kuwepo milele
Kwenye suala la ndoa nalo ni hivyo pia
Mwanamke na mwanaume wapo tofauti kimaumbile,kimaumbile mwanamke ndie huishi na mtoto kuanzia anapozaliwa na hata kabla ya kuzaliwa yeye ndie hubeba ujauzito,hivyo kwa sababu hizi za kimaumbile mwanamke ndie hulazimika kuishi na watoto kwa ukaribu kwa muda mrefu atake asitake ndivyo ilivyo,sasa kuishi na watoto ni pamija na yale yanayowahusu hao watoto
Majukumu yanayomuhusu huyu anaetakiwa kuishi na wtoto muda mrefu nimengi lakini kwa uchache ni haya yafuatayo,huwezi kuishi na mtoto halafu asile.asivae huko kuvaa kunaendana na kufua pia,kuoga n.k
Mtu mwenye majukumu hayo analazimika awe yupo nyumbani muda wote ili aweze kuyatimiza hayo majukumu itakiwavyo,sasa kama huyo anatakiwa awepo nyumbani muda wpte ili atimize majukumu hayo ipasavyo kunatakiwa awepo wa kutafuta hela kwaajili ya manunuzi ya hayo mahitaji ya hiyo familia,hapo ndipo yule asiehitajika kimaumbile kukaa na watoto muda wote anapotakiwa kwenda muyatafuta hayo mahitaji
Hapo ndipo unapouja mgawanyo wa majukumu na ndipo iipokuja kuonekana kuwa kuna kazi za kike na kazi za kiume chimbuko lake hi hayo,suala la wewe kutaka mumeo akuoshee vyombo au akupikie sijui wewe utakuwa unafanya nini,sidhani kama kuna mwanamke mwadilifu ambae atataka mumewe apike halafu yeye akae tu
Jukumu la kutafuta mahitaji ni la mume kimaumbile na kiasili,leo kuna wajinga tu wanataka kulibadili hili ndio maana kuna matatizo mengi sana ya kimalezi kwa watu leo hii
Kama wewe utakuwa unafanya kazi bado sio kigezo cha kutokuyafanya majukumu yako kama mke na wala huo sio utumwa na haijawahi kuwa hivyo!