Kunguru wa Dar es Salaam

Kunguru wa Dar es Salaam

al karim

Member
Joined
Aug 13, 2011
Posts
51
Reaction score
63
Salaam wakuu, hawa kunguru Dar wamekuwa sio tishio kwa viumbe wengine kama ndege n.k kwa kula mayai na vifaranga vyao, lakini pia wanasumbua binadamu kwa kelele, uchafu, kula mifugo yao kama vifaranga vya kuku, watu wa mazingira, ecosystem mko wapi jamani?

Binafsi nimejaribu kila sumu hawafi, mitego hawashikwi, msaada please!

Naomba kuwasilisha.
 
Hao Kunguru Wamefika Mikoani Sasa Hivi
Ni kweli,kama sasa hivi wamefika Pwani na Morogoro,na wakiingia tu wale kunguru native wenye alama nyeupe kifuani wanawakimbia maana pamoja na wao kuwa na umbo kubwa hawa weusi wanashambulia mayai na makinda yao. Ni tatizo sana
 
Salaam wakuu, hawa kunguru Dar wamekuwa sio tishio kwa viumbe wengine kama ndege n.k kwa kula mayai na vifaranga vyao, lakini pia wanasumbua binadamu kwa kelele, uchafu, kula mifugo yao kama vifaranga vya kuku...
Maliasili kuna kurugenzi ya kuwadhibiti hao Kunguru na Mkurugenzi wake alikuwa Bw. Linus Chuwa, sina hakika kama bado yupo kwenye hiyo idara ..tambua kwamba kuna nyakati wanapoteaga hao..kutokana na wizara kuweka sumu za kuwadhibiti! Kimsingi kunguru ni " Uchafu"
 
Mbona wanaliwa. Si huku tunakula sana tu sema hawana damu hafu nyama yao ngumu sana.
nimeshuhudia kwa macho yangu mtu akichoma na kumla kunguru hapa hapa Dsm! Ni kweli hawana damu ila wana tone jekundu kwenye kifua/ kidali na nyama yao ni nyeupee!
 
Serikali itangaze inanunua kunguru kwa sh 10,000 kila kungunguru. Wakitenga milioni 151 tu, kunguru watahama nchi.
 
nimeshuhudia kwa macho yangu mtu akichoma na kumla kunguru hapa hapa Dsm! Ni kweli hawana damu ila wana tone jekundu kwenye kifua/ kidali na nyama yao ni nyeupee!
Aisee muda wote ulikua anafatilia hayo mapishi ya kunguru hukuonja kweli?
 
Kunguru wanaliwaaa???
Karibu chakula 🐦

images (13).jpeg
 
Wakitangazwa kama dawa ya nguvu za kiume kwisha habari yao
 
Back
Top Bottom