Mzizi wa Mbuyu
JF-Expert Member
- May 15, 2009
- 7,323
- 6,810
Leo asubuhi nikiwa nasalimiana na mtu nje ya ofisi yangu, akaja kunguru na kutua juu ya kichwa changu.
Kwa muda nikahisi ni mtu amenishika kichwani kwa mkono lakini ilinishtua kidogo maana yule mtu niliekuwa namsalimia alifunua mdomo wake kwa mshangao, nilipoweka mkono wangu kwa nia ya kumgusa Kunguru yule akaruka.
Tukio hilo limeonwa na watu kadhaa waliokuwa jirani...
Sasa kimbembe, mie nililipuuza jambo lile na kuona labda yule kunguru kachanganyikiwa kwa kula sumu mbalimbali majalalani hivyo akapata ujasiri wa kutua kichwani. Lakini watu walioona au kusikia jambo hilo wananijia na ushauri wa kwamba eti siyo bure, lazima lile ni jini/uchawi natakiwa kwenda haraka kwa Waganga wa kienyeji ili waniokoe......... wamekomalia na kutoa mifano lukuki hadi nimeanza kuogopa tofauti na mwanzo....
Jamani nifanyeje?
Kwa muda nikahisi ni mtu amenishika kichwani kwa mkono lakini ilinishtua kidogo maana yule mtu niliekuwa namsalimia alifunua mdomo wake kwa mshangao, nilipoweka mkono wangu kwa nia ya kumgusa Kunguru yule akaruka.
Tukio hilo limeonwa na watu kadhaa waliokuwa jirani...
Sasa kimbembe, mie nililipuuza jambo lile na kuona labda yule kunguru kachanganyikiwa kwa kula sumu mbalimbali majalalani hivyo akapata ujasiri wa kutua kichwani. Lakini watu walioona au kusikia jambo hilo wananijia na ushauri wa kwamba eti siyo bure, lazima lile ni jini/uchawi natakiwa kwenda haraka kwa Waganga wa kienyeji ili waniokoe......... wamekomalia na kutoa mifano lukuki hadi nimeanza kuogopa tofauti na mwanzo....
Jamani nifanyeje?