DOKEZO Kuna Uzembe na Mazingira ya Rushwa Hospitali ya Muhimbili, Upanga

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Wagonjwa na ndugu zao wanaingizwa gharama za ziada zisizo na ulazima. Mgonjwa wangu ametoka kanda ya ziwa amefika Muhimbili wiki 2 zilizopita, hadi leo hakuna huduma yoyote ya kibingwa aliyopatiwa. Jumatatu ya wiki ya kwanza wakasema kuna vipimo atafanyiwa na pia madaktari watafanya kikao waone watampa huduma gani, wiki ikaisha.

Wiki iliyopita ambayo ni ya pili wakasema hawajaamua cha kufanya kwakua kuna Daktari hayupo hivyo asubiri Jumatatu ya leo ambayo inakua ni wiki ya 3, tumesubiri inafika leo wanasema inabidi akafanye X Ray kisha majibu yake yatajadiliwa wiki ijayo, yaani wiki ya 4.

Sasa hapa unajiuliza hizi wiki zote 3 hizi gharama ndugu tunaingia ni nini? Je ni kweli walishindwa kumuandikia X ray ile wiki ya kwanza? Na je hawawezi andika vipimo vyote mgonjwa akafanyiwa katika wiki ya kwanza? Au wanatengeneza mazingira ya rushwa?

Mbaya zaidi ni kuwa hakuna mifumo mizuri ya kutatu hizi shida pale.

Tunaomba tusaidiwe
 
Sasa hapa unajiuliza hizi wiki zote 3 hizi gharama ndugu tunaingia ni nini? Je ni kweli walishindwa kumuandikia X ray ile wiki ya kwanza? Na je hawawezi andika vipimo vyote mgonjwa akafanyiwa katika wiki ya kwanza? Au wanatengeneza mazingira ya rushwa?
Je ina maana huo ugonjwa wake ni mpya kabisa hawajawahi kukuta na case kama hiyo wakarejea tu walivyoishughulikia huko nyuma?
 
Yaani hii pia imemkuta mdogo wangu, yupo pale muhimbili hospital week ya pili sasa , na mtoto hali nibaya kila siku wanampga tarehe tu, kwakweli pafikie wawe na hofu ya mwenyezmungu kwani watu wanatoka mbali kuja kufata huduma na ukizingatia hali ni ngumu ukute mpaka kufika hapo amefika kwa michango ndugu,
 
Wagonjwa na ndugu zao wanaingizwa gharama za ziada zisizo na ulazima. Mgonjwa wangu ametoka kanda ya ziwa amefika Muhimbili wiki 2 zilizopita, hadi leo hakuna huduma yoyote ya kibingwa aliyopatiwa. Jumatatu ya wiki ya kwanza wakasema kuna vipimo atafanyiwa na pia madaktari watafanya kikao waone watampa huduma gani, wiki ikaisha.

Wiki iliyopita ambayo ni ya pili wakasema hawajaamua cha kufanya kwakua kuna Daktari hayupo hivyo asubiri Jumatatu ya leo ambayo inakua ni wiki ya 3, tumesubiri inafika leo wanasema inabidi akafanye X Ray kisha majibu yake yatajadiliwa wiki ijayo, yaani wiki ya 4.

Sasa hapa unajiuliza hizi wiki zote 3 hizi gharama ndugu tunaingia ni nini? Je ni kweli walishindwa kumuandikia X ray ile wiki ya kwanza? Na je hawawezi andika vipimo vyote mgonjwa akafanyiwa katika wiki ya kwanza? Au wanatengeneza mazingira ya rushwa?

Mbaya zaidi ni kuwa hakuna mifumo mizuri ya kutatu hizi shida pale.

Tunaomba tusaidiwe
Mgonjwa wako itakuwa yupo wodi ya uchunguzi ni Mwaisela au sewahaji kama sikosei, hawezi kupata matibabu ya kibingwa mpaka wagunduwe tatizo lake ni nini.

Kuna magonjwa ni complicated sana na serikali yetu haijawekeza kwenye vifaa tiba, ila nashauri badala ya kuangaika na xray mgonjwa afanyiwe kipimo cha MRI huwa hakidanganyi.

Labda nikuulize mgonjwa shida kubwa ni nini Kwa unavyohisi wewe?
 
mbona hizo rushwa zipo mda mrefu tumeisha zizoea ila chawa bado wanamsifu ummy
 
Mgonjwa wako itakuwa yupo wodi ya uchunguzi ni Mwaisela au sewahaji kama sikosei, hawezi kupata matibabu ya kibingwa mpaka wagunduwe tatizo lake ni nini.

Kuna magonjwa ni complicated sana na serikali yetu haijawekeza kwenye vifaa tiba, ila nashauri badala ya kuangaika na xray mgonjwa afanyiwe kipimo cha MRI huwa hakidanganyi.

Labda nikuulize mgonjwa shida kubwa ni nini Kwa unavyohisi wewe?
Serikali imwekeza sana kwenye vifaa vya uchunguzi

Itakua maamuzi tu

But utambue pia kama mgonjwa katoka lake zone kwenye Bugando, Basi ana issue kubwa or unique
 
Pole sana ndugu yangu naona maumivu mnayoyapitia siku hizi usiumwe alafu huna hela za matibabu utaomba Ardhi ipasuke Ila madaktari wanatofautiana sana kuna wengine wanapenda sana kuhudumia wagonjwa
 
Back
Top Bottom