Me nimekuwa na albamu zao ambazo walizigawa bure.kusema ukweli me sikupenda baadhi ya approach zao kama vile kutukana matusi direct tena ukizingatia Mr Sugu ni mheshima kwa sasa. ila nilipenda idea yao ya kutetea maslai yao na wasanii wengine. sasa najiuliza mbona wapo kimya? ni kwa sababu Sugu amepatana na Ruge? kwani hii ilikuwa ni kwa sababu ya bifu au ilikuwa ni kwa sababu ya kutetea maslahi ya wasaniii.? me ningependa mapambano yaendelee tena show zao zilikuwa zinajaza kwel kwel ... na watu walikuwa wanaburudika. nakumbuka ile ya fiesta ya Mbeya yaani ile ni fundisho kwa hao watu wa fiesta wanaowalipa wasanii wa ndani ujira mdogo. Sugu inuka uendeleze mapambano. ukikaa kimya kwa sababu eti umepatana na Ruge wakati ulikuwa unasema ni ukwel tutakuona ni msaliti na mnafki kwa sisi tuliokuwa tunakupa support kwenye hili jambo