Kuna vurugu kubwa maeneo ya stend ndogo Arusha

PRODA LTD

JF-Expert Member
Oct 20, 2016
1,005
1,333
Wanabodi,

Kuna vurugu kubwa maeneo ya stend ndogo Arusha Jiji la Arusha, vurugu hizi zimesababishwa na hatua ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha kutoa barua za kuwapa vibanda madalali ambao hawafanyi biashara. Mgogoro huu ambao umchukua sura mpya ikiwa ni pamoja na tuhuma za hao madalali kutoa rushwa kubwa kwa RC na Mkurugenzi ili wapendelewe.

Awali ilikubaliwa na baraza la madiwani kuwa utaratibu wa zabuni tena zabuni ya wazi ili kuondoa upendeleo. Zabuni hiyo imetolewa kwenye maeneo mengine yote kasoro stend ndogo tu. Kwanini RC na Mkurugenzi hawataki tena zabuni ambayo wao ndio walipendekeza? Nini hatima ya walionunua hiyo tenda kila mtu alilipa 50,000, tenda haijafika mwisho Mkurugenzi anatoa barua kwa watu wachache.

Tayari maduka yote yamefungwa kufuatia hofu ya vurugu!

Viongozi wa juu ingilieni huu mzozo,

Ni mimi mfanyiabishara

==============UPDATES

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ameliagiza Jeshi la Polisi kufika eneo la stand ambapo muda magari zaidi ya matatu yakiwa yamejaa polisi yamefika maeneo stand ndogo
 
Kuna watu wameteuliwa badala ya kwenda kufanya kazi wapewa wanaenda kuingilia majukumu kama huyu Mkuregenzi wa Jiji la Arusha nashindwa kuelewa kuna nini huko? Kwa nini Mkuregenzi anaingilia maamuzi ya madiwani kuhusu hivyo sijui vibanda kuna siri gani? ? Huu siyo muda wa kufanya siasa wananchi wanahitaji maendeleo
 
Madiwani komaeni, simamieni haki hata kama ni baba bashite kuvunja baraza wacha avunje kwa sababu mnatetea haki
 
Kuna watu wameteuliwa badala ya kwenda kufanya kazi wapewa wanaenda kuingilia majukumu kama huyu Mkuregenzi wa Jiji la Arusha nashindwa kuelewa kuna nini huko? Kwa nini Mkuregenzi anaingilia maamuzi ya madiwani kuhusu hivyo sijui vibanda kuna siri gani? ? Huu siyo muda wa kufanya siasa wananchi wanahitaji maendeleo

Mkurugenzi wa Arusha ni janga!
 
Kuna watu wameteuliwa badala ya kwenda kufanya kazi wapewa wanaenda kuingilia majukumu kama huyu Mkuregenzi wa Jiji la Arusha nashindwa kuelewa kuna nini huko? Kwa nini Mkuregenzi anaingilia maamuzi ya madiwani kuhusu hivyo sijui vibanda kuna siri gani? ? Huu siyo muda wa kufanya siasa wananchi wanahitaji maendeleo
Kwani wewe hujui kazi za mkurugenzi?
 
Hivi Dalali anayezungumzwa hapo ni hawa akina Morris Makoi?
 
Back
Top Bottom