Kuoa ni kujilipua ujasiri unahitajika

Daby

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
33,648
75,735
Itamsaidia zaidi anayeogopa ogopa kuingia.

Mimi nimesoma na I na J darasa moja kabisa. Tukamaliza wote STD seven I akafeli sisi na J tukaendelea na masomo ngazi zingine.

I akapelekwa shule nyingine akafaulu. hatukuonana naye tena.

Siku ya kwanza kumwona I yupo na rafiki yake N. Rafiki yake I ni mzuri saana akanisalimu mambo shemeji! kumbe tayari ni shemeji kwa kaka yangu. I naye kumbe mpenzi wa rafiki wa kaka yangu.

Miezi mitatu kupita baadae I akapata mimba lakini kizungumkuti kikaja ni ya nani? rafiki wa kaka bado anasoma na familia zao ni marafiki hakuweza kumtaja, akamtaja jamaa mwingine.

Kufupisha stori.

I akajifungua mtoto anafanana na rafiki wa kaka yangu. Kikwazo hawawezi rudiana tena mapenzi yalishakufa.

Classmate wangu J akajilipua akatangaza ndoa kwa I...leo hii wanaishi wanalea watoto. Huyu jamaa ni jasiri saana. Licha ya kuijua historia ya I vizuri lakini akasema hapana liwalo na liwe.

Hivyo, kuna mida ya kujilipua unafumba macho...Asaalam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…